Hasa kwa wanachama wote wa nyumba yetu, ambao wananidhamini sana."
Alipoulizwa kuhusu kuwa Freemason wa ngazi ya master (gunge), aliongeza: "Bado nina mshangao," huku akijaribu kukubali uhalisia wa ufanisi wake.
Lakini kikwazo kikuu zaidi pengine kwa wale wanaotaka kujiunga na kundi hilo huwa ni sifa zake za usiri mkuu pamoja na kuhusishwa kwake na ufisadi.
Chakula cha Wahadzabe cha matunda na nungunungu Tanzania
Kadhalika, tuhuma kwamba wanachama wa kundi hilo hufaana na kusaidiana ili kufanikiwa katika taaluma zao mbalimbali pamoja na biashara.
Hili si jambo ambalo Bi Penn analitambua.
"Nimekuwa wa Freemason kwa zaidi ya miaka 40 na sijawahi kuahidiwa chochote na mtu au kumfaa mtu mwingine yeyote (kwa sababu ni wa Freemason).
"Huwa unasikia hadithi hizi, lakini sijawahi kusikia kisa chochote kama hicho katika Freemason kamwe."
Image captionChristine Chapman anasema usiri ndio huwafanya Freemason kuwa wa kipekee
Mwaka 1997, kulikuwa na wito kutoka kwa waziri wa mambo ya ndani wa wakati huo Jack Straw kwa maafisa wa serikali na majaji kufichua kwa hiari iwapo ni wanachama wa Freemason.
Mpango huo ulifutiliwa mbali baada ya Freemason kutishia kuishtaki serikali ya Uingereza.
Christine Chapman, gunge mkuu (grand master) wa Honourable Fraternity of Ancient Freemasons, anasema ingawa wana "maafisa kadha wa polisi (ambao ni wanachama)...sijaona yeyote akisaidiwa [kwa sababu ya kuwa mwanachama]".
Lakini kwa muda mrefu kumekuwa na tuhuma kwamba kundi hilo huhusika katika ulaji rushwa katika idara ya polisi na idara ya mahakama.
Kanuni za kimasoni husema wanachama wanafaa kusaidiana na kufaana na kuweka siri za kisheria za wanachama wenzao. Hii imewafanya wengi kuwa na wasiwasi wa kutumiwa wka kundi hilo kuendeleza ulaji rushwa.