Muziki: Kwanini Isiwe Mbili Wakati Una Moja
Ni Jumatano leo na inaishiria, naamini hakuna ubaya nikijiaminisha kuwa umekuwa na siku nzuri sana leo ambayo ni mwangwi wa namna siku ya kesho itakavyokuwa. Kama haikuwa siku yako, worry not, kesho ni siku nyingine tena na kama ada, jua litawaka tena. usisubiri sana though.
Hakuna ubishi kuwa wote, well nisifanye sweeping generalization maana huchelewi kutaka datum ambayo kiukweli haya ni mawazo yangu tu na nimejiamisha tokana na kuyakabili mazingira. Kuwa na wivu wa maendeleo si kitu kibaya, kukinzana kwa ajili ya kurahisisha maisha si jambo baya, kutofautiana kwa ajili ya kujenga umoja si jambo la kukemewa. Kila mmoja ana mawazo sahihi kwa wakati sahihi, na leo nakukumbusha tu kuwa kuridhika si tabia ya mwanadamu. Tufanye tunayofanya kwa ajili ya kujiletea maendeleo na kurahisisha maisha. Popote ulipo hongera sana kapuku kwa kile unachofanya.
Muziki sasa, wakati wanaanza walikuwa watatu Nhlanhla Nciza, Theo Kgosinkwe na Tebogo Madingoane baadaye Tebogo mwaka 2004. Wanaitwa Mafikizolo, na pamoja na kifo cha Tebogo bado wameendelea kufanya vizuri katika muziki wakichanganya mitindo ya kisasa na ile ya jadi na kuwafanya kuwa ni kundi la kipekee ambalo maonesho yake huhudhuriwa na wapenda burudani wengi.
Burudika Kapuku muheshimika na kumbuka, wewe ni mtaalamu unayelifanya Jukwaa hili liwe la kipekee.
Baadaye tutakuwa na chaguo la Wapendanao na leo mtaasisi mwenzangu kajaa kwa chaguo lake