Makapuku Forum

Makapuku Forum

Leo ni siku ya watu wanaotumia mkono wa kushoto huadhimishwa kila mwaka tarehe 13 Agosti.

Siku hii iliadhimishwa mara ya kwanza mwaka 1976.

Haya hapa ni baadhi ya mambo kumi ya kushangaza kuhusu watu wanaotumia mkono wa kushoto:

1.Asilimia kumi kati ya watu wote duniani hutumia mkono wa kushoto, na kiwango hiki kimesalia hivyo kwa muda mrefu. Wanaume wana uwezekano mkubwa wa kuwa wanatumia mkono wa kushoto.

2.Kwa muda mrefu katika jamii nyingi, watu wenye kutumia mkono wa kushoto walichukuliwa kuwa dhaifu. Si ajabu kwamba huenda uliwaona au unawaona watoto wanaochapwa sana kwa kutumia mkono wa kushoto wakila au wakiandika. Katika baadhi ya jamii, kutumia mkono wa kushoto huhusishwa na uchawi.

3.Kumsalimia mtu kwa kutumia mkono wa kushoto kumekuwa kukitazamwa kama kumkosea mtu heshima. Hii ni kwa sababu watu zamani walikuwa wakitumia mkono wa kushoto kujitakasa baada ya kwenda msalani.

4.Bingwa wa tenisi duniani Rafael Nadal alibadilisha na kuanza kutumia mkono wake wa kushoto akicheza - kutokana na imani ya mkufunzi wake Toni Nadal kwamba ingempatia nafuu kiasi akikabiliana na wachezaji wengine uwanjani.

5.Mrengo wa kushoto? Jina hili lilianza kutumiwa miaka ya 1790 baada ya mapinduzi ya Ufaransa na kuondolewa kwa utawala wa kifalme. Wawakilishi wa chama cha kishoshialisto katika bunge walikuwa wakikaa upande wa kushoto wa kiongozi wa vikao. Wat wa mrengo wa kushoto wakati huo walikuwa wakitazamwa kama maadui wa wasomi na watawala.

Mkono 'huathiri' mawimbi ya simu

6.Kwa muda mrefu, dini ya Kikristo ilihusisha upande wa kushoto na maovu. Kwenye picha nyingi za Siku ya Kiama, wale waovu (mbuzi) hutumwa upande wa kushoto nao wale wa kuokolewa (kondoo) hutumwa upande wa kulia. Wakati wa kusulubiwa kwa Yesu, mwizi aliyetubu alikuwa amewekwa upande wa kulia na yule mwovu alikuwa upande wa kushoto.

7.Watano kati ya marais wanane wa karibuni zaidi nchini Marekani hutumia mkono wa kushoto kuandika. Marais hao ni Gerald Ford, Ronald Reagan, George H.W. Bush, Bill Clinton, na Barack Obama.

8.Kuna pahala penye jina Left Hand (Mkono wa Kushoto). Eneo hilo hupatikana katika jimbo la West Virginia na hutokana na kijito cha Lefthand Run.

Haki miliki ya pichaAFP/GETTYMiongoni mwa watu mashuhuri wanaotumia au waliotumia mkono wa kushoto:Rais wa zamani wa Marekani Barack ObamaRais wa Kenya Uhuru KenyattaWaziri Mkuu wa Israel Benjamin NetanyahuMwanamfalme William wa UingerezaMsanii Angelina JolieMwanasayansi Albert EinsteinMwigizaji Tom CruiseMwanamuziki David BowieMwanariadha Paula RadcliffeMwanakandanda PeleMwanaanga za juu Neil ArmstrongMwanasayansi Marie CurieBondia Manny PacquiaoMwanaviwanda Henry FordMwanamuziki Justin BieberMwanamuziki Lady GagaMwanamuziki Marshall Bruce Mathers III maarufu kama EminemMwanamuziki Paul McCartneyMwigizaji Jennifer LawrenceMwanafalsafa AristotleMvumbuzi na mchoraji Leonardo Da VinciSikio la kushoto

Kwa jumla, watu 40% duniani hutumia zaidi sikio la kushoto kusikia, 30% hutumia jicho la kushoto na 20% hutumia zaidi mguu wa kushoto.

Benedict: Nilikuwa ninaabudu shetaniNabii kutoka Malawi anayedai kutenda miujizaNjia bora ya kutimiza malengo yako ya Mwaka MpyaWanawake ambao ni wa FreemasonMabingwa wa tenisi

Ingawa ni asilimia 10% ya watu duniani hutumia zaidi mkono wa kushoto, tangu kuanza kwa enzi ya Open katika mchezi wa tenisi duniani, 23% ya mataji ya Wimbledon ya mchezaji mmoja mmoja yameshindwa na wachezaji wanaotumia mikono ya kushoto.

Image captionMabingwa wa tenisi ambao hutumia mkono wa kushoto

Mada zinazohusianaBarack ObamaUhuru Kenyatta

Mshirikishe mwenzako Unavyoweza kumshirikisha mwenzakoEmailFacebookMessengerTwitterWhatsApp

Rejea mwanzo wa ukurasa

Maelezo zaidi kuhusu taarifa hii

Mwanamume ambaye kidole cha mguu kilihamishwa kwa mkono

13 Julai 2017

Atengeza kitabu cha Quran cha mita 700 kwa mkono Misri

4 Mei 2017

Gumzo mitandaoni

Kanye West akanusha kupagawa wakati alipoulizwa swali kuhusu Trump



Chemsha bongo: Ni mchezaji gani ambaye alisusia mazoezi katika klabu yake kwa madhumuni ya kuihamia Real Madrid wiki hii?

Mwanadada anayesaidiwa kujitoa uhai na madaktari Uholanzi



Mambo muhimu kuhusu watoto wanaofanikiwa kuwa wachezaji soka

Wachezaji walionunuliwa na waliouzwa EPL



Mambo matano ya kuzingatia ukitumia simu
 
Watu wengi duniani hutumia mkono wa kulia kwa shughuli nyingi na si ajabu kwamba vitu vingi huundwa kwa kuwafikiria wanaotumia mkono wa kulia.

Wanaotumia mkono wa kushoto husumbuka sana katika kutumia vitu kama vile mkasi, vitabu au hata kufungua milango.

Fikiria pia kuhusu kipanya katika vituo vya kupokea huduma ya mtandao, mara nyingi utapata kimewekwa upande wa kulia.

Kuna pia viti vyenye sehemu ya kuandikia vyuoni, ni vichache sana hujengwa kwa matumizi ya watu wanaotumia mkono wa kushoto. Inakadiriwa kwamba kati ya watu asilimia 10 hadi 13 duniani hutumia zaidi mkono wa kushoto.

Chimbuko la Illuminati na dhana kuhusu nguvu zaoPapa Francis anataka sala ya Baba Yetu irekebishweRais wa nchi ya watu wawili afariki akiwa Israel
 
Miongoni mwa watu mashuhuri wanaotumia au waliotumia mkono wa kushoto:

Rais wa zamani wa Marekani Barack ObamaRais wa Kenya Uhuru KenyattaWaziri Mkuu wa Israel Benjamin NetanyahuMwanamfalme William wa UingerezaMsanii Angelina JolieMwanasayansi Albert EinsteinMwigizaji Tom CruiseMwanamuziki David BowieMwanariadha Paula RadcliffeMwanakandanda PeleMwanaanga za juu Neil ArmstrongMwanasayansi Marie CurieBondia Manny PacquiaoMwanaviwanda Henry FordMwanamuziki Justin BieberMwanamuziki Lady GagaMwanamuziki Marshall Bruce Mathers III maarufu kama EminemMwanamuziki Paul McCartneyMwigizaji Jennifer LawrenceMwanafalsafa AristotleMvumbuzi na mchoraji Leonardo Da Vinci
Screenshot_20180813-164103.jpeg
Screenshot_20180813-163913.jpeg
 
Sikio la kushoto

Kwa jumla, watu 40% duniani hutumia zaidi sikio la kushoto kusikia, 30% hutumia jicho la kushoto na 20% hutumia zaidi mguu wa kushoto.

Benedict: Nilikuwa ninaabudu shetaniNabii kutoka Malawi anayedai kutenda miujizaNjia bora ya kutimiza malengo yako ya Mwaka MpyaWanawake ambao ni wa FreemasonMabingwa wa tenisi

Ingawa ni asilimia 10% ya watu duniani hutumia zaidi mkono wa kushoto, tangu kuanza kwa enzi ya Open katika mchezi wa tenisi duniani, 23% ya mataji ya Wimbledon ya mchezaji mmoja mmoja yameshindwa na wachezaji wanaotumia mikono ya kushoto.
 
Wanawake wa Freemason wamekuwa wakikongamana kwa zaidi ya miaka 100 sasa - wakifanya matambiko na sherehe sawa na wenzao wa kiume.

Lakini si watu wengi wanaofahamu kuwepo kwa kundi hili. Sasa tunaweza kukufahamisha zaidi kuhusu shughuli za Freemason hawa wa kike baada ya kipindi cha redio cha Victoria Derbyshire cha BBC kuruhusiwa kuzungumza nao.

"Freemason ni nani?" anauliza mmoja wa viongozi wao ambao huitwa master (gunge) katika Kongamano Tukufu la Jumuiya ya Freemason wa Kale.

"Ni mfumo wa kipekee wa maadili ambao umezingirwa na istiari na ishara zenye maana," anajibu Dialazaza Nkela.

Nkela anashiriki katika sherehe ya kipekee ya kumfikisha ngazi ambayo hufahamika kama "shahada ya pili".

Ni sherehe ya kusherehekea kupanda hadhi kwake katika kundi lake.

Kufikia kwake "shahada ya kwanza" kuliadhimishwa kwa kuingizwa kwake katika kundi hilo, shughuli ambayo ilihusisha yeye kuweka wazi "mkono wake wa kulia, ziwa lake la kulia na goti la kulia" kitanzi kikiwa kimewekwa kwenye shingo lake.

Kila sehemu ya tambiko hilo, hudaiwa kuwa na maana yake - ingawa hatukufahamishwa zaidi.



Screenshot_20180813-165456.jpeg
 
Shahada ya tatu" hudaiwa kuwa "pale unapokumbana na kifo ili kuzaliwa upya" na huwakilishwa na "mwisho wa uhai mmoja na kuanza kwa maisha mengine".

Maana ya hili pia, wanaweka siri.

Lakini ufichuzi huu wenyewe ni kidokezo kuhusu shughuli na imani za kundi hili lenye usiri mkuu.

Watu wengi hata huwa hawafahamu kwamba kuna mafreemason wa kike.

Freemason wa kiume - ambao walianza rasmi mikutano yao zaidi ya miaka 300 - wamekuwa wakiangaziwa zaidi.

Kwa sasa huongozwa na mwanamfalme mtawala wa Kent.

Lakini ukijumlisha makundi mawili yaliyopo ya freemason wa kike - Honourable Fraternity of Ancient Freemasons na Order of Women Freemasons, ambayo yaligawanyika mapema karne ya 20 - kuna karibu mafreemason wa kike 5,000.

Image captionWanachama wa kundi la Kongamano Tukufu la Jumuiya ya Freemason wa Kale hukutana katika hekalu kama hili

Wanachama wa Order of Women Freemasons hukutana mara kwa mara katika mahekalu au nyumba kote nchini Uingereza.

Wakati wa sherehe zao, wanawake huvalia gauni ndefu za rangi nyeupe pamoja na mapambo shingoni kuashiria cheo cha kila mwanachama.

Ibada zao huanza kwa msafara kwenye njia kuu ya kuelekea kwenye madhabahu ndani ya hekalu.

Wanachama wa kundi hilo huinama wanapofika pale mbele, ambapo huwa ameketi mkuu wao ambaye hufahamika kama grand master (gunge mkuu).

Screenshot_20180813-165719.jpeg
Screenshot_20180813-165741.jpeg
 
Lugha inayozungumzwa na watu watatu pekee Afrika

Grand master (Gunge mkuu) wa sasa ni Zuzanka Penn ambaye huketi katika kiti kikuu ambacho hufanana na kiti cha enzi.

Huwa kuna maombi wakati wa ibada zao, na wakati mwingine unaweza kuhisi kana kwamba hilo ni kundi la kidini, ingawa Bi Penn anasisitiza wkamba hilo si kundi la kidini.

"Ili uwe wa Freemason, lazima uwe umeamini katika kiumbe (au roho) mkuu," anasema, lakini unaweza kuwa katika "imani (dini) yoyote ile".

"Huwa tuna watu ambao wana imani sana kidini, na wengine ambao hawafuati sana dini - lakini ni watu wa asili mbalimbali, au imani mbalimbali," anasema.

Haki miliki ya pichaORDER OF WOMEN FREEMASONSImage captionWamasoni huvalia mapambo kuashiria vyeo vyao

Wengi wa wanawake wamasoni huwa wana miaka 50 na kwenda juu - jambo ambalo wanataka sana kubadilisha.

Kwa sasa, wanawatafuta wanawake vijana, wakiwemo wale waliojiunga na vyuo karibuni, wawe wanachama.

Mtaalamu wa macho Roshni Patel anafanyiwa sherehe ya kumfanya kuwa wa ngazi ya Mastre katika kundi hilo.

Alijiunga na Freemason miaka saba iliyopita.

Hatukuruhusiwa kuhudhuria sherehe hiyo, lakini tunafahamu kwamba alipewa "heshima" ya kuketi kwenye kiti kile kinachofanana na kiti cha enzi.

"Shughuli yote ya kuwekwa kwenye kiti hicho, ilikuwa ya kuteka hisia sana," anasema, akiondoka.

Screenshot_20180813-165932.jpeg
 
Hasa kwa wanachama wote wa nyumba yetu, ambao wananidhamini sana."

Alipoulizwa kuhusu kuwa Freemason wa ngazi ya master (gunge), aliongeza: "Bado nina mshangao," huku akijaribu kukubali uhalisia wa ufanisi wake.

Lakini kikwazo kikuu zaidi pengine kwa wale wanaotaka kujiunga na kundi hilo huwa ni sifa zake za usiri mkuu pamoja na kuhusishwa kwake na ufisadi.

Chakula cha Wahadzabe cha matunda na nungunungu Tanzania

Kadhalika, tuhuma kwamba wanachama wa kundi hilo hufaana na kusaidiana ili kufanikiwa katika taaluma zao mbalimbali pamoja na biashara.

Hili si jambo ambalo Bi Penn analitambua.

"Nimekuwa wa Freemason kwa zaidi ya miaka 40 na sijawahi kuahidiwa chochote na mtu au kumfaa mtu mwingine yeyote (kwa sababu ni wa Freemason).

"Huwa unasikia hadithi hizi, lakini sijawahi kusikia kisa chochote kama hicho katika Freemason kamwe."

Image captionChristine Chapman anasema usiri ndio huwafanya Freemason kuwa wa kipekee

Mwaka 1997, kulikuwa na wito kutoka kwa waziri wa mambo ya ndani wa wakati huo Jack Straw kwa maafisa wa serikali na majaji kufichua kwa hiari iwapo ni wanachama wa Freemason.

Mpango huo ulifutiliwa mbali baada ya Freemason kutishia kuishtaki serikali ya Uingereza.

Christine Chapman, gunge mkuu (grand master) wa Honourable Fraternity of Ancient Freemasons, anasema ingawa wana "maafisa kadha wa polisi (ambao ni wanachama)...sijaona yeyote akisaidiwa [kwa sababu ya kuwa mwanachama]".

Lakini kwa muda mrefu kumekuwa na tuhuma kwamba kundi hilo huhusika katika ulaji rushwa katika idara ya polisi na idara ya mahakama.

Kanuni za kimasoni husema wanachama wanafaa kusaidiana na kufaana na kuweka siri za kisheria za wanachama wenzao. Hii imewafanya wengi kuwa na wasiwasi wa kutumiwa wka kundi hilo kuendeleza ulaji rushwa.

Screenshot_20180813-170152.jpeg
Screenshot_20180813-170058.jpeg
 
Takwimu muhimu kuhusu Freemason

Haki miliki ya pichaUNITED GRAND LODGE OF ENGLANDImage captionKuna takriban wamasoni milioni sita duniani na zaidi ya 200,000 Uingereza ambao huwa chini ya Jumuiya Kuu ya Wamasoni ya EnglandKuna takriban wamasoni 4,700 wa kike Uingereza, ukilinganisha na takriban wamasoni 200,000 wa kiumeWafreemason hukutana katika hekalu ambalo pia huwa wanaliita "lodge" (au nyumba).

Inafahamika kwamba huko ndiko waasi wa kale walikuwa wanakutana wakifanya kazi ya ujenzi wa kanisaHuwa wanavalia aproni maalum za kimasoni, utamaduni unaotokana na imani ya jadi kwamba wamasoni walitokana na waashi, ambao walikuwa wanavalia aproni maalum kujilinda dhidi ya mawe wakifanya kazi ya ujenziNgazi ya "shahada ya tatu" huwa ni ngazi ya mwisho katika kuwa mmasoni kamili. Sherehe ya kuingiza mtu katika ngazi hii huhusisha kuhojiwa vikali, ambapo wazo la kumpa mtu "shahada ya tatu" huwa na asili yake.Mafreemason maarufu ni pamoja na Sir Winston Churchill, Sir Arthur Conan Doyle, Rudyard Kipling, Robert Burns, Oscar Wilde na Peter Sellers

Bi Chapman anasisitiza kwamba usiri wa Freemason hutokana na haja ya kuunda mvuto fulani na pia upekee fulani na si "kuficha uovu fulani".

"Hatuna mipango ya kujaribu kutwaa udhibiti wa ulimwengu, licha ya dhana hizi ambazo huenezwa na watu waongo mtandaoni, na hatujaribu kupindua serikali au mambo kama hayo.

"Tunahitaji kuhifadhi kiasi fulani cha usiri kwa sababi hilo ndilo hufanya kundi letu kuwa maalum."

Screenshot_20180813-170349.jpeg
 
Moja ya mambo maarufu kuhusu umasoni huwa ni salamu zao - na kwa hilo hakuna tofauti kwa wanawake pia.

"Ndio, bila shaka [tuna salamu zetu za kipekee]," anasema Bi Penn, bila kueleza salamu hizo huwa vipi.

Haki miliki ya pichaOTHERImage captionKuna mambo mengi watu huamini kuhusu wamasoni, ikiwa ni pamoja na salamu za kipekee

"Ni siri yetu. Ni lazima ujiunge nasi kisha nitakwambia huwa zinahusu nini," anasema, huku akitabasamu.


Screenshot_20180813-170623.jpeg
 
Dini ya Kiislamu kuipiku ile ya Kikristo kwa ukubwa 2070

Sambaza habari hii Facebook Sambaza habari hii WhatsApp Sambaza habari hii Messenger Sambaza habari hii Twitter Mshirikishe mwenzako

Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionWaislamu wakifanya ibada. Utafiti unasema kuwa dini ya Uislamu inatarajiwa kuipiku ile ya Wakristo ifikiapo 2070

Uislamu ni dini ya pili kwa ukubwa baada ya Ukristo kwa sasa lakini inakua kwa haraka sana.

Hata hivyo hilo huenda likabadilika iwapo mwenendo wa watu wanaojiunga na dini hiyo utaendelea, kulingana na utafiti uliochapishwa na kituo cha utafiti cha Marekani Pew Research Center.

Kulingana na utafiti huo Uislamu unakuwa kwa haraka ikilinganishwa na dini nyengine yoyote ile duniani.

Itaipiku dini ya Kikristo ifikiapo 2070 kulingana na makadirio yake na hivyobasi kuwa dini yenye ufuasi mkubwa duniani

Screenshot_20180813-170913.jpeg
 
Msikiti mkubwa Afrika wajengwa Algeria

Mwaka 2010 taifa la Indonesia ndilo taifa lililokuwa na idadi kubwa ya Waislamu duniani lakini sasa India huenda ikawa na wafuasi wengi zaidi duniani ifikiapo 2050.

Hatahivyo taifa hilo litakuwa na wafuasi wengi wa dini ya Hindu.

Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionPapa Francis ,kiongozi wa kanisa katoliki duniani

Idadi ya Wakristo nchini Uingereza na Ufaransa itashuka kwa asilimia 50 na asilimia 10 ya watu wanaoishi Ulaya wanakadiriwa kuwa Waislamu kufikia 2050.

Albright asema ''yuko tayari kuingia sajili ya Waislamu''

Wanne kati ya Wakristo 10 duniani watakuwa wakiishi katika jangwa la sahara barani Afrika.

Na nchini Marekani mmoja kati ya watu 50 watakuwa Waislamu kufikia 2050.

Screenshot_20180813-171231.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom