Makapuku Forum

Makapuku Forum

Arsenal 4 leicester 3

Clkey
Brother shululu
mukuye tugonge glass

Kwa hisan ya kolasinic a.k.a braza mbavu a.k.a bodybuilder.

sent using my nokia ya tochi
Mkulu kumbe na wewe ni mr uvumilivu....njia pekee ya Arsenal kuwa salama Msimu huu basi ni kuomba Mustaph na Koscielny warudi haraka katika safu ya ulinzi..... Kwa kuendelea kuwasimamisha Nacho, Holding na Kolasinac kama mhimili wa eneo la ulinzi kwenye michezo ya ligi kuu ni kuendelea kujicementing katika nafasi ya sita.

Ebwanaaadaaaaaaaah ....Alexander Lacazete shikamoo mzee, kile kichwa ni record nyingine kabla ya lile goli..... Umetuletea Zawadi katika EPL Msimu huu. Unaweza kucheza nje ya box, unamudu vyema ndani ya box.... Kizungu wanasema "what a player"

Craig Shakespeare ...alikuwa ana mjaribu mzee Wenger kama akili inafanya kazi. Kuna wakati uwanja uliinamia golini kwa arsenal, hapo kila mtu aliwahurumia na kuwa cheka Arsenal ila kuna wakati wa uwanja uliinamia golini kwa Leicester city na mbaya zaidi walishindwa kujua chakufanya katika mipira iliyokuwa inakwenda katika box la Leicester city.
...anyway mr wenger ndo kawaida yake kuongoza kabla ya ligi na pindi ligi inapoonza mengine ya baadae ni majaliwa ...

Mm droo inanitosha
 
Nani huyo kapiga simu?"
aliuliza kwa sauti nCj4 wakati huo Shebby aligeuza gari kwa fujo na kugonga mti upande wa nyuma kabla hajatia gea ya mbele na kukanyaga mafuta kwa fujo bila kujali kishindo cha nyuma alipogonga kumetokea madhala kiasi gani.
"Nani kakupigia Shebby?"
aliuliza tena Cj4 huku akibamiza dashboard kwa kofi kali baada ya kuona Shebby yupo kimya huku akili yake ikiwa mbali sana.
"Ni mfanya kazi... Ni dada wa kazi kiongozi... aaagh! anaongea huku analia na nilisikia sauti za vitu vikiongwa gongwa..."
aliongea kwa pupa Shebby wakati huo barabara waliyokuwa wanapita mbele yake kulikuwa na kijiforeni kilichomfanya ahamie bara bara ya pili huku akivipana vile vizuizi vidogo vya barabara na kusababisha gari iruke ruke na kutaka kudondoka pasi nae kujali kuwa anaingia upande usiomruhusu ambao haukuwa na magari mengi na wala hakupunguza mwendo Shebby aliendelea kukanyaga mafuta huku akizikwepa kwepa gari zilizokuwa zinakuja mbele yake.

Kelele za honi zilisikika kwa fujo kama zile kelele za mavuvuzela katiaka kombe la dunia kule south pindi Shebby alipokuwa anakosana kosana kugongana na gari nyengine zilizokuwa zinakuja mbele yake na hiyo yote ilikuwa kutaka kuwahi nyumbani kuzuia matatizo yaliyokuwa yanatokea muda ule akihofia mr X asiwadhuru watu wote wa familia yake hususani baba na mamaake pamoja na mkwewe ambae ni Hussein bubu.
"Cj4 ushauri wako safari hii umeniponza. Aaaagh! umeona kumuacha Hussein bubu nyumbani matatizo yanatokea na kuwaumiza watu wasiohusika kabisaaaaa aaah! ona tunawaponza watu wengi zaidi? Ni bora tungemueka sehemu ya kumlinda wakati tukimsaka Mr X."
alilalama Kamishna Shebby huku machozi yakimtoka wakati kichwa chake kilipotengeneza mazingira ya nyumbani na kuona jinsi wazazi wake wanavyoumizwa na watu wa Mr X.
Wakati Kamishna Shebby akilalama Cj4 yeye alikaa kimya na kuvuta picha na kuona lazima Hussein ndie aliyeanzisha kasheshe huko baada ya kugundua kitu kuhusu Mr X, na si wala kwamba kuna mtu zaidi kavamia ile nyumba na kusababisha mauaji.

Gari iliiingia mkuku na kugonga geti hadi walinzi walistuka mno na hapo Kamishna Shebby alipiga teke mlango mdogo wa geti baada ya kushuka kwenye gari huku akiwa ameikamatia bastora ndogo mkononi na kustaajabu kukuta walinzi wakiwa wamejificha kwaajili ya kupambana na uvamizi waliotaraji kutokea na wao kushangaa kuona ni Kamishna Shebby.
Tofauti ya Shebby kwa upande wa Cj4 yeye hakuingilia pale getini zaidi alizunguka eneo la nyuma ya ukuta na kurudi nyuma kutafuta speed ya kukimbia kidogo kabla hajaruka beki kavu tatu zilizompeleka moja kwa moja hadi ndani ya fance sehemu kulipokuwa na bustani ya kupumzika na bwawa kubwa la kuogolea na ajabu zaidi Cj4 alijipanga kwa vita akiwa mikono mitupu.

* * * *

"Zaaainaab.. Zaiiiiinaaaab.. Zainaaaaaabuuuu leo na wewe lazima ulipe damu ya mwanangu."
aliongea Hussein bubu huku akipiga hatua kumsogelea mama Shebby kwa hasira pale chini alipokuwa anasote huku akilia kwa uchungu.
"Hapaanaaaa, hapaaanaa .. aaah! Haaapaana Mume wanguu."
alijitahidi kutoa sauti mama Shebby japo hakufanikiwa kuitoa kwa nguvu kama vile alivyoilazimisha ila ilitosha kusikiwa na Hussein.
"Mume wako? Mume wakoo!! hahahaha Mume wako unaemlilia huyu Shetani mtoa roho za watu? hahahaa nakusafirisha sasa hivi umfate huko aliko ila kwanza nataka unijibu swali moja Zai... KWANINI ULINIGEUKA NA KUSABABISHA KIFO CHA MWANANGU NA KUNIHARIBIA MAISHA YANGU YOTE???"
Aliuliza Hussein kwa hasira iliyokuwa inamfanya hadi atetemeke mwili mzima pindi alipokuwa amemfikia mama Shebby ambae ni kweli kabisa ndie Zai wake yule yule.
"Hapana Hussein, hapana sikujua kabisa kama yangekuja kutokea mazito kiasi hiki wala sikuweza kuyafanya yasiendelee kutokea aaahggggg nimejiponzajeeee mieeeee."
aliongea kwa uchungu Zai na kuendelea wakati huo Hussein alikuwa anazidi kutetema kwa hasira akingojea jibu la Zai kabla hajaanza na yeye kumponda ponda kichwa chake kwa kile chuma kilichotapakaa damu.
"Hussein, unastahiri kabisaaaaa kufanya haya Mume wanguuu......."
"STOOOOOP. Nihadithie kwanini na wala usinite Mume wangu. Utafanya nikuue kabla hata sijasikiliza jibu lako."
alimkatisha kwa hasira na kumpelekea Kofi moja kali lililomfanya Zai kupasuka lipsi ya mdomo baada ya kujing'ata kwa kupigiza kichwa pale kwenye ngazi.
"sawaaaa... sawaaa .. sawa..aaaghhhhh, wala sikumwambia Mr X akuue, wala sikupanga mwanangu azushiwe kuuliwa nawe pamoja na mimi mwenyewe, wala sikuyajua hayo yoteee Hussein. Naomba uniaminiiiii... Ila tatizo wewe hukuwa Mume wangu wa Kwanza kunioa na kunilipia mahali japo ulikuwa mwanaume wa kwanza kuniingiza katika ulimwengu wa mapenzi.
Sikuona jinsi gani ya kukwambia ukweli hadi unielewe na kuniruhusu nikaishi kwa mume wangu. Hussein najua leoo upo sahihi na mimi ndie niliekuwa nastahiki kulipa nafsi za hao wote.. Lakini unadhani ningefanyajeee? huyo Mr X ndie mume wangu kabisa wa kwanza aliyejulikana hadi na wazazi wangu..... wewe umemjua bibi tu Hussein lakini mimi nilikujua muda mrefu kabla hatujahamia Arusha.
Na ahadi yako ya utotoni hasa vile ulivyonambia kama utani naona leo inakuwa kweli aaaaaaaah!! Nataka ujue kabla hujaniua kuwa mimi ni KINOGE rafiki ako wa utotoni ZUNGU."
aliongea kwa uchungu zaidi Zai na kumshangaza tena Hussein baada ya kutajiwa kwa mara ya pili jina la Zungu na kukumbuka siku aliyokubaliwa kuwa na mahusiano na Zai alimwita jina hilo lakini alijikuta anachoka zaidi na kushangaa baada ya kujua kitu ambacho hakuwahi kukijua kumbe Zai ni Kinoge msichana waliyependana mno toka watoto na mara ya mwisho walipoteana wakiwa darasa la tatu.
"Haaa, KINOGE??!!"
Alitahayuri akiwa bado na hasira Hussein na ndipo kichwani mwake ilipokuja taswira na picha ile ya Kinoge pindi walipokuwa watoto.
....

ZUNGU => Kinoge Ona huyu ndio mtoto wetu, huyu ndio mimi hapo na huyu wewe harafu huyu aliyelala hapa adui nimekufuma nae anataka kuninyang'anya nimempiga nimemuua sasa nakupiga na wewe hapo hahaha nakuacha unalia harafu nam beba mwanangu tunaondoka hukoooo.
KINOGE => hahaha Zungu bwana, sasa kama wewe baba na mimi mama unafikiri adui atatoka wapi? tutakuwa tunapendana kama baba angu na mama angu si eti eeh?
ZUNGU => haya ila mi nitampenda sana mwanangu kama baba alivyokuwa ananambia kuwa mimi ndie ndugu yake na sio mamaangu kwani ana ndugu zake. Na wewe utakuwa na ndugu zako na mimi ndugu yangu mwananguuu.
KINOGE => Jamani Zungu, utakuwa unanipiga?
ZUNGU => Akuuu, ila nikikukuta na adui nitampiga hadi afe na wewe nitakupiga kibao kimoja tu..
^^^^^^
(<<<>>>) ^^^^ (<<<>>>)
.....................

Yalikuwa ni mawazo ya Hussein bubu pindi alipokumbuka mara ya mwisho kuongea na Kinoge siku hiyo majira ya jioni walipokuwa wanacheza mchezo wa kibaba baba huku akiwa ametengeneza watu wa kufinyanga kwa udongo na Kinoge alikuwa anapikapika kwenye vifuu.
Maneno ambayo aliwahi kuyaongea kitoto toto katika michezo ya watoto leo hii yamekuwa na ushabihiano mkubwa sana na kilichokuwa kinatokea japo hakuwahi kuwaza, kuhisi wala kujua kama Zai ndie rafiki ake wa utotoni yule aliyekuwa akimwita mchumbaake kabla ya wazazi wake kuhama na hakujua walihamia wapi na hata alipokua mkubwa ilifika wakati Hussein alisahau kabisa habari za Kinoge.

Lakini mbali na hayo yote bado msimamo wa Hussein ulibaki palepale, alishadhamiria kumuua na Zai na alikuwa anasubiri jibu moja tu lenye sababu za msingi kwani yote yale aliyokuwa anazungumza Zai ilikuwa kama anazunguka tu.
"Uwee Kinogeee uwe Zaaiii nataka kujua kwanini ulifanya yote yale na kuwa tayari kuimwaga damu ya mwanangu kinyama namna ile hata kichwa chake nisikionee?? Wee ni mwanamke wa aina gani!!??? Lazima leo Ufe na hii si kwa niaba yangu tuu, bali ni kwa niaba na damu ya mwanangu mliyeniekea viganja vyake mfukoni ili mkanifunge vizuri Wanyama Mbwa wakubwa nyiee... Hii ni kwaajili ya damu ya mwangu Mwin she heeeeeee...."
aliongea kwa uchungu Hussein na kukikamatia vizuri kile chuma huku akiwa kanyoosha mikono yake juu kwa niaba ya kuanza kumshushia kisago mama Shebby au Zainabu au kwa jina la utoto Kinoge.
Lakini akiwa kakamata kile chuma akinyanyua mikono kabla hajakishusha kichwani mwa Zai, ndipo alipopiga ukelele wa kukanusha kile alichokisema na kukiamini Hussein.
"HAPANAAAA, SIJAWAHI KUUA DAMU YANGU."
Kauli hii ilimfanya kwanza Hussein asite na kumuuliza Zai.
"Unamaana Gani? Nini kilitokea juu ya Mwanangu?!!"
"Hakuna kibaya chochote kilichompata mwanetu Mwinshehe... Mwanao mzimaaaa na ni rafiki ako mkubwa tuuu..."
"NINI? Unamaanisha nani? Kamishna??"
"hiiiiihiiii Nisameeeeheeee .. Ni kweliiiii Kamishna Shebby ndie mtoto wetu yuleyule Mwinshehe hiiiiigggr ... Eeee Munguuuu wanguuuuuuu"
Aliongea mama Shebby na kumzidisha machungu na taharuki Hussein aliebaki katumbua macho huku akiwa haamini kile anachokisikia masikioni mwake.
"NINI???!"
"Ndio hivyoooo aaah!! kweli mimi ni mkosaaaaji lakini Shaaban ndie mwnetu yule yule Mwinshehe na hata ile alama bado anayo pale nyuma ya shingo karibu na bega japooo aaaagh haaataa Mwin-chaaande umemuuua bila kutambuaa ukweli huuuuuuu"
kilio cha mama Shebby sambamba na maneno yake kilizidi kumkasilisha Hussein bubu ambae alizidi kutetemeka kwa hasira kuhu machozi yakimtoka na kuchirizika mashavuni huku yakisukuma damu iliyomgandia Hussein ambayo ilimrukia pindi alipokuwa anamuua mzee Mwinchande Mr. X.
"Ina maaaaanaaa Zaii.. aaah UmeniekaaUchiiii umenitukanisha vya Kutoshaaaa!!!!! HaaH! siamini mimiii Zainab?? Kinoge?? Mwanamke wa ndoto zangu leo acha maneno yangu yatimieeee"
aliongea kwa uchungu sana Hussein huku akizidi kunyanyua juu kile chuma na kukaza mikono.
"Wanawake ni Wauaji... Aaaagh! Wanawake ni Wauaji nyinyiii... Ona kwa sababu yako watu wangapi wamekufa Zai..Ona ulivyonitukanishaaa... Onaa sasaa wanangu mwenyewe nimewaoza mwenyeweeeeee!!! haaaaaaaa...
siwezi kumlaumu Asha wala Shebby iiiiiihhh Umenitukanajeeee!!? Kinogeee Hustahiri kabisa kubaki hai.. Hustahiri kabisa kuishi Zaiiii hata ninavyokuua leo sipaswi kuhukumiwa kwa hilo kwani hukumu yangu ya kukuua ilishapitishwa na kuitumikia miaka mingi sanaaaaaaa Zai kuishi sasa HUSTAHIRIIII"
Aliongea kwa hasira sana Hussein na sasa alikuwa anataka kushusha kile chuma kichwani mwa Zai ambae alijua sasa mwisho wake umewadia na hakuwa na ujanja wa kumkimbia Hussein bubu pale zaidi ya kufumba macho kusubiri kusikia chuma kikitua kichwani mwake na kusambaratisha fahamu zake zote kabla ya kuiacha dunia na kwenda kwenye makazi ambayo hajui yakoje.
Lakini kabla Hussein bubu hajashusha kile chuma kichwani kwa aliekuwa mkewe miaka hiyo bi Zainab ndpo ghafraaaaaaaaaaa mvunjiko wa kioo cha dirisha ulisikika sambamba na mtu aliyevaa mavazi ya polisi magereza mwenye cheo kikubwa alieonekana akiingia kwa mtindo wa kuruka huku mikononi akiwa kakamata mguu wa kuku (bastora ndogo) kishupavu kabisa na pindi alipoangukia tu mule ndani sekunde ileile kwa mbali alipomuona Hussein bubu akiwa anataka kumuua mamaake mzazi huku kushoto kwake akiuona mwili wa babaake mzazi ukiwa umepasuliwa vibaya sehemu za kichwa, nae palepale akiwa kakunja goti mguu mmoja alipiga kelele za uchungu huku akimfatulia risasi yule mtu aliemsimamia mamaake akitaka kumshushia vyuma vya kichwa na alimtambua kabisa kuwa yule ni nani ila aliamini kuwa amechanganyikiwa.
"HUSSEEEEENIIII BUUBUUUUU"
Alipiga ukelele Kamishna Shebby huku akiachia risasi mfurulizo kumuelekezea Hussein lakini sekunde ile ile kwa style ya ajabu kabisa alistukia kiatu kikubwa aina ya buti kikitua mikononi mwake Kamishna Shebby na kumshuhudia mwanaume wa shoka Cj4 akitokea upande ule wa juu kwenye ngazi na si kwa kushuka ngazi bali ni kwa kuruka nje ya ngazi na kutua pale alipokuwa anadondoka Hussein bubu na kumdaka kimaajabu na kubimbilika nae hadi maeneo ya mlango wa jikoni ambapo Cj4 aliingia na Hussein bubu na kujibanza nae nyuma ya Friza la kuekea nyama jikoni.
"aaaaaghrrr Na-kuuu-ku-mbuu-uu-k-kk-kaa raf--f-fiki--ang-gu"
aliongea kwa shida Hussein bubu mara macho yake yalipokutana na macho ya Cj4 aliekuwa kampakata nyuma ya lile friza lililokuwa karibu na mlango wa kuingilia jikoni.
"Polee rafiki angu mimi nipo hapa. Utapona tu"
"We-ni-As--ss-sskari?"
"Kweli rafiki angu mimi naitwa Cj4 ni askali niliyetumwa na serikali kwaajili ya kujua ukweli wako uliomfanya Shebby ashambuliwe kule Mkuyuni ila sasa kila kitu kipo sawa rafikiangu jikazee"
aliongea harakaharaka Cj4 huku akimuangalia kwa huruma Hussein bubu ambae damu zilianza kumvuja mdomoni na hata nyengine kuchuruzika kwenye mikono ya Cj4 na kugundua kuwa kuna risasi zilimpata Hussein mgongoni na kujilaumu Cj4 moyoni kuwa alichelewa kumuokoa Hussein.

"Cj4 kama umeungana na huyo Muuaji wa familia yangu tambua na wewe ni adui yangu sasaaaaa.. Aaaaaaggggggghh"
aliongea kwa hasira Shebby pindi alipoinuka na kuiokota bastora yake pale ilipodondokea na kuanza kuelekea kule jikoni alibimbilikia Cj4 na Hussein bubu.
"Mwananguuuuuu Shebbyyyyy usimuuue Husseeeeein ni babaaakoooo"
alipiga ukelele Zai ambae ni mamaake Kamishna Shebby ili kumzuia mwanae kutoendelea kufanya kile alichokifanya muda mfupi uliopita baada ya kufatua risasi mfurulizo zilizomfanya abaki kainama huku akiziba masikio na macho kwa uoga.
"Shebiii mwananguuuuu nisikilizeeeee"
alizidi kupiga kelele Zai lakini Shebby hakujali wala kusikia maneno ya mamaake kwa hasira alizokuwa nazo kwa kuhisi pia huenda na mamaake alikuwa kachanganyikiwa kwani anawezaje kumtetea mtu aliyekuwa anataka kumuua muda si mrefu? na tayari kamuua hadi mumewe? aliona wazi mamaake kachanganyikiwa na alikuwa tayari kupambana na Cj4 ambae alionekana kumtetea Hussein bubu.
("Huyu sasa anazidi upuuzi, acha kwanza nimfunze kuwa wanaume wanapokuwa kazini hutanguliza umakini mbele na si upendo.")
ilikuwa ni sauti ndani ya moyo wa Cj4 huku akimtoa mapajani mwake Hussein bubu pindi aliposikia vishindo vya hatua za minyato vya Shebby vikiwa vimekaribia pale mlango wa jikoni....
 
"Shebby mwanangu mimi Sijachanganyikiwaaaa wala huyooo unaetaaka kumuua hajaachanganyikiwaaaa... Nataka Ujue mimi ndie Zainab mke wa Hussein na wewe ndie mtoto wake aliyesingiziwaa kamuuaa na huyooo unayejuaa babaako ndie MR X.."
kauli hii ya mama Shebby aliyokuwa anaiongea kwa sauti ya uchungu sana na maumivu ndiyo iliyomfanya Shebby asiamame ghfra na kujikuta hadi ile bastora iliyokuwa mkononi mwake ikimdondoka chini kwa mshtuko mkubwa na kugeuka kumtazama mamaake aliekuwa anasota kumfata pale aliposimama mlango wa kuingilia jikoni.
"Mwananguuu Shebby, Hussein ndie babaako kweli kabisaaa. Ni kweli kabisaaa kweli sisi wanawakeee ni wauajiii aaaaaaaaaghhhh Nisamehe mwananguuuu"
aliongea huku akilia Zai akiwa amekamata miguu ya Shebby aliejikuta anashindwa kuongea lolote zaidi ya kuchezesha midomo tu kwa mtetemo ambao ulikuwa haukujulikana kama ni hasira au maumivu.

