
Baba yetu na Mungu wetu tunakushukuru sana kwa wema wako ,fadhili zako na Ulinzi wako hata kutufikisha siku hii njema sana ya leo JUMATATU , 20 NOVEMBA ,2017 Baba Sifa Shukurani Heshima Utukufu ni kwako Mfalme wa Amani.
Tunakuomba, utusamehe makosa yetu yote tuliyotenda kwa mawazo maneno matendo na kutotimiza wajibu mbalimbali
Tunaomba Utulinde siku ya leo na wiki nzima Utukinge na ajali na hatari zote za mwili na za roho Ukawatume Malaika Walinzi Kila tunapokuwa Baba na Utupe nguvu ya kukutumikia wewe.
Wabariki watu wote katika Familia zetu, Wasaidizi wetu, wanandoa ,Watoto, Ndugu Jamaa ,majirani na Marafiki Damu ya Yesu itufunike.
Walinde wenye mahitaji na shida mbalimbali Ponya Wagonjwa Fariji Wafiwa Wajane Wagane Yatima Wafungwa na wote Walioumizwa na kukata tamaa wape Tumaini Baba.
Walinde Wasafiri wote Majini ,Nchi kavu, Angani uwe Dereva Utufunike kwa Damu yako ya Thamani Tutokako na Tuendako
Bariki kazi zote za mikono yetu Ukaonekane kwetu katika Ajira ,Ujasiriamali Biashara tupate riziki halali na tukutumikie vyema.
Mungu wetu na Baba yetu tunakuomba utusaidie tuwe na Upendo wa kweli tukawe msaada kwa wenzetu kimwili na kiroho na tusipungukiwe Baba tuitende kazi yako bila kuchoka wala kukatishwa tamaa..Tunayo mipango mingi mbele yetu Baba tunaomba UKATUFANIKISHE ,kila jambo tulilopanga lifanyike kwa utukufu wa jina lako takatifu
Asante Baba kwakuwa Unatupenda na Utatutendea sawasawa na Mapenzi yako.
Tunaomba haya yote kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu amen.Damu Takatifu ya Yesu ikanene mema wiki nzima kuanzia leo. Amen.
SIKU NJEMA,WIKI NJEMA YENYE BARAKA TELE
