Numbisa
JF-Expert Member
- Dec 12, 2016
- 348,116
- 1,249,274
Farasi ni mnyama mwenye nidhamu sana ukiwa mgongoni kwake ukaanguka hawezi kuendelea na safari mpaka utapozinduka kama ulizimia, lakini pia ni mnyama mwenye upendo hawezi kukupeleka sehemu yenye hatari ukiona anagoma kusonga mbele tambua kama hakuna nyoka basi pana hatari ambayo wewe huioni, Macho yake ni makubwa sana na yana uwezo mzuri wa kunasa matukio vyema mbele na nyuma kwa umakini sana.
Mbali na uwezo huo wa kuona vyema lakini pia farasi yupo vizuri katika kunusa, hamuwezi kukamatwa kizembe na wanyama wakali hasa wale wanaovizia kwa kujificha ukiwa na farasi, unapomfunga ukiona anapiga kelele na kuinua inua miguu kama anapasha ili atimue mbio, haraka sana mtii na mtoke eneo hilo, vinginevyo ataka kamba na kuondoka mwenyewe kisha umalizane na hatari hiyo mwenyewe kama ni simba,chui au mbwa mwitu.
Farasi hula kilo tano mpaka 12 za majani kwa siku, hapa hutegemea sana na umri pamoja na uzito wake, mnyama anayekula nyama anayeweza kumkamata kwa kumfukuza ni duma na mbwa mitu wa kizungu (wolf) pekee, hawa akina simba, sijui fisi nyama yake wataishia kuisikia tuu, mbali na uwezo huo wa kuchanja mbuga farasi pia hupatwa na hisia pamoja na maumivu ukimtendea ubaya usichangae akidondosha machozi na akikushusha kuanzia juu mpaka chini, hapo ujue amekudharau tuu.
Wanyama hawa huuzwa ghari sana, farasi mmoja kwa hapa kwetu hufikia million 5 na ushee, na bei ya farasi hupangwa kutokana na rangi, usitegemee kabisa ukafikiri mkubwa ndio atakuwa bei, rangi ambazo ni adimu ndio huwa ghari zaidi hivyo basi kwa ukijua nyeupe na nyeusi si rangi ghari kumnunua farasi, labda ziwe na mngaro wa kipekee.
Mbali na uwezo huo wa kuona vyema lakini pia farasi yupo vizuri katika kunusa, hamuwezi kukamatwa kizembe na wanyama wakali hasa wale wanaovizia kwa kujificha ukiwa na farasi, unapomfunga ukiona anapiga kelele na kuinua inua miguu kama anapasha ili atimue mbio, haraka sana mtii na mtoke eneo hilo, vinginevyo ataka kamba na kuondoka mwenyewe kisha umalizane na hatari hiyo mwenyewe kama ni simba,chui au mbwa mwitu.
Farasi hula kilo tano mpaka 12 za majani kwa siku, hapa hutegemea sana na umri pamoja na uzito wake, mnyama anayekula nyama anayeweza kumkamata kwa kumfukuza ni duma na mbwa mitu wa kizungu (wolf) pekee, hawa akina simba, sijui fisi nyama yake wataishia kuisikia tuu, mbali na uwezo huo wa kuchanja mbuga farasi pia hupatwa na hisia pamoja na maumivu ukimtendea ubaya usichangae akidondosha machozi na akikushusha kuanzia juu mpaka chini, hapo ujue amekudharau tuu.
Wanyama hawa huuzwa ghari sana, farasi mmoja kwa hapa kwetu hufikia million 5 na ushee, na bei ya farasi hupangwa kutokana na rangi, usitegemee kabisa ukafikiri mkubwa ndio atakuwa bei, rangi ambazo ni adimu ndio huwa ghari zaidi hivyo basi kwa ukijua nyeupe na nyeusi si rangi ghari kumnunua farasi, labda ziwe na mngaro wa kipekee.