Makapuku Forum

Makapuku Forum

Uchaguzi wa hao wenzetu kina mnangagwa matokeo yanategemewa kutangazwa Lini kwa anayefahamu

...kama ilivyo kawaida kwa nchi nyingi a kusini mwa Sahara, ZEC itatangaza matokeo ndani ya siku tano, maana yake Aug 4 watatangaza matokeo ya uraisi ila kwa nafasi nyingine za ubunge na udiwani hayo ni papo kwa papo.

FYI: Mbali ya nafasi ya urais, kuna nafasi 300+ za uwakilishi wa ngazi za ubunge na udiwani. Usisahau pia kuna utaratibu wa 'proportional representation'

Zaidi ya vyama 55 vinashiriki na MDC na Zanu-PF ndivyo nyenye nguvu zaidi.

Kuna wagombea 23 ngazi ya urais, wanaume 19 na wanawake 4.

Mshindi wa ngazi ya urais lazima apate asilimia 50+1 wasipopata utarudiwa


Ni mara ya kwanza waangalizi wa EU na Commonwealth wameruhusiwa kuangalia (observers)

Facts nyingi nimezitoa Aljazeera na Magazeti ya Zimbabwe
 
Asante moudgulf kwa picha nzuri za kuhamasisha utalii (na zaidi kushawishi kina sie kununua simu zenye kamera bora au kama vipi kununua kamera nzuri kama yangu, yeah, nina kamera Panasonc Lumix)
Asante SHAMMA kwa kuwepo hapa, Mgagaa na Upwa karibu, Slim5 ni jambo zuri kukuona hapa kila wakati

Tumosa mimi sijambo na ulisema kuna kitu utaniambia jioni, jioni imepita na usiku ndo huu hapa, bado kipo au kimepotea, asante kwa salamu.


Wadau wote najua mlikuwa na wikend nzuri.

Kuna jipya?
 
Kwa wapenzi wa Soka na historia kidogo tu. Leo mwaka 1966 England walishinda Kombe la Dunia kwa kuwafunga Ujeumani Magharibi bao 4-2

GettyImages-515454342-727637e.jpg

Pichani ni kapteni wa England Bobby Moore akinyanyua kombe na wachezaji wenzake
 
Tafasiri Unavyoweza: Uwakilishi na Uwakala, Kuna Tofauti

Tunajiandaa na uchaguzi mwingine mdogo, kama ubongo wangu unanitendea haki, miaka miwili kabla ya bunge kuvunjwa, utafanyika uchaguzi mwingine endapo mbunge atajiuzuru kwa sababu zilizooneshwa kwenye katiba na sheria ya uchaguzi. Kuna mbunge amejiuzuru wikend ya jana. Kujiuzuru ni haki ya kila mmoja, ikifikia wakati unaona mlionao hamsafiri pamoja basi unashuka na kudandia usafiri mwingine unaodhani unaenda kasi kufikia kile unachokiamini (kama kweli kipo). Hesabu za wanasiasa ni tofauti ni tofauti na uzijuazo, wakisema wanajumlisha angalia vizuri uone alama ya msalaba, usiangalie jibu. Tafasiri unavyoweza.

Tafiti ya mwaka 2016 kuhusu siasa na chaguzi barani Africa iliyofanywa na taasisi ya OD (Open Democracy) ilionesha tatizo kubwa la rushwa katika chaguzi na mbaya zaidi rushwa baada ya uchaguzi ambapo wawakilishi wanahongwa ili kuwa wakala wa chama hongaji (mara nyingi ni chama tawala) kutengeneza namba kubwa ili kupitisha sheria na mambo mengine ya kibunge. Baadhi ya nchi rushwa ilionekana kuwa tatizo kiasi kwamba ni asilimia 5 hadi 6 tu ya waliohojiwa walisema hakuna rushwa wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.

Kumbuka na lazima iingie akilini, chaguzi ni gharama na asikudanganye yeyote, gaharama hizi zinabebwa na mwananchi maskini ambaye anamtegemea mwanasiasa, awe mwakilishi wake katika kuandaa mipango ya kuondoa umaskini kwa jamii.

Bahati mbaya sana mwanasiasa ana mawazo tofauti, hesabu zake ni za ajabu na akipata jibu gaharama za ukokotoaji utazilipa wewe unayenisoma sasa maana mwakilshi makini hawi wakala hata siku moja. hata kama amesimama kwa tiketi ya chama fulani, waliompigia kura ni wananchi ambao wanahitaji mwakilishi na si wakala., tafasiri unavyoweza
 
Asante moudgulf kwa picha nzuri za kuhamasisha utalii (na zaidi kushawishi kina sie kununua simu zenye kamera bora au kama vipi kununua kamera nzuri kama yangu, yeah, nina kamera Panasonc Lumix)
Asante SHAMMA kwa kuwepo hapa, Mgagaa na Upwa karibu, Slim5 ni jambo zuri kukuona hapa kila wakati

Tumosa mimi sijambo na ulisema kuna kitu utaniambia jioni, jioni imepita na usiku ndo huu hapa, bado kipo au kimepotea, asante kwa salamu.


Wadau wote najua mlikuwa na wikend nzuri.

Kuna jipya?
Mkuu Obe nasema Ahsante sana!
 
Muziki: Pamoja MmojaMmoja

....nimekaa mahali wikend hii na kama unavyojua tena ilikuwa ni juma la mshahara kwa wafanyakazi, kifupi walikuwa na hela ya kuangusha moja moja na bahati mbaya sana na mimi ni mmojawapo wa waliokuwa na hela wikend hii. eeh, wikend hii tu maana siku hazigandi hata kama zinaenda polepole. Basi nimekaa sehemu niliyokuwepo, mafichoni kiasi kwa usalama wangu binafsi na nikaona nisiache kukusalimia wewe mdau unayelifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo.

Muziki sasa, ni Jumatatu na mambo ni matatumatatu na kwa hiyo tuko pamoja mmojammoja.

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom