Makapuku Forum

Makapuku Forum

Nawasalimu
_91065862_hi035157726.jpeg
 
Tai
Ndege huyu ana kila aina ya sifa ambazo hujitokeza kwa ndege wenzie, pia ni ndege ambaye jina lake linajitokeza hata katika vitabu vya dini, kwa asili ni ndege mkorofi sana, si kwa wanyama wengine anaopenda kuwabughuzi kwa kuwaparua kwa makucha yake, bali hata ndege wenzie huionja shubiri yake, achilia mbali mchezo wake wa kunyang'anya chakula kwa binadamu, ni ndege mwenye nguvu sana kiasi cha kufanya baadhi ya Mataifa makubwa kumtumia kama mnyama wa Taifa, kwa Afrika Egypt wamempa heshima hiyo, na Taifa la marekani wanafanya hivyo pia.
Pamoja na sifa hiyo pia Tai ni ndege mwenye mbio sana, ukimtoa ndege kozi ni yeye ambaye hufuata kwa kukimbia, zipo aina nyingi sana za Tai na kila mmoja wao hubeba sifa yake ya upekee, wapo ambao hukimbia sana, wapo ambao ni wakatili sana, wapo wapole na wengine wengi wenye sifa kem kem.
Unapomuona jicho lake huwa na rangi nyeusi iliyotawala sana, mdomo wake umechongoka, miguu yenye nguvu na kucha kali, mbawa zake ni kubwa sana na ndio humfanya aonekane na kimo kikubwa zaidi pamoja kwamba mwili wake si mkubwa sana, uzito wake hucheza kati ya kg 4 mpaka 8, miaka yake ya kuishi huwa ni zaidi ya 25, na chakula chake kikuu ni nyama, huweza kula mizoga, nyoka wakubwa, wanyama wadogo nk.
 
Ni ndege mwenye sauti nzuri sana awapo angani, inapendeza kutumika kama muito wa simu (ringtone),kwa watengenezaji wa filamu pia sauti yake inapendeza ikitumiwa katika upambaji wa matukio au mwanzo wa filamu, anapotoa sauti yake hiyo pamoja na uzuri wake kwa ndege wenzie huwa ni hofu, mwewe, bundi, kozi hujihadhari kwa kukaa mbali, na sauti yao hiyo hubadirika kutokana na mawasiliano wanayofanya baina yao.
Ndege Tai anaogopeka sana, kiasi kwamba kimvuli chake kionekanapo tuu, wanyama wadogo hukimbia hovyo, na wakubwa wakitafuta njia za kupambana naye.
 
***********SIFA ZAKE ZA KIPEKEE ***********
1. Ni ndege muwindaji sana, kama walivyo wanyama wengine wala nyama mfano simba, chui nk.
2. Mashambulizi yake ni ya kushitukiza sana, akiwa angani hufyatuka kama mwewe aibapo kifaranga, lakini kama atakuwa anawinda kiumbe ambacho kukabiliana nacho si jambo jepesi utamuona akitizama kwa maringo juu ya mti na akifuatilia hatua za kiumbe huyo mdogo mdogo.
3. Pamoja kwamba jicho lake ni dogo lakini uwezo wake wa kuona ni mkubwa sana, kama upo nje tizama juu macho yako yanapoishia kuona yeye huona mara nne zaidi.
4. Tai hawezi kuwinda mwanadamu, lakini akitambua binadamu ni mgonjwa, dhaifu, goigoi atahangaika na wewe tuu.
5. Huweza kubeba viumbe wazito na hufanya hivyo kwa sababu zifuatazo mosi kuhofia usalama wake anaponyakua windo katika jamii ya wanyama hao, pili hubeba kisha huchia kutoka juu lengo likiwa ni kupasua na aweze kula kwa urahisi.
6. Ubabe wake humfanya naye kujenga ngome imara sana, yaani viota ambavyo hujenga vikubwa na huzungusha kwa miiba ili tuu kuzuia nyoka wasiweze kuwafanya wanaye au mayai yao kama mlo.
7. Bibilia inasema kupitia mithali ya kwamba mwendo wa tai ni wa kustaajabisha na kushangaza, kama hilo lilinakutatiza kufahamu nakujuza ya kwamba awapo juu, tai huweza kuganda kwa muda kidogo, na anaweza kuendelea na safari pasina kupiga mbawa zake, akiwa katika mwendo mdogo.
 
8. Tai ni waaminifu katika mapenzi, huishi kwa kusaidiana na kuaminiana sana, aina ya Tai wabaya huwezi kuta dume akitafuta jike mwingine au jike akihangaika na dume mwingine, anapotoka mapenzi yake hubakisha kwa mwenza wake, na mwenza wake asipomuona mwenzie kwa siku mbili hupata hisia ya kwamba huenda mwenzie kauwawa, hapo huondoka na kutafuta mwenza mpyaa.
9. Tai hurudia viota vyao, kila baada ya muda flani wanapotaka kutaga, hufanya ukarabati kidogo tuu.
10. Wakiwa katika kundi wakakuweka kati binadamu dakika 20 nyingi minofu yote watakuwa washamaliza.
Je ungependa kuwaona ndege hawa, Tanzania tunao katika mbuga zetu, Kilimanjaro, udzungwa pia Serengeti ukifika huko utafurahi na roho yako, achana na uzushi ya kwamba Tai anaweza beba binadamu labda umkaribishe wewe mwilini mwako endapo utakuwa una vinono unakula na yeye akakuona
 
Kiboko ni Mnyama ambaye maisha yake amewekeza katika makazi ya aina mbili, huishi nchi kavu pamoja na majini, anatambulika kama farsi wa majini, kwa ufanano ukimtizama vyema huonekana kama nguruwe, ila kwa taarifa yako huyu ni miongoni ya wanyama ambao huishi majini kama ilivyo kwa nyangumi na pomboo, ukimtoa tembo na faru, kiboko ndio mnyama mkubwa kwa wanyama wa ardhini, ni mnyama mtata, mkorofi na mbishi vilivyo, ukimzidi nguvu nchi kavu atakimbilia majini, lakini kwa binadamu kumshinda nguvu si jambo jepesi hata kidogo, ndiyo mnyama mkubwa wa ardhini ambaye ameua binadamu wengi kuliko mnyama yoyote mkubwa kama simba, chui nk.

Macho, masikio na pua vyote vimejipanga juu ya uso wa mdomo wake, ni mnyama pekee ambaye anaweza kuufungua mdomo wake kwa upana kama ameweka msamba hivi, uzito wao huzidi tani moja, na miaka yao ya kuishi duniani ni mpaka 50, wanyama hawa ni wababe sana hivyo si jambo rahisi kuwindwa ingawa simba na mamba huwajaribu, lakini kumbuka si wakubwa huwinda watoto wao, kidevu cha mnyama huyu kimeshamiri ndevu ambazo ni ngumu ngumu sana kama waya, kiasi kwamba akipitisha kwenye mwili wako utaziona tuu damu.
 
Jike wa boko huwa na uzito pungufu kwa dume, mahaba na kuzaa kwake vyote hufanyikia majini, na jike huzaa mtoto mmoja tuu, na kwa nadra sana huzaa wawili, ajabu la wanyama hawa ni kwamba ukiwaona kwenye maji unaweza ukajua wana umoja sana, lakini si hivyo wana tabia ya kufanya maamuzi ya kibinafsi sana, linapotokea suala la kutafuta mlo, pengine ni jike mwenye watoto tuu ndio ataweza kuambatana na wanaye lakini wengine wote kila mmoja ni maamuzi yake.

Muda wake mwingi akishiba huutumia kukaa majini, na kama ulikuwa hujui boko hawezi kucheza na maji kama samaki, hivyo inapotokea suala la kulala hulala ndani ya maji, na hata akiwa usingizi hupanda juu kupumua na kurudi chini ya maji pasina ya kuamka, ndio maana ukiwaona kwenye maji unaweza ona anazama na kuibuka huku akirusha maji juu.
 
***Sifa zake za kipekeeee *****

1. Ndiye mnyama aliyeua wanadamu wengi zaidi kuliko wanyama wakubwa wote.

2. Mashambulizi yake ni ya kushitukiza atakapo kufanya balaa.

3. Sio muoga anapomuona adui yake yeye ndio humfuata.

4. Ni mnyama anayejua sana kuvizia, kwa mfano akiingia katika shamba lako na wewe ndio umefika alfajili hiyo mtaelewena tuu.

5. Wakati wanyama wote maziwa yao yakiwa meupe, boko hapendi mambo ya kuigana yeye maziwa yake ni ya pinki, ajabu jingine boko ni viumbe wanaopatikana Afrika kwa wingi lakini maziwa yao huuzwa ulaya na amerika.

6. Kwenye mahaba kuyaanza si lazima viungo vyao visisimuke ndio dume ampande jike, wanaweza kuanza hivyo hivyo kusisimuka kukawakuta mbele ya safari.

7. Ukimuona usijekaa nakuanza kufikiri utamshinda mbio, na unene wake ule ana mbio balaa.

8. Anaweza kusafiri umbali mrefu kutafuta malisho na kuachana na maji pasina ya shida yoyote, cha ajabu maji yakianza kukauka viboko hufa wengi sana.

9.kiboko ni chanzo cha chakula kwa viumbe wengine, kwa mfano wadudu mbali mbali humtumia kama chakula akiwa hai, hata hivyo ndege nao huwala wadudu hao, nje hapo wawapo majini wanapohasama sana midomo yao mabaki ya chakula huanguka na samaki hula, lakini yeye binafsi hutumia zaidi ya kilo 65 za mimea kama chakula.

10. Kiboko si mnyama mla nyama, hivyo usifikiri anakula samaki wala wanyama wengine, mnyama asiyempenda wa kwanza ni wewe unayesoma, jiulize ulimkosea nini ?
 
Ukikutana naye ufanyaje ? ****

Mnyama huyu ni hatari pasina mfano huua kikatili sana, akikukamata huhasama mdomo wake na kubana mbavu kisha kuanza kutingisha tingisha ikiwa ni ishara ya kuvunja vunja kabisa, usije fikiri kupambana naye ni rahisi hata kama una silaha, kitu pekee cha kumtisha nacho ni moto, ila sijui panga, bastora utaumia tuu, usifikirie kumkimbia ana uwezo mzuri sana wa mazoezi hayo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom