Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kwa Taarifa yako Tu

Tumeanza wiki (juma) la kuwakumbuka na kutambua kazi nzuri inayofanywa na wauguzi katika hospitali, zahanati na vituo vya afya ambavyo tuko karibu navyo.
Tenga muda wako wiki hii nzima kkumwambia muuguzi (nurse) asante kwa kazi kubwa anayoifanya kutuhudumia bila kujali uchovu anaokuwa nao kwa sababu ya kuhudumia watu wengi.

Nakumbuka enzi hizo naenda hospital na nurse ananidunga sindano naugulia maumivu na yeye ananiambia pole huku akitoa tabasamu la ukweli kabisa ambalo ni nadra sana kuliona kwa mwingine isipokuwa kwa muuguzi na mama/baba.

kiweza weka chochote unachokumbuka kuhusu kazi nzuri ya muuguzi.

4.jpg

Hawa ni wauguzi wa hospital ya Bugando (Picha nimeitoa BMG leo)


3.jpg
 
Kwa Taarifa yako Tu

Tumeanza wiki (juma) la kuwakumbuka na kutambua kazi nzuri inayofanywa na wauguzi katika hospitali, zahanati na vituo vya afya ambavyo tuko karibu navyo.
Tenga muda wako wiki hii nzima kkumwambia muuguzi (nurse) asante kwa kazi kubwa anayoifanya kutuhudumia bila kujali uchovu anaokuwa nao kwa sababu ya kuhudumia watu wengi.

Nakumbuka enzi hizo naenda hospital na nurse ananidunga sindano naugulia maumivu na yeye ananiambia pole huku akitoa tabasamu la ukweli kabisa ambalo ni nadra sana kuliona kwa mwingine isipokuwa kwa muuguzi na mama/baba.

kiweza weka chochote unachokumbuka kuhusu kazi nzuri ya muuguzi.

4.jpg

Hawa ni wauguzi wa hospital ya Bugando (Picha nimeitoa BMG leo)


3.jpg
Wauguzi popote mlipo shikamooni
 
Tafasiri Unavyoweza: Tuna Safari Ndefu

...ndiyo, safari ni mwendo/hatua ndivyo wanavyosema wengi na hili halina ubishi. Leo safari ndefu nitaangalia hali ya ulemavu katika jamii yetu. Ulemavu (disability) ni ile hali ya kuwa na changamoto iwe ya kimwili, kiakili au kijamii anayokuwa nayo mtu na inamfanya asitimize majukumu kama binadamu 'aliyekamilika'. Jamii yetu bila kupepesa macho bado ina safari ndefu sana katika kuweka usawa na kuhakikisha angalau kila mlemavu anapata haki zake kama mwananchi mwingine iwe ni haki ya kielimu, ajira, matibabu, pamoja na fursa nyingine za kijamii. Tafasiri unavyoweza.

Takwimu zilizoandikwa na FikraPevu kuhusu wanafunzi walemavu mwaka 2017 zinaonesha kuwa asilimia 48 ya walemavu nchini kwetu hawajui kusoma, kuandika na kuhesabu. Hii ni hali mbaya sana kwa sababu katika dunia ya leo usipozijua angalau hizi K tatu nani utaweza kuwasiliana naye achana na ukweli kwamba utawezaje kufanya kazi bila hizi dhana muhimu. Sheria ya ulemavu (the Persn with Disabilities Act 2010) inatabainisha kuwa ni kosa kumnyima mlemavu elimu. tuna shida kubwa ya miundombinu mizuri mashuleni ya kumwezesha mwanafunzi mlemavu kujifunza na kufaulu. Majengo, walimu na vifaa kama vipo basi havifanyi kazi na havitoshi wacha walimu wenye mafunzo juu ya ulemavu. si ajabu matokeo ya kidato cha nne mwaka jana, shule ya walemavu kanda ya kusini ilishindwa kufaulisha mwanafunzi hata mmoja, wote walipata sifuri. Hiki si cha kufumbia macho.

Tuna safari ndefu na itazidi kuwa ndefu endapo juhudu za kuweka miundombinu sahihi kuwawezesha walemavu kupata elimu hazitakuwa moja ya agenda za kitaifa. Tusiishie kuhimiza viwanda ilhali hatuwawezeshi walemavu kuwa sehemu ya maendeleo ya viwanda vyetu. tafasiri unavyoweza.

Natangaza maslahi: Nimesoma shule mchanganyiko yenye walemavu, na nikapata 'mchongo' wa kutoka nje ambako nimefanya kazi katika university idara ya teknolojia saidizi (assistive technology) kuwawezesha walemavu kupata elimu bila kuwatenga darasani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom