"Shebby mwanangu mimi Sijachanganyikiwaaaa wala huyooo unaetaaka kumuua hajaachanganyikiwaaaa... Nataka Ujue mimi ndie Zainab mke wa Hussein na wewe ndie mtoto wake aliyesingiziwaa kamuuaa na huyooo unayejuaa babaako ndie MR X.."
kauli hii ya mama Shebby aliyokuwa anaiongea kwa sauti ya uchungu sana na maumivu ndiyo iliyomfanya Shebby asiamame ghfra na kujikuta hadi ile bastora iliyokuwa mkononi mwake ikimdondoka chini kwa mshtuko mkubwa na kugeuka kumtazama mamaake aliekuwa anasota kumfata pale aliposimama mlango wa kuingilia jikoni.
"Mwananguuu Shebby, Hussein ndie babaako kweli kabisaaa. Ni kweli kabisaaa kweli sisi wanawakeee ni wauajiii aaaaaaaaaghhhh Nisamehe mwananguuuu"
aliongea huku akilia Zai akiwa amekamata miguu ya Shebby aliejikuta anashindwa kuongea lolote zaidi ya kuchezesha midomo tu kwa mtetemo ambao ulikuwa haukujulikana kama ni hasira au maumivu.
Maneno yale pia yalisikiwa vizuri sana na Cj4 na hata Hussein mwenyewe aliekuwa anahangaika na roho yake huku kila alivyojitahidi kuongea ndivyo damu zilipozidi kumvuja mdomoni na kubaki anaongea na Cj4 kwa kumtazama tu na alifanya hivyo hata pale Cj4 alipotaka kumlaza chini kwa kujiandaa kumuadhibu Shebby, Hussein bubu alimtazama kwa jicho lile la kumzuia asifanye hivyo.
"MAMAA !!! Ina maana...."
alitaka kusema kitu Shebby na kujikuta akishindwa ndipo alipokimbilia ndani mule jikoni kumuangalia Hussein bubu na kumkuta akiwa kashikiliwa na Cj4.
"Amini hivyo Shebby ukweli huyu ndie babaako."
alikazia Cj4 pindi Shebby alipoingia ghafra na hapo Hussein alijikuta kama anapata nguvu tena mara baada ya macho yake kukutana na uso wa Shebby na kumuashiria asogee pale na ainame.
Kwa mwendo wa 'sielewi' na taharuki nyingi alisogea Shebby na ajabu alipoinama tu Hussein aliweza kumuinamisha zaidi na kumuingiza mkono begani mwake kupitia ile kora ya shati ya Shebby na hapo mkono wa Hussein ulikutana na uhisio wa alama kama ile ya lengelenge mtu kaungua ama viuvimbe vyeusi vinavyowatoka watu (sunzua) kikiwa kwa urefu kuelekea maeneo ya begani.
Shebby alistuka na kutaka kuutoa mkono wa Hussein lakini Cj4 alimzuia aache na baada ya Hussein kuridhika aliutoa ule mkono huku akiwa katabasamu hali iliyowashangaza na hata mamaake Shebby nae aliingia kule jikoni kwa mtindo ule ule wa kusota mithili ya mlemavu huku akiwa bado analia huku akimsisitizia Shebby kuwa yule ndie babaake.
"ww-wa-ww-waa-aa-n-.."
alibabaika kusema Hussein na kujikaza kumwambia Shebby na Cj4 pale kwa mara nyengine na wote wakiwa wametaharuki Hussein bubu akarudia tena.
"uwwwan-aa-ang-uu Wa-na-wa-ke ni- Wa---u-aj-i."
na hiyo ndio ilikuwa kauli ya mwisho ya Hussein bubu na kuaga rasmi dunia akiwa mikononi mwa Cj4 huku pembeni yake alikaa mwanae ambae ni Shebby na kwa mbele mlangoni alionekana Zainab mamaake Shebby.
"BAABAAA"
Aliita kwa nguvu Shebby na kujipiga piga kichwa kwa majuto kwani alijua fika risasi zilizofatuliwa kwa mikono yake mwenyewe Shebby ndio zilizosababisha umauti wa mtu ambae alikuwa hajui kwanini moyo ulimsukuma mno kumsaidia na leo hii anajua akiwa amemuua kwa mkono wake akijua anamtetea mtusahihi kumbe sivyo.
Lakini toka hivyo Shebby alisimama na kutoamini kama yule ni babaake na yule ndie Mr X na wazo hili lilipomjia alikumbuka kauli ya yule marehemu Mnyungunyungu kuwa mr X ana alama usoni nahapo alijikuta anaingiwa roho mbaya nusu chizi Shebby alirudi pale ilipokuwa maiti ya mtu aliyeamini siku zote ni babaake na kuanza kumpekua usoni ambapo alikuwa na mdevu nyingi na katika hali ambayo hakuitaraji ni kweli aligundua alama ya X iliyokuwa usawa wa chini ya kidevu karibu na koromeo na hapo ndipo alipoanza kuamini sasa kuwa kweli yule mtu aliyedhani babaake alikuwa ndie mr X na jina X lilitokana na ile alama yake ambayo huwezi kuiona kwa kumtazama tu, lakini alijiuliza kwanini yamekuwa yote yale? ndipo hapo kwa uchungu mno Shebby alianza kulia huku akimuuliza swali mamaake kwanini imetokea yote hayo.
"Maaaaaa Why? kwanini mama yamekuwa yote hayaa? aaaaghh"
Maumivu aliyokuwa nayo Shebby hayapaswi hata kusimuliwa kwa jinsi alivyokuwa anaumia huku akifikiria kwanza kamuoa dadaake, pili kamuua babaake wa kweli, tatu ni kwanini mamaake aliishi na siri iliyokuwa inapoteza roho za watu kila siku???
"Mwanangu Shebby ni kweli sistahiri kabisa kuishiii aaaaah! leo nimejifunza wakati tayari ni too late, ila naamini mwanangu mimi ndio chanzo cha yote hayaa... Eee Mungu naomba unipe tu hukumu inayostahiki juu yangu ..... Shabaan mwanangu vyovyote utachoamua unisamehe ama usinisamehe lakini ukweli mimi ndie chanzoooo aaaaaaaah! Ama Kweli sisi Wanwake ni Wauaji."
*<>*<>*<>*<>*<>*
^^^^^^^
CHANZO
^^^^^^^
*<>*<>*<>*<>*<>*<>
( MIAKA 50 NYUMA )
.................................
...............
Ilionekana familia moja ya bwana na bibi Juma wakiwa katika kupanga panga vitu vyao husasi mabegi na kadhalika huku vijana wengine watatu walionekana kubeba viti, mbao za kitanda sambamba na magodoro wakipeleka nje na kupakia kwenye gari moja aina ya Canter iliyopaki karibu kabisa na ile nyumba ikionesha dhahiri bwana na bibi Juma walikuwa wanahama sehemu ile na kuhamia sehemu nyengine kwenye makazi mapya.
Wakati heka heka za kuhama zikiwa zinaendelea, upande wa pili kulipokuwa na nyumba inayotazamana na ile ambayo walikuwa wanaishi bwana na bibi Juma alionekana kijana mdogo wa kiume mwenye umri usiopungua miaka 12 akiwa amekaa mlangoni ameshika tama huku akiwa na huzuni kubwa wakati anaishuhudia familia ile ikihama pale mtaani kwao.
Moyo ulimuuma sana yule mtoto ambae alikuwa maarufu pale mtaani kwa watoto wenzie kwa jina la Zungu japo jina lake halisi halikuwa hilo.
Kilichokuwa kinamuumiza zaidi si kuhama kwa bwana na bibi Juma bali ni kuondoka pamoja na mtoto wao mdogo wa kike aliyekuwa na umri wa miaka 8 ambae alikuwa ni rafiki ake mkubwa sana shule na mtaani walicheza wote na mara nyingi walipenda kujiita baba na mama.
"Kinoge mbona humuagi rafiki ako Zungu si unamuona alivyopooza"
aliongea bwana Juma kumuambia mwanae yule wa kike ambae nae alionesha kutoipenda kabisa ile safari na alijisikia moyo kumuuma hata kumuaga kwa mdomo rafiki ake zaidi ya kumuangalia kwa jicho huruma na kumnyooshea mkono wa kwaheri pindi alipokuwa anapandishwa ndani ya gari ile mara baada ya kila kitu kumalizika kupakiwa.
("wewe ndie rafiki niliekuzoea, leo hii unaondoka na kuniacha mwenyewe. Najua huko utapata rafiki mwengine utayecheza nae kama mimi kibaba baba lakini jua kama nikimuona nitamuua kwa kua atakuwa tayari adui yangu.")
aliwaza maneno mazito sana yule mtoto Zungu pindi alipoishuhudia gari ile ikiondoka eneo lile la mtaani kwao na kumuachia msiba mzito wa upweke moyoni mwake....
"Hussein mwanangu, usiwe mnyonge hivyo. Ndugu yako nipo hapa si nishakwambia...? mimi ndio ndugu yako babaa"
ilikuwa ni sauti ya mwanaume mtu mzima iliyosikika nyuma ya mlango alipokaa mtoto Zungu ambae jina lake halisi alikuwa anaitwa Hussein.
Sauti ile ilimfanya Hussein ageuke huku machozi yaliyojazana machoni muda mrefu alipokuwa anawaangalia kina Kinoge wakihama bila kupepesa macho, yalianza sasa kutiririka mashavuni mwake na kumtazama kwa uchungu yule mtu aliyemsemesha.
"baba, babaa unajua inauma sana. sasa wewe umewezaje kukaa mwenyewe na kuvumilia bila kulia pindi mama alipoondoka?"
aliuliza mtoto Hussein na kumfanya yule mtu ambae alikuwa ni babaake mzazi amnyanyue pale na kumkumbatia kwa nguvu huku akimsihi atulize kwanza moyo kwa kumshikashika kichwa akizichezea nyele zake ndogo za kipilipili huku mkono mwengine akimpigapiga mgongoni.
"Mwanangu Hussein, mbona ni rahisi sana baba...! ni rahisi mwanangu twende ndani nikakuhadithie"
aliongea babaake Hussein na kumchukua mwanae mpaka chumbani kuwapisha wapangaji wengine waendelee na shughuli zao mida ile pale ukumbini waliposimama jilani na mlango wa kutokea.
"Mwanangu mamaako amekuacha ungali una miaka mitano lakini japo nilimkumbuka ila haikuwa sababu ya kunifanya niwe mnyonge na kukosa kabisa furaha. Unajua kwanini?"
alianzisha maongezi babaake Hussein pindi walipokua wamekaa kitandani pale chumbani kwao.
"hapana baba, sijui"
"Kwa sababu wewe ulikuwepo, unajua kwanini uwepo wako ulikuwa sababu ya mimi kukosa huzuni na kuwa na furaha mbali ya kuwa mamaako hakuwepo tena?"
"Hapana baba sijui."
"Kwa sababu wewe ndie ndugu yangu na yule alikuwa mke wangu na ndio maana ameolewa tena na mwanaume mwengine na hata huko anaweza kuondoka tena na kuolewa pengine."
"aaah, sasa baba na mimi mama sio ndugu yangu?"
"Hapana mwanangu, wewe ni zaidi ya ndugu yako kwa sababu wewe ni mwanae na yeye ni mamaako unapaswa kumuheshimu na kumtembelea mara kwa mara."
"sawa baba, kwa hiyo Kinoge sipaswi kumlilia kwa kua sio ndogo yangu na huko aendako anaweza kupata rafiki kama mimi na wakihama tena atamuacha na kwenda kupata rafiki mwengine ikawa hivyohivyo eeeh.."
"Ni kweli kabisa mwanangu, hutakiwi kumuweka sana moyoni mwanamke mwengine zaidi ya mamaako mzazi ambae hawezi kuondoka na kukuacha moja kwa moja hata uwe uweje, ila hawa wengine mwanangu usiwaamini kabisa na kuwaeka sana moyoni kwani wataweza kukusababishia maumivu na mateso makubwa pindi watapogeuka na kwenda kwengine."
"sawa baba"
"Ndio hivyo mwanangu hupaswi kuumia mimi nipo na hata kama nisipokuwepo amini wa kukusaidia kweli ni mwanaume mwenzako japo wanawake ndio wanaoonekana kuwa na mioyo mepesi ya kusaidia lakini bado msaada wa ukweli upo kwa mwanaume baba. haya nyamaza wewe ni mmwanaume shika hela hii kanunue chapati uje tunywe chai"
"Asante baba nimeelewa, nami nakuahidi sitoumia tena kwa sababu ya Kinoge"
aliongea Hussein na kufuta machozi baada ya kuchukua pesa kwenda kununua hivyo vitafunwa huku akimuacha na tabasamu zito babaake.
* * * * *
Safari yao iliwachukua masaa mengi garini siku hiyo tokea asubuhi ile walipoliacha jiji la Dar na kuingia jijini Arusha majira ya saa moja usiku ambapo safari bado iliendelea mpaka kwenye vijiji vya mbali na Arusha mjini na huko ndiko kulikokuwa na makazi mapya ambayo walihamia familia ya bwana na bibi Juma pamoja na mtoto wao kipenzi aliyeitwa Kinoge.
"haaa! mamaa ndio tumefika hapaa!!?"
aliuliza kwa mshtuko Kinoge pindi alipoyaangalia mazingira waliyofikia kwa nje ambapo muda huo wale vijana waliopakia vitu kule jijini walikuwa wanavishusha wakipewa maelekezo pa kuviingiza na bibi mmoja ambae ndie alikuwa mwenyeji wao aliyewapokea.
"Kinoge kwani wee unapaonaje si pazuri tuu.. tena huku kuna maembe na machungwa kibaoo unayopenda furaaaahi basii."
mama alijaribu kumliwaza mwanae ambae sasa alikuwa tayari kakunja uso kutokana na kuchukizwa na mazingira yale ya kijijini.
Aliangalia kwanza hakukuwa na umeme, hakukuwa na barabara nzuri, nyumba zilikuwa zipo mbalimbali hali iliyomuumiza Kinoge na kuona ni afadhali wangemuacha jijini Dar na rafiki ake Zungu asingekuwa mpweke kuliko kuletwa pale ambapo aliamini hata marafiki wa kucheza nao kama Zungu hawakuwepo.
"iiihhhhhhyyaaaaaaaaaa.. sipaaatakiii mimiiii... Nirudiisheeeni kwa Zunguuuuu"
alianza kulia kwa sauti Kinoge na mamaake kujitahidi kumnyamazisha wakati huo babaake alikuwa anasombelea vitu na kuvipanga kwenye ile nyumba pamoja na wale vijana.
Baada ya shuguli zote za uhamiaji kukamilika na ile gari waliyokuja nayo kuanza safari kuelekea mjini na hatimae sasa Kinoge aliamini kuwa kweli wamefika na hasa pale alipokuja babaake na kumwambia.
"Mwanangu Kinoge, maisha ni mlima leo unapanda kesho unashuka harafu maisha ni popote usiangalie mazingira kwanza ukayakimbia unafikiri hata kule mjini kulikuwa vile? kule napo kulikuwa kama huku.. Watu wakahamia na kupasafisha wakaishi na kupatengeneza hadi leo umepaona vile. Basi hata huku napo kutakuwa kama vile endapo tutakaa na kupatengeneza. Haya twende ndani ukasalimiane na bibi eeeh"
Maneno ya babaake ndio yaliyompa nguvu Kinoge na kupiga moyo konde kuwa tayari kuanza maisha mapya.
Bwana Juma ambae ni baba mzazi wa Kinoge yeye alikuwa ni mwalimu wa shule ya msingi na wakati huo alikuwa amepata uhamisho wa huko Arusha ambapo aliuomba yeye mwenyewe ili apate nafasi ya kurudi nyumbani kwa mamaake ambae alikuwa mzee na alihitaji uangalizi wake na kwa kuwa miaka mingi aliipoteza Dar mpaka anazaliwa Kinoge na kufikia umri ule alikuwa hajawahi kufika pale kijijini lakini sasa hawakuwa na budi wote kwa pamoja walihamishia makazi kijijini kabisa.
Na huo ndio ukawa mwanzo wa Kinoge kupotezana na Zungu.