Mchezaji huyo mwenye miaka 32 aliingia dimbani mara 189 katika ligi hiyo katika kipindi cha miaka mitano aliyochezea klabu ya Manchester City. (Sky Sports)
Romelu Lukaku, 25, ambaye ni mshambulizi wa Manchester United na Belgium amegusia ndoto yake ya siku zijazo ya kucheza katika ligi Italia ya Serie A. (Gazzetta dello Sport, via Goal)
Meneja wa Manchester City, Pep Guardiola pia huenda siku moja akahamia Italia, baada ya kusema hana shaka ya kuwa mkufunzi wa moja ya vilabu vinavyoshiriki ya ligi hiyo maarufu kama Seria A. (Manchester Evening News)
Inter Milan inajiandaa kufufua azma yake ya kumchukua kiungo wa kati wa Real Madrid na timu ya taifa ya Croatia Luka Modric, 33. (Corriere dello Sport)
Kiungo wa kati wa Ufaransa Tiemoue Bakayoko, 24, huenda akarejea Chelsea baada ya AC Milan kutishia kufutilia mbali makubaliano ya yeye kucheza kwa mkopo kutokana na ''kusindwa katika michezo yake". (Corriere dello Sport via Mirror)