Makapuku Forum

Makapuku Forum

TUOMBE

Mungu wetu na Bwana yetu Asante kwa Neema yako kutupa siku hii ya leo JUMAPILI TAREHE 10 JUNI 2018 Ni Furaha yetu kuona Unazidi kuachilia Neema yako ya Uzima. Tumenyenyekea mbele zako Mungu kuonesha utii wetu kwako. Tunaomba Baraka zako,futa majonzi,masikitiko kwa kila Moyo Iliyokata tamaa na kuachilia Furaha na Pendo litokalo kwako. Kutana na haja za mioyo yetu na kuzidi kutufundisha Kweli yako, Bariki kutoka na kuingia kwetu. Mikono yetu ikakuzalie matunda yadumuyo. Fungua Uchumi wetu,asiye na kazi apate kazi. Mungu wakumbuke wagonjwa na wengine wote wanaotafuta kukuona, wakutane na uso wako. Mioyo yetu ikutukuze wewe sasa na hata milele na ibada zote siku ya leo UONEKANE MFALME WA AMANI NA MFARIJI WETU MUNGU USIYESHINDWA WATANGULIE WATUMISHI WA MUNGU WOTE WATAKAOSIMAMA MADHABAHUNI POPOTE ROHO MTAKATIFU AWEPO AMINA.

SIKU NJEMA,JUMAPILI NJEMA,IBADA NJEMA
Ameni mpendwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom