Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki wa Mdhamini: Wasilisha Hisia Acha Wasiwasi

Sitaki kumsemea mtu, si unajua kwanini, kwanza huwa nakuwa wa mwisho kujua vitu humu ambavyo wote mnavijua tangu jana na kingine japo ni tuhuma lakini kuna mdau kasema mimi ni domo zege. sasa niliposoma list ya domo zege nikapata njaa maana nikajua zege ni chipsi yai, nikajiuliza hilo zege limewekewa na chachandu au lina mishkaki. Lahaula nilikuwa mbali na ukweli kumbe domo zege ni ile changamoto ya kutongoza. Mmmmh, hebu jiulize , muulizeni BH kama mimi ni domo zege. Maana nimemuimbisha mwaka wa 7 huu hadi nilipopendana na mpendwa wangu, kipenzi changu wa ukweli. Sijitetei maana tatizo langu sio udomo zege ila ni kutokubaliwa kabla ya kukutana na kipenzi changu mnayemjua humu.

Muziki wa mdhamini unaletwa kwenu na Shunie aunt yangu ninayemfagilia sana. Mimi na yeye hatuchukiani na tunafurahiana mno na wote mnalijua hilo. Mnasalimiwa na anko wangu mkubwa yule anayempenda aunt yangu achana na huyu mdogo Lyon Lee nyumba nyingi, juzi kaenda kufumania mchepuko wake kilichomkuta atawasimulia asubuhi au atajidai kukaa kimya kuepusha shari la penzi jipya


Ahsante sana mtaasisi
 
ZABURI 4

4.Mwe na hofu
wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.

8.Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara,Maana wewe Bwana peke yako Ndiwe unijaliae kukaa salama

SHALOM..SHALOM
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom