Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tafasiri Unavyoweza: Maandamano Yamelipa

Hakuna ubishi kuwa leo maandamano yamefanyika, ndiyo yamefanyika tena kwa kiwango kikubwa sana. Maandamano haya unaweza kuyatafasiri unavyoweza nami nitakueleza kuwa wakati wewe ulikaa ndani leo polisi wengi kwa karibu wiki nzima hii walikuwa wakiandamana (wenyewe wakiita mazoezi) kumuunga mkono dada jasiri (hata kama hukubaliani na baadhi ya mbinu zake za kuwasilisha ujumbe) Mange Kimambi. Ukiwaacha polisi walioandamana kwa wingi sana, raia wengi walikuwa na ufahamu wa tukio la maandamano ya leo na kwa kuunga mkono maandamano haya waliandamana kifikra. Tafasiri unavyoweza.

Ujumbe umetumwa na umefika kikamilifu, ni bahati mbaya sana kuona rais na serikali inayojinasibu kufanya mambo mazuri inakuwa katika nafasi ya kujihami zaidi kuliko kujitokeza nje na kusikiliza yale ambayo yanasemwa kuwa haifanyi. Haki ya kujieleza kama ilivyo haki ya kuandamano na mikutano ni kitu kilichokubaliwa ndani ya katiba, si hisani ya rais, au chama kilichoko madarakani. Ni ushamba mkubwa kudhani kuwa mtu mmoja au kikundi cha kisiasa kinaweza kuamua tofauti na katiba. Ni suala la muda tu, bubu atasema kwa kupaza sauti na hapo ndo walioshika madaraka watapazwa kwa kasi ya kobe, waugulie maumivu kwa kila hatua. Sio utabiri huu ninaoandika, naandika utafasiri unavyoweza.

Asanteni sana jeshi la polisi kwa kuandamano na kumfanya Mange na hoja zake ziwe na mashiko, bahati mbaya sana wakati mnaandamana hakukuwa na chombo kingine cha kuwazuia kuandamana
Hakuna kitu kibaya kama kujiona ww ndio sahihi.
 
Muziki: Heko ya Kuzaliwa shululu

Nafurahi hujaandamana barabarani leo, ni jambo zuri kufanya kilicho sahihi kwako na ndiyo maana Tumosa aka mama JJ kaamua kumtunuku shululu wimbo mzuri siku ya kukumbuka kuzaliwa kwake. nami ninakusalimia kapuku na kukutakia wakati mzuri wakati ukitafakari siku ya Ijumaa itakavyokuwa.

Burudika na muziki na tumtakia Shululu heko ya kuzaliwa

Reggae is music that i need.. [emoji444] [emoji445] [emoji445] [emoji445]
 
Hakuna kitu kibaya kama kujiona ww ndio sahihi.

...Maulana katupa utashi na uwezo wa kufikiri na hii ni tunu ambayo haijawahi kuondolewa na yeyote iwe enzi za Mongol ya Genghis Khan ambaye pamoja na maguvu yake alikuwa na uvumilivu kwa wale anaowaongoza au alikwapua himaya zao itakuwa zama za leo!

Yana mwisho.
 
...Maulana katupa utashi na uwezo wa kufikiri na hii ni tunu ambayo haijawahi kuondolewa na yeyote iwe enzi za Mongol ya Genghis Khan ambaye pamoja na maguvu yake alikuwa na uvumilivu kwa wale anaowaongoza au alikwapua himaya zao itakuwa zama za leo!

Yana mwisho.
Ukiishi kwa kufumba macho na kuwakataa watu wasikushike mkono tegemea kuingia topeni ama kuzama shimoni..
 
Back
Top Bottom