Maneno yale pia yalisikiwa vizuri sana na Cj4 na hata Hussein mwenyewe aliekuwa anahangaika na roho yake huku kila alivyojitahidi kuongea ndivyo damu zilipozidi kumvuja mdomoni na kubaki anaongea na Cj4 kwa kumtazama tu na alifanya hivyo hata pale Cj4 alipotaka kumlaza chini kwa kujiandaa kumuadhibu Shebby, Hussein bubu alimtazama kwa jicho lile la kumzuia asifanye hivyo.
"MAMAA !!! Ina maana...."
alitaka kusema kitu Shebby na kujikuta akishindwa ndipo alipokimbilia ndani mule jikoni kumuangalia Hussein bubu na kumkuta akiwa kashikiliwa na Cj4.
"Amini hivyo Shebby ukweli huyu ndie babaako."
alikazia Cj4 pindi Shebby alipoingia ghafra na hapo Hussein alijikuta kama anapata nguvu tena mara baada ya macho yake kukutana na uso wa Shebby na kumuashiria asogee pale na ainame.
Kwa mwendo wa 'sielewi' na taharuki nyingi alisogea Shebby na ajabu alipoinama tu Hussein aliweza kumuinamisha zaidi na kumuingiza mkono begani mwake kupitia ile kora ya shati ya Shebby na hapo mkono wa Hussein ulikutana na uhisio wa alama kama ile ya lengelenge mtu kaungua ama viuvimbe vyeusi vinavyowatoka watu (sunzua) kikiwa kwa urefu kuelekea maeneo ya begani.
Shebby alistuka na kutaka kuutoa mkono wa Hussein lakini Cj4 alimzuia aache na baada ya Hussein kuridhika aliutoa ule mkono huku akiwa katabasamu hali iliyowashangaza na hata mamaake Shebby nae aliingia kule jikoni kwa mtindo ule ule wa kusota mithili ya mlemavu huku akiwa bado analia huku akimsisitizia Shebby kuwa yule ndie babaake.
"ww-wa-ww-waa-aa-n-.."
alibabaika kusema Hussein na kujikaza kumwambia Shebby na Cj4 pale kwa mara nyengine na wote wakiwa wametaharuki Hussein bubu akarudia tena.
"uwwwan-aa-ang-uu Wa-na-wa-ke ni- Wa---u-aj-i."
na hiyo ndio ilikuwa kauli ya mwisho ya Hussein bubu na kuaga rasmi dunia akiwa mikononi mwa Cj4 huku pembeni yake alikaa mwanae ambae ni Shebby na kwa mbele mlangoni alionekana Zainab mamaake Shebby.
"BAABAAA"
Aliita kwa nguvu Shebby na kujipiga piga kichwa kwa majuto kwani alijua fika risasi zilizofatuliwa kwa mikono yake mwenyewe Shebby ndio zilizosababisha umauti wa mtu ambae alikuwa hajui kwanini moyo ulimsukuma mno kumsaidia na leo hii anajua akiwa amemuua kwa mkono wake akijua anamtetea mtusahihi kumbe sivyo.
Lakini toka hivyo Shebby alisimama na kutoamini kama yule ni babaake na yule ndie Mr X na wazo hili lilipomjia alikumbuka kauli ya yule marehemu Mnyungunyungu kuwa mr X ana alama usoni nahapo alijikuta anaingiwa roho mbaya nusu chizi Shebby alirudi pale ilipokuwa maiti ya mtu aliyeamini siku zote ni babaake na kuanza kumpekua usoni ambapo alikuwa na mdevu nyingi na katika hali ambayo hakuitaraji ni kweli aligundua alama ya X iliyokuwa usawa wa chini ya kidevu karibu na koromeo na hapo ndipo alipoanza kuamini sasa kuwa kweli yule mtu aliyedhani babaake alikuwa ndie mr X na jina X lilitokana na ile alama yake ambayo huwezi kuiona kwa kumtazama tu, lakini alijiuliza kwanini yamekuwa yote yale? ndipo hapo kwa uchungu mno Shebby alianza kulia huku akimuuliza swali mamaake kwanini imetokea yote hayo.
"Maaaaaa Why? kwanini mama yamekuwa yote hayaa? aaaaghh"
Maumivu aliyokuwa nayo Shebby hayapaswi hata kusimuliwa kwa jinsi alivyokuwa anaumia huku akifikiria kwanza kamuoa dadaake, pili kamuua babaake wa kweli, tatu ni kwanini mamaake aliishi na siri iliyokuwa inapoteza roho za watu kila siku???
"Mwanangu Shebby ni kweli sistahiri kabisa kuishiii aaaaah! leo nimejifunza wakati tayari ni too late, ila naamini mwanangu mimi ndio chanzo cha yote hayaa... Eee Mungu naomba unipe tu hukumu inayostahiki juu yangu ..... Shabaan mwanangu vyovyote utachoamua unisamehe ama usinisamehe lakini ukweli mimi ndie chanzoooo aaaaaaaah! Ama Kweli sisi Wanwake ni Wauaji."

*<>*<>*<>*<>*<>*
^^^^^^^
CHANZO
^^^^^^^
*<>*<>*<>*<>*<>*<>
( MIAKA 50 NYUMA )
.................................
...............

Ilionekana familia moja ya bwana na bibi Juma wakiwa katika kupanga panga vitu vyao husasi mabegi na kadhalika huku vijana wengine watatu walionekana kubeba viti, mbao za kitanda sambamba na magodoro wakipeleka nje na kupakia kwenye gari moja aina ya Canter iliyopaki karibu kabisa na ile nyumba ikionesha dhahiri bwana na bibi Juma walikuwa wanahama sehemu ile na kuhamia sehemu nyengine kwenye makazi mapya.

Wakati heka heka za kuhama zikiwa zinaendelea, upande wa pili kulipokuwa na nyumba inayotazamana na ile ambayo walikuwa wanaishi bwana na bibi Juma alionekana kijana mdogo wa kiume mwenye umri usiopungua miaka 12 akiwa amekaa mlangoni ameshika tama huku akiwa na huzuni kubwa wakati anaishuhudia familia ile ikihama pale mtaani kwao.
Moyo ulimuuma sana yule mtoto ambae alikuwa maarufu pale mtaani kwa watoto wenzie kwa jina la Zungu japo jina lake halisi halikuwa hilo.
Kilichokuwa kinamuumiza zaidi si kuhama kwa bwana na bibi Juma bali ni kuondoka pamoja na mtoto wao mdogo wa kike aliyekuwa na umri wa miaka 8 ambae alikuwa ni rafiki ake mkubwa sana shule na mtaani walicheza wote na mara nyingi walipenda kujiita baba na mama.
"Kinoge mbona humuagi rafiki ako Zungu si unamuona alivyopooza"
aliongea bwana Juma kumuambia mwanae yule wa kike ambae nae alionesha kutoipenda kabisa ile safari na alijisikia moyo kumuuma hata kumuaga kwa mdomo rafiki ake zaidi ya kumuangalia kwa jicho huruma na kumnyooshea mkono wa kwaheri pindi alipokuwa anapandishwa ndani ya gari ile mara baada ya kila kitu kumalizika kupakiwa.
("wewe ndie rafiki niliekuzoea, leo hii unaondoka na kuniacha mwenyewe. Najua huko utapata rafiki mwengine utayecheza nae kama mimi kibaba baba lakini jua kama nikimuona nitamuua kwa kua atakuwa tayari adui yangu.")
aliwaza maneno mazito sana yule mtoto Zungu pindi alipoishuhudia gari ile ikiondoka eneo lile la mtaani kwao na kumuachia msiba mzito wa upweke moyoni mwake....

"Hussein mwanangu, usiwe mnyonge hivyo. Ndugu yako nipo hapa si nishakwambia...? mimi ndio ndugu yako babaa"
ilikuwa ni sauti ya mwanaume mtu mzima iliyosikika nyuma ya mlango alipokaa mtoto Zungu ambae jina lake halisi alikuwa anaitwa Hussein.
Sauti ile ilimfanya Hussein ageuke huku machozi yaliyojazana machoni muda mrefu alipokuwa anawaangalia kina Kinoge wakihama bila kupepesa macho, yalianza sasa kutiririka mashavuni mwake na kumtazama kwa uchungu yule mtu aliyemsemesha.
"baba, babaa unajua inauma sana. sasa wewe umewezaje kukaa mwenyewe na kuvumilia bila kulia pindi mama alipoondoka?"
aliuliza mtoto Hussein na kumfanya yule mtu ambae alikuwa ni babaake mzazi amnyanyue pale na kumkumbatia kwa nguvu huku akimsihi atulize kwanza moyo kwa kumshikashika kichwa akizichezea nyele zake ndogo za kipilipili huku mkono mwengine akimpigapiga mgongoni.
"Mwanangu Hussein, mbona ni rahisi sana baba...! ni rahisi mwanangu twende ndani nikakuhadithie"
aliongea babaake Hussein na kumchukua mwanae mpaka chumbani kuwapisha wapangaji wengine waendelee na shughuli zao mida ile pale ukumbini waliposimama jilani na mlango wa kutokea.

"Mwanangu mamaako amekuacha ungali una miaka mitano lakini japo nilimkumbuka ila haikuwa sababu ya kunifanya niwe mnyonge na kukosa kabisa furaha. Unajua kwanini?"
alianzisha maongezi babaake Hussein pindi walipokua wamekaa kitandani pale chumbani kwao.
"hapana baba, sijui"
"Kwa sababu wewe ulikuwepo, unajua kwanini uwepo wako ulikuwa sababu ya mimi kukosa huzuni na kuwa na furaha mbali ya kuwa mamaako hakuwepo tena?"
"Hapana baba sijui."
"Kwa sababu wewe ndie ndugu yangu na yule alikuwa mke wangu na ndio maana ameolewa tena na mwanaume mwengine na hata huko anaweza kuondoka tena na kuolewa pengine."
"aaah, sasa baba na mimi mama sio ndugu yangu?"
"Hapana mwanangu, wewe ni zaidi ya ndugu yako kwa sababu wewe ni mwanae na yeye ni mamaako unapaswa kumuheshimu na kumtembelea mara kwa mara."
"sawa baba, kwa hiyo Kinoge sipaswi kumlilia kwa kua sio ndogo yangu na huko aendako anaweza kupata rafiki kama mimi na wakihama tena atamuacha na kwenda kupata rafiki mwengine ikawa hivyohivyo eeeh.."
"Ni kweli kabisa mwanangu, hutakiwi kumuweka sana moyoni mwanamke mwengine zaidi ya mamaako mzazi ambae hawezi kuondoka na kukuacha moja kwa moja hata uwe uweje, ila hawa wengine mwanangu usiwaamini kabisa na kuwaeka sana moyoni kwani wataweza kukusababishia maumivu na mateso makubwa pindi watapogeuka na kwenda kwengine."
"sawa baba"
"Ndio hivyo mwanangu hupaswi kuumia mimi nipo na hata kama nisipokuwepo amini wa kukusaidia kweli ni mwanaume mwenzako japo wanawake ndio wanaoonekana kuwa na mioyo mepesi ya kusaidia lakini bado msaada wa ukweli upo kwa mwanaume baba. haya nyamaza wewe ni mmwanaume shika hela hii kanunue chapati uje tunywe chai"
"Asante baba nimeelewa, nami nakuahidi sitoumia tena kwa sababu ya Kinoge"
aliongea Hussein na kufuta machozi baada ya kuchukua pesa kwenda kununua hivyo vitafunwa huku akimuacha na tabasamu zito babaake.

* * * * *

Safari yao iliwachukua masaa mengi garini siku hiyo tokea asubuhi ile walipoliacha jiji la Dar na kuingia jijini Arusha majira ya saa moja usiku ambapo safari bado iliendelea mpaka kwenye vijiji vya mbali na Arusha mjini na huko ndiko kulikokuwa na makazi mapya ambayo walihamia familia ya bwana na bibi Juma pamoja na mtoto wao kipenzi aliyeitwa Kinoge.
"haaa! mamaa ndio tumefika hapaa!!?"
aliuliza kwa mshtuko Kinoge pindi alipoyaangalia mazingira waliyofikia kwa nje ambapo muda huo wale vijana waliopakia vitu kule jijini walikuwa wanavishusha wakipewa maelekezo pa kuviingiza na bibi mmoja ambae ndie alikuwa mwenyeji wao aliyewapokea.
"Kinoge kwani wee unapaonaje si pazuri tuu.. tena huku kuna maembe na machungwa kibaoo unayopenda furaaaahi basii."
mama alijaribu kumliwaza mwanae ambae sasa alikuwa tayari kakunja uso kutokana na kuchukizwa na mazingira yale ya kijijini.
Aliangalia kwanza hakukuwa na umeme, hakukuwa na barabara nzuri, nyumba zilikuwa zipo mbalimbali hali iliyomuumiza Kinoge na kuona ni afadhali wangemuacha jijini Dar na rafiki ake Zungu asingekuwa mpweke kuliko kuletwa pale ambapo aliamini hata marafiki wa kucheza nao kama Zungu hawakuwepo.
"iiihhhhhhyyaaaaaaaaaa.. sipaaatakiii mimiiii... Nirudiisheeeni kwa Zunguuuuu"
alianza kulia kwa sauti Kinoge na mamaake kujitahidi kumnyamazisha wakati huo babaake alikuwa anasombelea vitu na kuvipanga kwenye ile nyumba pamoja na wale vijana.

Baada ya shuguli zote za uhamiaji kukamilika na ile gari waliyokuja nayo kuanza safari kuelekea mjini na hatimae sasa Kinoge aliamini kuwa kweli wamefika na hasa pale alipokuja babaake na kumwambia.
"Mwanangu Kinoge, maisha ni mlima leo unapanda kesho unashuka harafu maisha ni popote usiangalie mazingira kwanza ukayakimbia unafikiri hata kule mjini kulikuwa vile? kule napo kulikuwa kama huku.. Watu wakahamia na kupasafisha wakaishi na kupatengeneza hadi leo umepaona vile. Basi hata huku napo kutakuwa kama vile endapo tutakaa na kupatengeneza. Haya twende ndani ukasalimiane na bibi eeeh"
Maneno ya babaake ndio yaliyompa nguvu Kinoge na kupiga moyo konde kuwa tayari kuanza maisha mapya.

Bwana Juma ambae ni baba mzazi wa Kinoge yeye alikuwa ni mwalimu wa shule ya msingi na wakati huo alikuwa amepata uhamisho wa huko Arusha ambapo aliuomba yeye mwenyewe ili apate nafasi ya kurudi nyumbani kwa mamaake ambae alikuwa mzee na alihitaji uangalizi wake na kwa kuwa miaka mingi aliipoteza Dar mpaka anazaliwa Kinoge na kufikia umri ule alikuwa hajawahi kufika pale kijijini lakini sasa hawakuwa na budi wote kwa pamoja walihamishia makazi kijijini kabisa.
Na huo ndio ukawa mwanzo wa Kinoge kupotezana na Zungu.
 
DID YOU KNOW?!
814cca55c3c0d2d557e3e6a87bfc9c63.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom