
TUOMBE:Baba yetu Mtakatifu uketiye mahali pa juu sana tunalihimidi jina lako ,tunakuja mbele zako kwa shukurani kwa kutuamsha salama siku mpya na mwezi mpya wa leo , Jumatatu Tarehe 1 OKTOBA 2018.Asante sana maana umekuwa mwena kwetu hata kutuvusha salama ,Tunaomba Toba kwa yote ambayo tumekosa kwa mawazo ,maneno ,matendo Turehemu twakusihi.
Tunaomba mwezi huu tuanze nawe Baba na tumalize nawe hesabu hatua zetu Mfalme wa Amani tuishi maisha ya kukupendeza..Bariki kazi za mikono yetu.Bariki familia ..Bariki Nchi yetu iwe ya Amani.Ponya wagonjwa majumbani na mahospitalini ponya Majeraha yote fariji wafiwa,wape tumaini wajane,wagane,yatima na wote waliovunjika mioyo.Tupe neema ya kulishika na kuliishi neno lako.
Bariki kazi za mikono yetu na inua uchumi wetu.
Tunaombea familia zetu ziongoze ziishi maisha ya kukupendeza na Upendo utawale.Roho Mtakatifu mwalimu wetu tufundishe tuongoze kaa nasi mwezi huu wote uwe wa kukutafuta Mungu kwa bidii.Epusha ajali,maafa..wasafiri waende na kurudi salama nchi kavu,angani,majini tulinde Baba.
Tunaomba yote katika jina la Yesu Kristo Amen
JUMATATU NJEMA NA MWEZI WA OKTOBA MWEMA WA BARAKA NA MAFANIKIO


