Makapuku Forum

Makapuku Forum

84621a2e6ab1d9906b3a55ab5f1b7f1c.jpg
Safi sana
 
Tuombe


Bwana Yesu asante kwa ljumaa njema ya leo.

Asante kwa ulinzi wako kwetu Mungu Mkuu

Umetulinda Baba
Bwana wa majeshi

Ni wengi walitamani kuiona hii siku lakini hawakuweza kufika.

Baba siku ya leo ni siku ambayo wengi tunakuwa katika maombi

Mungu ninakuomba katika Jina la Yesu Kristo Maombi yetu Bwana yakawe ni manukato mazuri mbele zako.

Kumbuka wenye shida mbali mbali
Taabu na mateso ya kila aina EeeMungu ukatukumbuke

Angalia ndoa ambazo hazina amani wala furaha nyoosha mkono kwao Baba

Mungu warudishie upendo wao wa kwanza

Ambao hawajakujua wewe Mungu wa kweli katika jina la Yesu Kristo Bwana ukawaokoe.
Kumbuka wamama wanaohitaji Watoto
Bwana ukafungue matumbo yao.
Wanafunzi, wagonjwa ,Yatima na wajane
wagane,wakumbuke ee Yesu
wasafiri ,nchi kavu, majini ,angani uwe dereva
Nimeomba haya nikiamini yamekuwa ni katika Jina la Yesu Kristo wa Nazareth

Roho Mtakatifu kaa nasi siku zote za maisha yetu..

Amina
 
MKE JEURI

(The Wife's Tyrant)

Sehemu Ya 33

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487

Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←

"aaahhhh mr Rajabu"
"ndio boss"
"ivi tulikuwa tunamdai kiasi gani"
"aahh hapa imeandikwa milioni mia moja na hamsini (Milioni 150)"
"aaahhh mary... Mimi nilishasema pesa ndogo ndogo kama hizo mpatie Sharbiny afatilie... Mimi nileteeni wale wenye kuanzia milioni 500 kwenda mbele sio milioni 100"
"Samahani boss... Nilijua boss sheby atakuwa bize, mana alipelekewa kazi na rose muda sio mrefu"
"mpelekee atajua aanze ipi amalize ipi"
Kitendo cha mary kuambiwa apeleke documents za benki kule ofisini kwa sheby kwake ilikuwa ni furaha sana katima moyo wake....
"leo lazima nionyeshe hisia zangu kwake"
Aliongea Mary huku akiruka ruka kwa furaha ya hali ya juu,... Mary alishusha sketi yake vizuri mana haitaji kumtaga kwa lolote lile, ispokuwa ampende mwenyewe na sio kumtamani kimapenzi... Mary akiwa kafika mlangoni moyo ukiwa unamwenda mbio kwa furaha ya kuja kwa sheby akiwa peke yake, mana kawaida anaepeleka documents ni rose, sasa muda huo rose alikuwa hayupo, hivyo mary akachukiwa nafasi hio, sasa ndio mana anajiskia raha sana....
"sheby naomba unielewe hata kwa macho yangu tu"
Mary aliongea hivyo huku akikiminya kitasa cha mlango,.. Tena kwa wenge aliokuwa nalo la kukutana na sheby, hata hodi hakupiga kwa furaha alionayo kwa siku ya leo

ENDELEA..........

Wakiwa katika moja ya mapenzi mazito baina ya sheby na rose, na wakati huo wametoka pale ofisini wameingia kwenye chumba cha kupumzikia, yaani hata kule kwa baba yake sheby pia ofisini kwake ni dabo rum, yaani ni vyumba viwili, cha kwanza cha kazi cha pili ni cha kupumzikia pale mtu anapochoka na hakuna kazi,... Sasa huko ndani rose alikuwa mweupeee hana hata chembe ya nguo, shwby ndio kabisa yani Usiseme na zakaria yake ilikuwa imesimama wima, rose ni mtoto wa mjini aliishika na kuanza kuimba kilugha chao... Unajua kuimba kilugha wewe?... Sasa rose wakati akiwa anaimba juu ya mic ya sheby.. Walistuka kuskia mlango umefunguliwa kwa nguvu zote na mtu kuingia ndani,....
"itakuwa ni baridi baby"
Aliongea rose huku akiendelea kuinyonya zakaria ya sheby....

Sasa kumbe huku aliofungua alikuwa ni mary, mkononi alikuwa kashika documents za banko ili sheby afatilie hio pesa.....
Sasa mary kufika hajakuta mtu,.. Sasa akawa anageuka ili arudi ofisini kwake afu atazileta kwa wakati mwingine, lakini sasa ile anafanikiwa tu kugeuka, mary alibahatika kuiona chupi ya rose, kumbe waliiacha pale mezani,...
Documents zote zilimdondoka mary na kufanya sheby ashtuke tena
"baby una presha ya nini lakini"
"nahisi kuna kitu"
"hakuna kitu baby"
Rose alizidi kumpotezea sheby asiwe na wasiwasi wowote kuhusu pale ofisini,... Sasa huku mary alipoiona ile chupi aliijua ni chupi ya rose na istoshe alisikia visauti sauti huko ndani... Mary kwa hasira aliokota documents zake na kuondoka... Lakini alipofika kwenye kordo fulani hivi alimwona baba yake sheby anakuja katika ofisi ya sheby... Huezi amini mary kaumia sana moyoni mwake lakini karudi ofisini na kuichukuwa ile chupi ya rose ili baba yake sheby asije kuiona, mana rafiki yake angefukuzwa kazi, kwa kitendo hicho, sasa ile anatoka tu akakutana na boss mlangoni
"boss,.. Boss sheby katoka"
"aaahhh hayupo"
"ndio... Nilimuona katoka boss"
"aahhhh ok basi akija umwambie nimetoka kidogo sawa"
"sawa boss"
Baba yake sheby aliondoka zake na kupotelea zake.. Na mary nae hakutaka kubaki....

BAADA YA NUSU SAA KUPITA

Sheby alionekana kutaka penzi tena yaani hapo sijui ni raundi ya ngapi.. Rose alikuwa hataki tena kwasababu keshachoka afu mbaya zaidi ni ofisini hivyo rose alitaka kumtoa hamu tu, sasa sheby kanogewa anataka tena,..
"please sheby, kumbuka ofisi zipo wenyewe eti Please"
"sasa kwanini unionjeshe lakini"
"nitakupa tukitoka, please nielewe baby"
"ok poa"
Rose na sheby walianza kuvaa nguo zao lakini kwa upande wa rose nguo moja haionekani,...
"baby chupi yangu ipo wapi"
Aliuloza rose huku akiwa na wasiwasi juu ya nguo hio kitoonekana
"si uliiacha kule mezani wewe"
"oooohhh yes, nimekumbuka baby"
Basi rose alitoka kwa furaha mpaka pale mezani lakini bado hakuiona
"boss, mbona siioni"
Aliongea rose huku wasiwasi ukirudi tena kwa mara nyingine....
"khaaaa we si uliiweka hapa.... Aaahhh mimi ndio mana spendi kufanya mapenzi ofisini ona sasa ishakuwa tabu hiii"
"lakini boss chupi ilikuwa hapa"
"lakini mi nilikwambia tukiwa ofisini achana na mapenzi, ona sasa kilichotokea"
"nisamehe boss"
"sasa hata nikikusamehe haijalishi kitu, bado nguo haionekani"
Rose alitoka mbio mbio mpaka ofisini kwake na kumkuta mary kajiinamia kwenye meza yake,..
"mary... Mary.... We mary mambo"
Rose kwa wenge alilokuwa nalo alijikuta anamsalimia tena mary na wakati wamekuja wote na walikuwa wote muda sio mrefu...
"eti uenda ofisini kwa boss sheby"
"niende kufanya nini na wakati mpeleka documents ni wewe"
"ok.. Hakuna documents zingine za kupeleka"
Rose hakutaka kumwambia Mary kile kilichotokea na anachokitafuta...
"nilizipeleka kwa boss mkubwa, na alizipeleka kwa mtoto wake"
Rose alishtuka almanusura azimie
"ati unasemaje mary"
"kwani boss mkubwa hatakiwi kuingia kwa boss mdogo"
"aahhh ok... Ni sawa hakuna shida"
"kwani kuna nini"
"ah ah hakuna kitu"
Rose alikaa kimya na wakati huo hana chupi kavaa sketi tu basi...
"sasa si ukae..."
Mary alikuwa anajua rose anaogopa kuwa huenda hio chupi kaichukuwa baba yake sheby na ndio kizibiti cha kuachishwa kazi... "
"we mary hizi documents vipi zinaenda wapi"
Rose aliziona zile documents zilizoletwa kutoka Bank za kwenda kuchukua pesa zao za kusafirisha bidhaa za serikali,...
"zinakwenda kwa sheby"
"sasa mbona husemi we mary"
"lakini si umekuja sasa hivi tu"
"ok sawa... Ngoja nizipeleke"
Sasa rose ile anatoka tu mary kamuangalia kwa nyuma, rose alikuwa anatetemesha makalio mana hakuwa na chupi...
"we rose we"
"abeee"
"afu leo hujavaa chupi wewe"
Mary alikuwa akiongea tu lakini roho ilikuwa ikimuuma mno....
"amna nimevaa sema haijanibana tu"
Yaani angalijua kuwa hio chupi anayo mary wala asingeendelea kumdanganya...
"haya nenda"
Rose aliondoka lakini mary aliendelea kulia kisiri siri yaani mtu ampendae leo kasex na rafiki yake..
"rose rose rafiki yangu.. Nakutuma uniseidie kumbe nawe unampenda why lakini"
Mary aliongea mwenyewe baada ya rose kuondoka
Rose alipofika ofisini alikimbilia kwa sheby,...
"boss, huezi amini chupi sijaiona.. Na mbaya zaidi mary kanambia eti baba yako alikuja huku"
"Whatt??"
"ndio"
"lakini saa ile mimi nilikwambia, ofisini kuna mtu lakini wewe ukazidi kubisha tu, sasa ona sasa chupi haipo"
"lakini mi siamini kama baba yako ndio kaichukuwa kwa ajili ya kidhibiti cha kuniachisha kazi"
"ata sijui"
Ghafla rose kapiga magoti chini na kumuomba sheby msamaha, mana sheby nae alikuwa hana hata raha, baada ya kusikia baba yake alikuja hapa ofisini kwake...
"boss, Nisamee kwa hilo... Naomba niendelee na kazi"
"kwani nimekufukuza?"
"baba yako hatoniacha kwakweli"
"aahhhh mi sijui... We utakaa tu nyumbani, umefanya ujinga sana, umekuja ya nini lakini"
"nisamehe boss wangu... Ni hamu tu"
"toka bwana... Ushaniletea balaa hapa"
Sheby aliamka na kwenda ofisini kwa baba yake na kumwacha rose akilia pale chini... Sheby alipofika ofisini hapo hakumkuta baba yake,... Sheby alianza kupekuwa kwenye makabati huko kila mahari, fungua droo zote changua kila kona lakini hakuiona,.. Lakini sasa katika kupekuwa pekuwa vizuri alifanikiwa kuona picha moja ambayo baba yake sheby na baba yake mwanaheri wakiwa wamesimama pamoja,... Lakini baba yake sheby alionekana kutokuwa na chochote, yaani alikuwa na hali mbaya ya kimaisha... Ila baba yake mwai alionekana kuwa na hali nzuri ya kimaisha, yaani alikuwa kama boss boss hivi... Ila baba yake sheby alikuwa choka mbaya, tena hata viatu vyake vilikuwa vimeisha upande mmoja... Sheby alishangaa sana kuona kuwa kumbe baba yake mwai na baba yake walikuwa marafiki sana miaka ya huko nyuma... Lakini mbona ni choka mbaya hivi... Sheby alijikuta anapata Stress zingine tofauti na stress iliomleta.. Sheby aliichukuwa ile picha na kuingia nayo kule ofisini kwake... Alimkuta rose bado analia lia pale ndani...
"we bado hujatoka tu"
"yaani sijui nifanye nini mimi"
"nenda ofisini kwako.. Afu huu ujinga siutaki tena, yaani kaa mbali na mimi"
"boss Usiseme hivyo, kama ni mapenzi ndani ya ofisini kweli staki tena, ila kukuacha siwezi sheby Please"
"ondoka bwana aaah"
"ok... But documents hizo hapo ni za kufatilia benki"
Rose alikabidhi documents kisha akaondoka

BAADA YA MASAA KADHAA KUPITA

Na sasa ni mida ya jioni muda wa kutoka kwenda majumbani mwao,..
"mary jamami nitakwenda vipi nyumbani"
"sa unaniuliza mimi"
"lakini mbona una chuki juu yangu mary"
"ivi nikuulize Kitu"
"nini sasa"
"ivi sheby nampenda mimi au wewe"
"lakini mary"
"hakuna cha lakini... We ni mtu wa aina gani, tumefanya mangapi mimi na wewe, leo nakuomba uniseidie kuwa na sheby kumbe nawe unampenda, kwanza we mkubwa wala hulingani nae unamuonea tafuta wakubwa wenzio"
Mary alikuwa akiongea huku akitaka hata kulia...
"nilikuamini kama dada yangu, kuwa kama mshenga mi nampenda sheby na sio kumtamani kama ulivyotamani wawe,.. Bila mimi kujitoa siku ile tusingepata kazi,.. Au mbona wewe uliachia msala wote.. Lakini kwakuwa mtoto wa watu hana tabia mbaya aliniacha na kujikuta anachukuwa jukumu la kutufundisha kazi... Leo nimempenda mimi afu unaenda kulala nae wewe... Mungu anakuona kwa hilo rose"
"mary... Kwani mi nimelala na sheby"
"fara wewe, usilete usenge wako apa... Na nitahama hata kama chumba unalipia wewe nina uwezo wa kulipia chumba hata mimi... Nitalala hata kwenye godoro lakini siwezi tena kuishi na mtu kama wewe"
Mary alikasirika sana mpaka kufikia hatua ya kutengana na rafiki yake... Lakini wakiwa wanaendelea kutupiana maneno ghafla maadam alikuja, mana kwenye hio kampuni kuna mama mtu mzima ambae anawaweka wafanyakazi wa kike sawa kwa ajili ya wageni, hivyo wanamwita maadam,...
"nyie tatizo ni nini.... "
Waliulizwa lakini hakuna aliokuwa akijibu zaidi ya wote kusema hakuna kitu
"hakuna kitu maadam"
"ok kuna tatizo limetokea kwenye kampuni hiii... Tunaomba mtoke nje"
"tatizo gani tena maadam"
"utalijua nje.. Nyie tokeni pale mkakagulowe... Kuna wizi umetokea humu ndani"
"sawa maadam, ngoja tuchukuwe mabegi yetu"
Maadam alipita kwenda kwenye ofisi zingine ili kuwapa taarifa juu ya wizi uliotokea hivi punde.... Sasa akina rose na mary kufika nje walikuta watu wanasachiwa kila kona,.. Yaani hakukuwa na mtu aliotoka bila kusachiwa...
"kabla hujafika sehemu husika ya kukaguliwa, kwanza unaweka mkoba wako hapa vitu vyako vyote vitolewe hadharani ili kuukagua mkoba"
Aliongea baba yake sheby, huku wafanyakazi wakianza kuweka mkoba pale mmoja baada ya mwingine... Sasa mary presha juu mana kwenye mkoba wake kuna chupi ya rose, afu sasa rose nae presha juu kwasababu endapo atagundulika hana chupi ni kosa kubwa sana katika kampuni hio mana ni kampuni yenye maadili hivyo hutakiw kuja kihuni... Na kama ni mwanamke anasachiwa na mwanamke mwenzie, na kama ni dume basi anasachiwa na dume mwenzie, na mtu wa kusachi hatakiwi kuficha kitu pale palipo na tatizo... Hofu ya wawilo hawa ni kuhusu hio nguo ya ndani, mana wataulizwa ofisini walikuwa wanafanya nini... Mbona mmoja hana chupi na mmoja chupi ipo kwenye mkoba, kwahio kuna kitu walikuwa wakikifanya... Sasa ni zamu ya mary mkoba wake kusachi.. Mama aliushika ule mkoba wa mary na kumwaga vitu vyote pale chini....
"haaaaaaaaaaaaaaa"
Kila mtu alishangaa na kushika mdomo, hata boss haamini kwa kile walichokiona... Lakini sasa mbaya zaidi ni kwamba hata mary mwenye mkoba wake nae kashangaa, kana kwamba kitu kilichoonekana hata yeye hakijui,... Ilionekana ni tofauti na kile alichokidhania yeye....
 
MKE JEURI

(The Wife's Tyrant)

Sehemu Ya 34

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487 WhatsApp


Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←

Sasa akina rose na mary kufika nje walikuta watu wanasachiwa kila kona,.. Yaani hakukuwa na mtu aliotoka bila kusachiwa...
"kabla hujafika sehemu husika ya kukaguliwa, kwanza unaweka mkoba wako hapa vitu vyako vyote vitolewe hadharani ili kuukagua mkoba"
Aliongea baba yake sheby, huku wafanyakazi wakianza kuweka mkoba pale mmoja baada ya mwingine... Sasa mary presha juu mana kwenye mkoba wake kuna chupi ya rose, afu sasa rose nae presha juu kwasababu endapo atagundulika hana chupi ni kosa kubwa sana katika kampuni hio mana ni kampuni yenye maadili hivyo hutakiw kuja kihuni... Na kama ni mwanamke anasachiwa na mwanamke mwenzie, na kama ni dume basi anasachiwa na dume mwenzie, na mtu wa kusachi hatakiwi kuficha kitu pale palipo na tatizo... Hofu ya wawilo hawa ni kuhusu hio nguo ya ndani, mana wataulizwa ofisini walikuwa wanafanya nini... Mbona mmoja hana chupi na mmoja chupi ipo kwenye mkoba, kwahio kuna kitu walikuwa wakikifanya... Sasa ni zamu ya mary mkoba wake kusachi.. Mama aliushika ule mkoba wa mary na kumwaga vitu vyote pale chini....
"haaaaaaaaaaaaaaa"
Kila mtu alishangaa na kushika mdomo, hata boss haamini kwa kile walichokiona... Lakini sasa mbaya zaidi ni kwamba hata mary mwenye mkoba wake nae kashangaa, kana kwamba kitu kilichoonekana hata yeye hakijui,... Ilionekana ni tofauti na kile alichokidhania yeye....

ENDELEA..........

Sasa kabla hatujaendelea na hapo ilipoishia, tuanzie pale walipokuwa wakigombana baina ya rose na mary ndipo wakakatishwa ugomvi wao na maadam...

"nyie tatizo ni nini.... "
Waliulizwa lakini hakuna aliokuwa akijibu zaidi ya wote kusema hakuna kitu
"hakuna kitu maadam"
"ok kuna tatizo limetokea kwenye kampuni hiii... Tunaomba mtoke nje"
"tatizo gani tena maadam"
"utalijua nje.. Nyie tokeni pale mkakaguliwe... Kuna wizi umetokea humu ndani"
"sawa maadam, ngoja tuchukuwe mabegi yetu"
Aliongea rose huku akilifuata begi lake la kwapani,.. Lakini mary akiwa bado ana hasira na rose alikuwa mahari fulani kajiinamia kwenye meza... Sasa huyu rose wazo moja la kijinga lilimjia,...
"kwenye huu ukaguzi najua tutasachiwa na maadam suzy, sasa najua lazima anikute sina chupi, nalo ni kosa... Sasa bora wote tukitwe na makosa kuliko nikutwe mwenyewe"
Aliongea rose kimoyomoyo kisha akachukuwa kitu fulani kutoka kwenye begi lake na kukiweka kwenye begi la mary, ili tu wakutwe wote wana makosa, ila kitu alichoweka hakikujulikana ni kitu gani mana kilienea katika kiganja cha mkono wake... Wakati bado wanajishika shika pale mara maadam alirudi tena na kuwakuta bado wanazubaa zubaa tu,
"nyie bado hamjatoka tu"
"tunakuja maada, sema kuda documents nilikuwa nazisevu hapa kwenye kompyuta"
"hebu changamkeni nataka kuondoka.. Kule sasa wanasachiwa wanaume sasa inafuata zamu yenu wanawake"
"maadam tunakuja usijali"
Mwanamke wa watu aliondoka zake kuelekea nje... Lakini sasa mary aliona kuliko rafiki yake akajulikane hana chupi, ni bora ampe mana nia yake alikuwa asimpe ili aumie kwa mawazo kiwa huenda nguo yake imechukuliwa na baba yake sheby,..
"shika takataka yako.. Mschiuuuu... Haya kataa tena hujafanya nae"
Rose hana la kusema zaidi ya kuchukuwa chupi yake na kuivaa...
"lakini kwanini ukae na chupi yangu muda wote huo"
Kabla mary hajajibu maadam kaita tena, hivyo wakatoka mbio mbio, lakini huku nyuma rose alitamani atoe kile kitu kwenye mkoba wa mary ikashindika... Rose anataka kumuita mary lakini maadam alikuwa anaona hivyo ikabidi aache tu,... Mpaka walipofikia eneo la kusachiwa mabegi yao, linaanza begi kisha unafata wewe mwenye begi unasachiwa kila kona ya mwili wako, japo hakijulikani kitu kilichoibiwa humo ndani.... Kwenye hii kampuni ni kampuni yenye heshima kubwa sana, hivyo mfanyakazi wa kike haruhusiwi kuja na nguo za mitego, mfano ukutwe huna chupi, utaeleza kwanini hujavaa hio nguo, na ndio maana kukawekwa maadam mtu mzima ili kuwaweka sawa wafanyakazi wa kike, na wafanyakazi wa kiume haruhusiwi kuja ukiwa umepiga kata K... Haruhusiwi kuvaa kihuni...
Sasa baada ya wafanyakazi wa kiume kuisha walifuata wafanyakazi wa kike, rose alikiwa na wasiwasi mkubwa mana anakijua kitu alichokifanya kwa rafiki yake,... Ila mary yeye hana wasiwasi wowote kwasababu anajua chupi keshampa mwenyewe... Maskini ya mungu zamu ya mary ilifiki likachukuliwa begi lake na kumwagwa vitu chini ilivyofanyika kwa wengine....
"haaaaaaaaaaaaaaa"
Kila mtu alishangaa na kushika mdomo, hata boss haamini kwa kile walichokiona... Lakini sasa mbaya zaidi ni kwamba hata mary mwenye mkoba wake nae kashangaa, kana kwamba kitu kilichoonekana hata yeye hakijui,... Sheby alikuwa akiongea na simu lakini aliposikia zile sauti za haaaaaaaa ikabidi ageuke na kuangalia... Nae aliona kila kitu, maskini ya mungu mary alikuwa akimwangalia sheby huku akitikisa kichwa... Lakini ghafla boss mkubwa alipiga makofi, sekunde hio hio wafanyakazi nao wakapokea kupiga makofi kama boss wao alivyofanya...
"kiukweli sio tabia nzuri kwa kampuni yetu, lakini ameonyesha ni jinsi gani anajilinda na afya yake... Ni vizuri sana kwa kitembea na kinga... Hongera sana mwanangu"
Lakini mbali na kupewa sifa na baba yake sheby, bado sheby akiwa yupo pembeni katulia tu,... Rose anajikuta anampa sifa kubwa mary, lakini mary alijua kajenga sehemu fulani, ila kabomoa sehemu kubwa ya moyo wa mtu, kitendo cha sheby kuona pakiti ya kondom iliotoka kwenye kibegi cha mary ni dhahiri kuwa upendo kuupata pale ni ngumu, mana mtoto wa kike kukutwa na kondom ni jambo baya sana japp unajilinda lakini inaleta sifa ya umalaya, kana kwamba popote utakapokutana na mwanaume papo hapo unafanya yako, yaani inaashiria umalaya wa hali ya juu sana, ila ni umalaya wa kujilinda.....
"boss, tumesachi kila mmoja lakini hakuna aliokutwa na chochote cha ofisini"
Aliongea maadam ambae ndio msemaji mkuu wa wanawake katika kampuni hio
"sasa nani kaingia ofisini kwangu na kuchangua changua"
Sasa sheby kusikia kuwa nani kaingia ofisini kwa mzee, ndio akakumbuka kuwa mbona yeye ndio alioingia na kwenda kuvuruga kule ndani pale alipokuwa akitafuta chupi kama baba yake aliichukuwa, ndipo sheby akakuta picha ya baba yake mwai na baba yake wakiwa wamepiga pamoja, ila ni picha ya zamani sana...
"sasa mzew wangu, unahangaisha watu bure, kwanini usingesema nani kaingia ofisini kwako"
Aliongea sheby huku akimsogelea baba yake,
"kwani nilikwambia ni wewe"
"ndio ni mimi ndio nimeingia ofisini kwako, kuna documents ya zamani sana nilikuwa naitafuta... Sasa nilipoipata nikawahi kwenda kuisevu kwenye kompyuta yangu, na hapo ndipo nilipo sahau kuja kurudishia vizuri mafaili yako.. Ila mimi ndio nilioingia ofisini kwako"
"sasa kwanini usingelisema mpaka tunasumbua watu.. Toto jinga sana wewe..... Mama naomba ukanipangie yale mafaili kule ofisini kwangu"
Aliteuliwa mary aende kupanga yale mafaili ambayo sheby kayavuruga kwa kutafuta documents,...
"jamani naomba mnisamehe kwa usumbufu uliojitokeza"
Mzee Rashidy aliomba msamaha kwa wafanyakazi wake, kisha staff bus likawachukua wale wasio na usafiri na kuwapeleka majumbani mwao, mana kuna wale wenye usafiri na wale wasio na usafiri,... Kila mmoja aliondoka zake, hata rose alimsubiri mary mpaka kachoka ikabidi aondoke zake, wakati huo sheby nae kuna kazi alikuwa akimalizia ofisini kwake,.. Hivyo walibakia wawili tu kampuni nzima.. Nje ni mlinzi tu ndio kabakia... Sheby alimaliza kazi aliokuwa anaimalizia kisha kazima kompyuta yake kisha akafunga mlango wa ofisi yake,.. Sheby alishasahau kuwa ndani kuna mtu anaendelea kupanga mafaili,.. Saa ngapi hajafunga mlango na kwenda kwenye gari yake,.. Sasa mary yeye kashtuliwa na start ya gari iliokuwa ikiondoka....
Alipochungulia dirishani aligundua sheby ndio anaondoka hivyo... Ikabidi ampigie simu mana akiita sauti haitofika kutokana na vioo vya kuzuia sauti kuwekwa, mana ni jengo la vioo tupu, hivyo hata upige kelele vipi husikiki... Wakati huo yapata mida ya saa moja hivi jioni kagiza ndio hako kameanza... Mary kupiga simu ya sheby haipatikani,... Na sheby wakati huo ndio kwanza haelewi hili wala lile, anashika simu yake na kuiwasha, wakati alishapigiwa kama mara mbili hivi hakupatikana,.. Mary akawa anamtafuta mtu mwingine, akampigia maadam,.. Simu ya maadam iliita kisha ikapokelewa
"haloo madame suzy"
"ee habari yakl mary"
"salama... Sasa naomba uje na ufunguo madame.. Sheby kanifungia huku ndani"
"whatt... Kakufungia kwa lipi... Umemfanya nini mpaka akufungie"
"no, hajui kama mi nipo ndani"
"sasa si umpigie"
"nimepiga hapatikani"
"mungu wangu... Kuna namba yake ya siri sana hataki ujulikane, sasa sjui itakuwaje, na hio ndil anapatikana muda wote"
"please madame nisaidie, mana ndio anatoka getini sasa hivi"
"ngoja nimpigie basi"
"sawa"
Madame aliitafuta hio namba ambayo ndio namba anayopatika kila siku mana hio ya kwaida imezidi usumbufu hivyo akiizima anabakiza ile ya kifamilia tu..
"haloo boss"
"yes madame"
"mbona umemsahau mary kule ndani"
"Aaaaiiiiiiiiiiiiiiii shit.. Nilikuwa Nimesahau kabisaaaa.. Ok wacha nimrudie"
Sheby alikuwa keshaingia kwenye highway Road hivyo itabidi azunguke kwanza ndio arudi kule, mana hawezi kugeuza papo kwa papo, kutokana na wingi wa magari yaliopo nyuma yake, kitendo cha kwenda kugeuzia huko muda ulizidi kwenda mpaka ikafika saa moja na nusu usiku...
"piii piiii"
Ni sauti ya honi iliokuwa ikipiga ili mlinzi afungue geti... Haraka haraka geti likafunguliwa na sheby kaingia ndani... Haraka haraka kachukuwa funguo na kwenda kufungua mlango wa ofisi.... Aliwasha taa zote mana kulikuwa kiza sana...
"mary.... Mary"
"abeee boss"
Aliitikia mary lakini ni kwa sauti ya chini sana
"upo wapi"
"nipo huku boss"
Sheby aliingia mpaka ofisini kwa baba yake ndipo alipomkuta mary kajikunyata kwa baridi, mana jumba zima limezungukwa na Air Condition (AC) zinazofanya kazi muda wote....
"amka twende sasa"
Mary alikuwa kamaliza kupanga vitu alivyoagizwa sema kachelewa kutoka kwasababu alifungiwa,.. Sheby alimnyanyua mary, lakini mary nae alikuwa na mitego yake, kachoka kutuma mtu afu ageukwe, nae akaanza kuringa ringa kama mtoto, na ule uzuri wa sura yake, umbo lake jinsi alivyo laini,.. Mary aligoma kwenda na kujifanya anaskia baridi sanaaa,..
"nini sasa mary"
"nashindwa kitembea... Haya ma AC yenu yana baridi sana"
Sheby aliona mary anamchelewesha tu, alimkusanya na kumbeba... Sasa mary ndio kajifanya na usingizi kabisaa.. Kufika nje sheby kafungua mlango wa gari na kumweka kwenye siti za nyuma,... Kisha akatoka kwenda kufunga milango ya ofisini.. Alipomaliza alikuja na kuingia kwenye gari, uzuri ni kwamba wanapoishi anapajua hivyo hapo ni kumpeleka tu... Sasa sheby ikabidi apige jicho vizuri kwa nyuma ili akiendesha gari asije kudondoka mana hapo alipo kajikunja sana kwa baridi... Lakini sasa ile sheby kupiga jicho nyuma, kakutana na paja lilionona haswa, akapanda na paja hilo hilo mpaka alipokutana na chupi ya pinki... Balaa la Sheby ni kuona hio nguo, yaani hio ndio shida yake kuu... Sheby akatikisa kichwa ili kujitoa ufahamu, akamfunika vizuri lakini bado akili inawaza tu kumfinya... Alipiga moyo konde, aliwasha gari kisha huyooo.. Mpaka kwao rose katoka nje baada ya kusikia muungurumo wa gari,...
"ebu mchukiwe rafiki yako"
Rose alitoka na kumshika mkono, kiukweli mary alikuwa wabaridi sana kutoka AC ya kule ndani
"mbona ana baridi hivi"
"nilisahau nikajikuta nimemfungia kule ndani"
"mungu wangu sasa si ataugua huyu"
Rose alimkokota rafiki yake mpaka ndani kisha akarudi kwa sheby...
"boy nina maongezi na wewe"
Aliongea rose huku akimsogele kijana huyo.......... Dakika chache mbele sheby alitoa gari na kurudi nyumbani kwake, hata mke wake sikuhizi hakasiriki hovyo wala hamkasirikii mumewe, anampokea kwa shangwe sana... Lakini leo alishangaa mkewe kawa kimya afu mbaya zaidi alikuwa akimwangalia,..
"haya niambie.. Naona makiss ya mdomoni na mashavuni hayajakutosha,.. Ila ukaona uje unidhibitishie kwa kupigwa mabusu mpaka kwenye mashati"
Sasa sheby kuangalia kwenye kifua chake katika shati, laaaaa haulaaaaa shati limejaa rangi ya mdomo, (lipstick)
 
MKE JEURI

(The Wife's Tyrant)

Sehemu Ya 35

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487 WhatsApp

Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←

Sasa sheby ikabidi apige jicho vizuri kwa nyuma ili akiendesha gari asije kudondoka mana hapo alipo kajikunja sana kwa baridi... Lakini sasa ile sheby kupiga jicho nyuma, kakutana na paja lilionona haswa, akapanda na paja hilo hilo mpaka alipokutana na chupi ya pinki... Balaa la Sheby ni kuona hio nguo, yaani hio ndio shida yake kuu... Sheby akatikisa kichwa ili kujitoa ufahamu, akamfunika vizuri lakini bado akili inawaza tu kumfinya... Alipiga moyo konde, aliwasha gari kisha huyooo.. Mpaka kwao rose katoka nje baada ya kusikia muungurumo wa gari,...
"ebu mchukiwe rafiki yako"
Rose alitoka na kumshika mkono, kiukweli mary alikuwa wabaridi sana kutoka AC ya kule ndani
"mbona ana baridi hivi"
"nilisahau nikajikuta nimemfungia kule ndani"
"mungu wangu sasa si ataugua huyu"
Rose alimkokota rafiki yake mpaka ndani kisha akarudi kwa sheby...
"boy nina maongezi na wewe"
Aliongea rose huku akimsogele kijana huyo.......... Dakika chache mbele sheby alitoa gari na kurudi nyumbani kwake, hata mke wake sikuhizi hakasiriki hovyo wala hamkasirikii mumewe, anampokea kwa shangwe sana... Lakini leo alishangaa mkewe kawa kimya afu mbaya zaidi alikuwa akimwangalia,..
"haya niambie.. Naona makiss ya mdomoni na mashavuni hayajakutosha,.. Ila ukaona uje unidhibitishie kwa kupigwa mabusu mpaka kwenye mashati"
Sasa sheby kuangalia kwenye kifua chake katika shati, laaaaa haulaaaaa shati limejaa rangi ya mdomo, (lipstick)

ENDELEA........

Sasa kabla hatujaanzia hapo naomba tuanze nyuma kidogo wakati amemmbeba mary,... Mary akiwa kule ndani alijipara mdomo yaani alijipaka rqngi za mdomoni huku akisema
"kama nitashindwa kukuambia basi we gundua upendo wangu kwa rangi"
Aliongea hivyo mary kisha akajifanya kulegea lege lege... Sheby alipokuja aligundua mary aliathiliwa na air condition za humo ndani hivyo kakosa nguvu ya kutembea,.. Na hapo ndipo sheby alipochukuwa jukumu la kumbeba mpaka kwenye gari, sasa hicho kitendo cha kubebwa hapo ndipo alipompaka sheby rangi ya mdomo katika kifua chake, tena vile sheby akitembea huku mary alikuwa akimkiss kijana huyo katika kifua chake, bila kujua hio ni hatari sana katika ndoa yake... Kijana yalimpakia mary vizuri kisha akaondoka zake, alipofika nyumbani kwao rose alitoka na kuja kumpokea rafiki yake, japo wana kabifu ka kimapenzi wenyewe ni siri yao... Rose alimpeleka mary ndani kumlaza lakini ukumbuke kuwa mary hakuchoka kivile bali aliweza kuongea na kutembea pia, lakini kulegea kule alifanya makusudi kwa yule ampendae... Lakini kabla sheby hajaondoka rose alimwita sheby
"Boy, nina maongezi na wewe"
Aliongea rose baada ya kumpeleka mary ndani, lakini mary yeye hakulala aliamka na kuchungulia dirishani, kana kwamba wivu ulikuwa ukimsumbua mtoto wa kike... Sasa ukumbuke sehemu iliopita hatukujua walichoongea hawa watu wawili, na dhumuni la kuianzia stori huku nyuma kabisa, ni ili tuyajue yale maongezi baina ya rose na sheby..
"unajua nachelewa"
Aliongea kijana huyo huku akiangalia saa yake ya mkononi,
"i Know, but nipe dakika tano tu"
Rose alisogea karibu na sheby, lakini sasa rose kuangalia vizuri kifuani kwa sheby aligundua shati lake lilichafuliwa na makiss ya mary,.. Rose akajua basi mary keshamaliza kila kitu, kama mpaka mabusu wamepigana basi keshamaliza kazi yake... Lakini rose alipoangalia vizuri, makiss yenyewe yalionekana kama kuiba iba hivi ndipo alipogundua kuwa bado hajafanya lolote lile...
"boss.... Kwanza kabisa naomba unisamehe mimi, sisi ni wafanyakazi wako, lakini kibaya zaidi ni kwamba wote tumejikuta tukikupenda weww peke yako... Mpaka sasa hivi hapo ndani hapatokalika tena, mary anataka kuhama kwa kile nilichomfanyia"
Aliongea rose huku akiwa anafikicha vidole vyake kana kwamba anaanza kumseidia mary
"sasa kwanini umfanyie mwenzio kitu ambacho hapendi"
"kitu ambacho hapendi, ni kufanya mapenzi na wewe"
"Ati nini"
Wakati huo mary anasikiliza kupitia dirishani,
"kiukweli Mary alikuwa akinituma mimi kama dada yake kwako kukudhihirishia kuwa anakupenda, lakini badala yake nikawa naitumia nafasi hio kujielezea badala yake... Nakumbuka hata siku ile mary alilazimika kwenda bafuni kuoga ili kunipa nafasi ya mimi na wewe nikuelezee ni jinsi gani anakupenda... Lakini nikawa najitengenezea mimi kwa tamaa zangu za mwili"
"kwaio point ni ipi"
Aliongea kijana huyo huku akitaka kuondoka mana hakuna kilichokuwa kikimuingia akilini,
"najua nimeshaharibu sana, na mpaka sasa hatuna raha tena baada kugundua tumefanya mapenzi mimi na wewe... Na hata ile chupi yangu yeye ndio alichukuwa"
"kwasababu gani afanye hivyo"
"aliniambia kuwa alileta documents fulani, ndipo akakuta nguo yangu juu ya meza, anavyosema yeye aliondoka lakini kufika mbele akakutana na baba yako anakuja ofisini kwako,.. Ikabidi arudi mbio na kuichukuwa ile nguo ili baba yako asije kuiona... Hivyo ndivyo ilivyokuwa na kwa kitendo hicho tu nimegundua mary ananipenda sana na hakutaka nifukuzwe kazi japo niliekuwa nafanya nae mapenzi ni mtu anaempenda kwa dhati.... Boss, ndio maana nikatanguliza Samahani, kwasababu tumejikuta tunakupenda tu, ila najijua mimi ni tamaa zangu tu, lakini mary, anakupenda kutoka moyoni... Mfikirie tu, kama ni mimi niache mana ilikuwa ni nafasi yake"
Rose alimaliza kuongea kihivyo huku akitaka kuondoka
"mshanifanya mi malaya eee?.. Yeye leo si kafanya na mtu ofisini"
Rose kashangaa kuskia mary alikuwa na mtu kazini,.. Hata mary nae akawa makini kuskia hapo
"alikuwa na mpenzi ndani"
Aliuliza rose huku akiwa katoa macho
"ina maana we hujaona kondom zile"
Rose kuskia hivyo akapumua kwa nguvu, mana alikuwa anamjengea rafiki yake japo keshaharibu lakini ivo ivo tu
"afu boss Samahani, sijakuelezea kuhusu zile kondom... Zile mimi ndio niliziweka tukiwa ndani ili tukutwe na hatia wote, kwasababu muda nilioweka zile kondom kwenye begi lake, alikuwa bado hajanipa chupi, hivyo nikajua nikikutwa sina chupi nitafukuzwa kazi, sasa nikaona tuingie wote nitoke peke yangu haiwezekani ndipo nikamuekea kondom kwenye begi lake... Lakini Nilitamani kuzitoa baada ya kunipa nguo yangu ila nilikosa nafasi hiyo, nikaacha tu ndio akakutwa nazo"
Sheby aliona ni kama anaimba tu, aliingia kwenye gari yake kisha huyoo kaondoka zake, rose kaingia ndani na kumpa taarifa mary
"haya sasa kazi yako nimeshamaliza"
Aliongea rose huku akikaa kitandani
"sina shida"
Mary alijibu kwa nyodo kali, na anajua kweli kamwambia, lakini haiseidii kitu mana hata akimkubali, atakuwa keshatembea na shemeji yake,...
"sasa mbona unakusanya nguo jamani"
"niache niondoke zangu... Kisa unalipa chumba wewe ndio uninyanya kwenye mapenzi"
"mary jamani, nimeshasema yote"
"sina shida na ukuadi wako.. Naondoka"
"mary please kumbuka tumetoka mbali eti"
"staki kujua"
Mary kweli alikuwa akikusanya mabegi yake tayari kwa kuondoka,.. Rose alichukuwa simu na kumpigia rafiki yao mkubwa ambae ni mwai
"halooo shost mwai"
"vp saa hizi"
"mary anataka kuondoka jamani eti kisa nimeshindwa kumtongozea boss wetu"
"ivi nyie mna akili nyie... Ebu mpe simu niongee nae"
Mary alipewa simu na rose, hakusita kuichukuwa mana mwai ndio rafiki aliewapokea hapa mjini
"we mary, unakwenda wapi usiku huu.. Utakuja ubakwe bure na kibikra chako kiozee mbele, tuliza miguu hapo"
"siwezi kuishi na hasidi mimi"
"ebu ngoja kwanza, naomba kesho Jumapili mje nyumbani kwangu tulizungumze vizuri"
"sawa lakini staki kukaa kwake tena"
"mary nisikilize mimi kama dada yako.. Usinidharau.. Kama ni huyo mwanaume hata mimi naweza kukuseidia"
"ok sawa... Lakini naomba mwisho wa kuishi na huyu mtu iwe leo, kesho natafuta chumba changu"
"sawa hakuna shida"

Wakati mwai anaongea na simu ghafla honi ya gari inapigwa hapo getini, kana kwamba sheby ndio alikuwa anaingia kwa wakati huo,
"sawa basi kesho muje wote"
Mwai alikata simu kisha kasimama mlangoni ili kumpokea mume wake, siku hizi habebi bebi vipocho pocho vingi mana si anapika, mwanzo alikuwa akibeba kwasababu kulikuwa hakupikwi,... Sasa mwai kabaki mdomo wazi baada ya kuona shati la mume wake limejaa rangi ya mdomo
"haya niambie.. Naona makiss ya mdomoni na mashavuni hayajakutosha,.. Ila ukaona uje unidhibitishie kwa kupigwa mabusu mpaka kwenye mashati"
Sheby kucheki Ayaaaaaa... Kweli imekaa mabusu sio mabusu.. Lakini sasa huyu ni mtoto wa kiume na anajua kuikwepa mitego kama hio
"ayaaaaaaa ina maana yule bibi kizee anapakaga huu ujinga"
Aliongea hivyo huku mwai akiuliza kuwa
"ina maana siku hizi unatembea na watu wazima"
Sasa sheby kuskia hivyo nae Kukasirika na kusema
"kwani ata wewe ni lika langu, si mtu mzima kabisa wewe, muone vile"
Mwai roho ilimuuma mana kwa sasa ana vichembe chembe vya upendo kwa mumewe...
Sheby alimsukuma na kuingia zake ndani,
"lakini bado nina haki ya kujua huu upumbavu wa kwenye shati umeutoa wapi, laa sivyo hapalaliki hapa"
Mwai kaamua sasa mana kupenda penda kijinga imekuwa kero..
"kuna bibi aligongwa na gari ndio nikamseidia, ndio maana mwanzo nikasema ina maana mpaka bibi kizee anapa huo ujinga.. Umeridhika"
"basi nenda zako kalale uko"
Sheby aliingia chumbani kwake na kulala bila hata ya kuvua viatu kwa kuchoka...

Kesho yake ikiwa ni siku ya Jumapili sheby akiwa katika gari kuelekea kwa akina zai,... Leo kwa mara ya kwanza toka waachane na zai ndio anakanyaga kwao,... Lakini sasa ile anakata tu kona ya kuingilia kwenye boma ya akina zai, aliona gari ya saidi kwa mbali, sheby alitamani kukata na kurudi lakini hapakuwa na nafasi ya kugeuzia, ni mpaka ufike pale ndipo ugeuze,.. Saidi akiwa ndani na mke wake mtarajiwa alisikia sauti ya gari ya boss wake,...
"heeeeeeeee kwa mfano boss kapajuaje hapa"
Saidi aliongea kimoyomoyo huku akiwaza boss wake kapajuaje hapo, mana anakumbuka alimwomba gari tu sasa vipi leo kaja,.. Ukumbuke saifi hajui kama sheby na zaituni walikuwa ni wachumba waliokuwa wakisubiri ndoa...
"karibu baba"
Mama zai alimkaribisha, wakati huo ndani zaituni anaogopa kuwa saidi akijua kuwa mimi nilishawahi kuwa mpenzi wa boss wake, atamuacha na mwishowe atakuwa kakosa bara na pwani,...
"Ahsante mama shkamoo"
"Marahaba ujambo baba"
"sijambo mama angu"
Sheby kaingia mpaka ndani na kuwakuta zai na saidi wamekaa kochi moja ili kuonyesha upendo wa hali ya juu,...
"za saa izi jamani"
Sheby alitoa salamu kwa wawili hao,
"safi tu boss, vp umejuaje kuwa nipo huku"
"aaahhh nimekuja kumsalimia mama hapa"
"aaahhh kumbe unafahamiana na hii familia"
"ndio, tena kwa kiasi kikubwa sana"
"aaaaahh duuu nimeshangaa kuskia upo hapa na sijawahi kukuleta"
"ahahahaha mi mbona mwenyeji hapa"
Lakini sasa mama ni mtu mzima alishaanza kuona kitakachotokea mbele baada ya saidi kujua boss wake alishapita hapo... Mama alimwangalia sheby kisha akatikisa kichwa, kana kwamba kama sheby kuna kitu alitaka kufanya asifanye tena, mana ataharibu uchumba wa mtoto wake... Sasa kwakua sheby yeye hana nia ya kuharibu hivyo alimsikiliza mama kisha akajifanya kamfuata Zainabu mana kuna zainabu na zaituni...
"aaahhh zainabu yupo wapi"
Zaituni alishangaa kumsikia sheby anamuulizia ndugu yake, na sheby anajua fika kuwa zainabu ni malaya wa kutupwa
"yupo nje hapa baba"
Mama alitoka na sheby kisha akawa anamwangalia zainabu... Kwa bahati nzuri hakuwepo mana ilikuwa ni gia ya kutokea pale ndani.. Mama hakutaka kuuliza kilichotokea baina yao na zaituni, mana kitendo cha zaituni kuleta mwanaume mwingine ni dhahiri kuwa alishindwa kuvumilia hali ya kijana huyo... Sheby aliwasha gari yake bila hata ya kuaga kule ndani....

Ikiwa ni mida ya jioni huku nyumbani kwa kijana sheby kulikuwa na ugeni wa wasichana wawili... Mary na rose
"karibuni jamani mashost zangu"
Mwai aliwakaribisha wageni zake, kama unakumbuka aliwaalika waje wale chakula cha jioni,.. Wakati huo kijana sheby yupo njiani kuelekea nyumbani kwake, asijue hili wala lile huko nyumbani kwake
"jamani nimewamis nyie, toka siku ileee ya sherehe mpaka leo"
"mmmhh mbona sie tupo, sema bize"
"bize ya hao wachumba zenu mnaowagombea kila siku.. Oleweni mtulie kama mimi mwenzenu"
"enheee hapo mwai umeongea kitu, ebu mwambie mary, nimemuomba msamaha mimi lakini hataki kusikia sijui ana nini huyu"
"lakini nawe rose, kwanini utembee na mtu wa watu eee, Kama we umejua anampenda kwanini usimfanyie mpango yeye"
"lakini mwai si unajua shetani tu"
"kwahio huyo mtu mnafanya nae kazi ofisini kwenu"
"ndio tena ni boss wetu mdogo mdogo hivi"
Waliongea bila hata ya kumeza mate, kama unavyojua mashostito wanapokutana mahali, na wakati huo kijana sheby yupo mlangoni tayari kiganja chake kimetua kwenye honi
"piii, piiii"
Mlinzi kama kawaida yake kuchakalika kwa hapa na pale kutokana na kazi yake
"mmeo nini huyo"
Aliuliza rose huku kama wanaogopa ogopa hivi mana kwenda kubwata umbea kwenye nyumba za watu ni kitendo kibaya sana tena kwa sisi wanaume hua hatukipendi kabisa yani, mwanamke utoke kwako uje huku kuleta umbea tu, ndio uharibifu wa ndoa sema hawajui tu wenyewe.. Sasa kama kawaida ya mke wa sheby kukaa mlangoni ili tu ampokee na maneno,
"leo hujaleta hata chochote, yaani mwanaume wewe"
Mwanaheri aliongea hivyo huku sheby akishuka kwenye gari na msunyo mkubwaaa,...
"nipishe mimi"
"lakini si nimekuuliza tu"
"unaniuliza mie baba ako"
"Wwhaaaaaat"
Sasa mwai anasema What, sheby nae ndio anawaona akina mary...
"ooohhh leo kuna ugeni leo"
Sasa mary na rose ndio wanashangaa, ina maana kumbe rafiki yao ndio kaolewa na boss wao,. Sasa mwai nae anataka kutambulisha anakuta watu wanajuana siku nyingi tu,.. Mwai anashanga hawa wakina rose na mume wake wamejuana wapi...
"nyi... Nyie... Nyie mnajuana"
Mwai au mke wa sheby Aliuliza, na sheby pale pale akajibu kwa uchangamfu wa hali ya juu..
"ndio... Ni wafanyakazi wenzangu hawa.. Sasa kwanini umekuja usiku jamani"
Sasa sheby yeye anajua katembelewa yeye,...
"rose na mary, anachokisema mme wangu ni kweli mnafanya nae kazi"
"ndio.. Tena ni boss wetu huyu"
Sasa mwai kuskia hivyo akagundua jambo
"ina maana siku zoote hizo kumbe mnamgombania mume wangu rose??... Hapana kitaeleweka tu hapa"
Mwai alianza kufunga kanga kiunoni, wakati huo sheby nae anashangaa kumbe mkewe na akina rose wanajuana.....

Je? Nini kitaendelea hapo???... Watajitetea vipi?.....
 
Muziki: Ukishindwa Kuvumbua, Iga Uigwe!

Ni Furahiiiiiiday, hakuna asiyejua japokuwa nimeisema kwa sauti kubwa ili hata kama uko kwenye makelele ya bakulutu, unajamiiana (socialize) au vigodoro basi angalau ushituke na ujue nimekuja kwenye kipengele ninachokipenda zaidi, muziki. Na ujue ninakipenda kipengele hiki kwa sababu gani, mmmh, simple sana mbona, kwa sababu wewe uko hapa na zaidi unalifanya jukwaa hili kuwa 'live', sehemu nzuri ya kujifunza na kupata maarifa. Sababu yote hii ni kwa sababu upo hapa, asante sana.

Friday ndo mwanzo wa wikend, sikufundishi namna ya kuitumia wikend yako maana una maisha yako, nami ninayo yangu ila ukidedicate siku mbili hizi ukiwa na family yako, friends and those close to you itakuwa poa sana. Unaweza kuiga hili na sio jipya. Vingi sana vimevumbuliwa, tunachofanya ni kuiga tu na kuvipendezesha, waliovumbua vitu au alama wasingeigwa wasingeeleweka. Kuiga ni jambo zuri but it should not be slavish, you know, unaiga hadi nukta. Pendezesha unachoiga na ukiiga toa credit kwa mwenye wazo , inajenga heshima na kuaminika na zaidi ni uungwana. Iga mazuri zaidi ya mengine, sio kama anko wangu ambaye mimi humuiga akili zake sharp sio matendo maana matendo yake ya kimwili hayatulii kwa shangazi yangu tu. Iga uigwe.

Muziki sasa, nikushukuru sana shululu kwa magazeti, ujue mdau siwezi kuchoka kukushukuru kwa hili na wengine wote mnaolifanya jukwaa hili kuwa kama supu iliyotiwa ndimu ya pilipili. Asante anko Lyon Lee kwa UF, asante husna muba kwa hadithi, asante my BH BlessedHope kwa maneno ya kiimani, asante SHIMBA YA BUYENZE kwa nukuu za kuchangamsha. Asante Shunie , Tumosa , dingimtoto ,Nyagei , mtugani wa wapi huyo , Jagood , Sweetiepie , Mkushi wa kusi , mzeewakungoa , makaveli10 , Sakayo , Transcend , Gentries , moneytalk , Tetramelyz , Linamo , demi , ABJ , Clkey , Madame S , Bitoz , Jimena , Werrason , Mussolin5 , koncho77 na wewe Kapuku ambaye unalifanya Jukwaa hili kuwa mahali pazuri pa kuelimika, kuburudika, kufurahi na zaidi kuwa sisi


 

Similar Discussions

Back
Top Bottom