Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tafasiri Unavyoweza: NiUSiU

Inawezekana kichwa cha habari hukielewi, sio shida hata mimi kilinichanganya hasa baada ya kuamua kuchukua herufi za mwanzo katika maneno niliyochagua yawe kichwa cha habari cha makala haya mafupi. Bila kuyafupisha kichwa kitasomeka Ni Uchaguzi Si Ubaguzi, kuna tofauti sana katika haya maneno. Uchaguzi ni utaratibu uliowekwa kwa ajili ya kumchagua mtu/kikundi cha watu kushika madaraka ya kisiasa, na ubaguzi nao ni utaratibu unaweza usiwe wa kimfumo bali wa kibinafsi ambao unalenga kulitenga kundi moja dhidi ya jingine. Ubaguzi kama ulivyo uchaguzi, ukifanyika kimakosa na kwa upendeleo unaathari sana kwenye jamii. Waulize wabaguzi kule SA na wote waliocheza na uchaguzi hapa kwa majirani zetu.

Uchaguzi umekwisha kwa hapa kwetu japokuwa ni ukweli kwamba mwisho wa uchaguzi mmoja ndiyo mwanzo wa uchaguzi mwingine, kwa sasa vyama vinapiga jaramba (niwe mkweli hapa) CCM wanafanya kampeni sasa na wapinzani wao hawana uwanja wa kufanya kampeni kwa sababu mikutano imewekewa vizingiti visivyojali kuwa kuna watu wanaishi, kazi yao ni siasa. Tutafika tu.

Kauli ya mkulu kuwa mikopo ya elimu ya juu italenga zaidi wale waliosoma shule za serikali. Kwa hisia kupendelea shule za serikali inasikika vizuri sana lakini nani hajui kuwa shule zinaozoongoza kwa kufanya vibaya! Walimu maslahi duni, vifaa vya kufundisha na kujifunzia ni duni, na mzazi anajipiga amtafutie mwanaye shule binafsi ambayo ina mazingira mazuri ya kujifunza, analipa kodi sawa sawa na mzazi anayesomesha shule za serikali ila inapokuja kuingia chuo ndipo mizengwe inaanza. kwanini? Ni udumavu au kuvimbewa kwa kushiba uchaguzi wenye ubaguzi. Tafasiri unavyoweza
 
Muziki: Nitumie Nisome

...nimekumbuka tu kitu miaka hiyo wakati ndo mitandao inashamiri mijini. Ilikuwa mwendo wa kupeana website ili mmoja atembelee kjwa sababu mwingine keshatembelea na kaona uzuri wa ule mtandao sasa anaaamua kukutumia nawe utembelee. Lilikuwa ni jambo zuri na limenikumbusha kukusalimia wewe Kapuku mwenzangu na kukupa hongera kwa mchana uliokuwa nao. Mimi sijambo asante kwa kutouliza.

Muziki sasa, leo ni 2 in 1 ambapo aunt yangu Shunie kaomba muziki na bahati nzuri wimbo wenyewe unapendwa pia na Tumosa mama JJ. Tuburudike na endeleeni kupokea salamu nyingi sana toka kwa BH, yule mwanamke ninayempendaga upeo.

 
Muziki: Nitumie Nisome

...nimekumbuka tu kitu miaka hiyo wakati ndo mitandao inashamiri mijini. Ilikuwa mwendo wa kupeana website ili mmoja atembelee kjwa sababu mwingine keshatembelea na kaona uzuri wa ule mtandao sasa anaaamua kukutumia nawe utembelee. Lilikuwa ni jambo zuri na limenikumbusha kukusalimia wewe Kapuku mwenzangu na kukupa hongera kwa mchana uliokuwa nao. Mimi sijambo asante kwa kutouliza.

Muziki sasa, leo ni 2 in 1 ambapo aunt yangu Shunie kaomba muziki na bahati nzuri wimbo wenyewe unapendwa pia na Tumosa mama JJ. Tuburudike na endeleeni kupokea salamu nyingi sana toka kwa BH, yule mwanamke ninayempendaga upeo.

Binamu jamani naomba uniwekee na audio ndio nilikuwa naitaka sana binamu yangu
 
Binamu jamani naomba uniwekee na audio ndio nilikuwa naitaka sana binamu yangu
Nimejaribu kuangalia google music (Play Music) na Pandora zote zinanipeleka kwenye video clip, hivyo shukuru kwa hichi ulichopata kwanza ni kizuri unaweza hata kujifunza mastyle ya kucheza maana nyie watoto wa siku hizi kucheza ni sifuri
 
Muziki: Nitumie Nisome

...nimekumbuka tu kitu miaka hiyo wakati ndo mitandao inashamiri mijini. Ilikuwa mwendo wa kupeana website ili mmoja atembelee kjwa sababu mwingine keshatembelea na kaona uzuri wa ule mtandao sasa anaaamua kukutumia nawe utembelee. Lilikuwa ni jambo zuri na limenikumbusha kukusalimia wewe Kapuku mwenzangu na kukupa hongera kwa mchana uliokuwa nao. Mimi sijambo asante kwa kutouliza.

Muziki sasa, leo ni 2 in 1 ambapo aunt yangu Shunie kaomba muziki na bahati nzuri wimbo wenyewe unapendwa pia na Tumosa mama JJ. Tuburudike na endeleeni kupokea salamu nyingi sana toka kwa BH, yule mwanamke ninayempendaga upeo.

Mm nmemiss huyo BH jamani hebu tuletee atusalimie mwenyewe
 
..tupo naye hapa tunafanya mambo ya msingi. Sasa hivi ninatumia simu yake, ukiona nimeandika mambo ya maana sana ujue ni yeye ila ukisoma mafindofindo basi jua ni mimi.

Hajambo na anazidi kung'aa tu na hzi mvua anazidi kurutubika tu
Anarutubuka au una mrutubisha!!

Mpaka mvua zikikata hakikisha awe karutubika vizuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom