Makapuku Forum

Apo anatakiwa Coutinho awe kati.. Mane kulia Salah kushoto... Firminho false 9. Utastarehe.
Ni kweli ila nazungumzia apate hizo 80 kibindoni alafu mane atibue kati make mapafu anayo kuanzia nyuma ya mstari mpaka ndani kabisa

Ila ikitokea kudaadeeekiiii jamaa hajauzwa na Mane arudii jamvini weka na guu la dhahabu la Salah daaadeeekii Liverpool kama nawaona wakitesa kwa zamu ...ila mabeki ndo nina wasiwasii ...

Ila msimu hujao patakuwa patamu make hata westham kaamua ...
 
7/Roger LaFontant
Alizaliwa mwaka 1931 na kufariki dunia 1991 akiwa na miaka 60
Huyu alikuwa kiongozi wa kijeshi huko Haiti ambapo mwaka 1991 alikuwa Rais kwa masaa 24 tu
Rais alijiuzulu hivyo Katiba ya nchi hiyo kumpa madaraka Jaji Mkuu Estha Pascal Trouillot ambaye aliitisha Uchaguzi wa kidemokrasia
Lakini bwana mkubwa Fountant akatumia fursa hiyo kufanya mapinduzi na kujitangazia Urais

Lakini ghafla bin vuuuu wajanja zaidi yake wajampindua ndani ya masaa 24 tu yaani wakati anaamka tu huko Ikulu hata swimming pool hakugusa

..............
 
Bado wiki mbili tu mbivu na mbichi tuzijue
 
6/Joseph Goebbels

Alizaliwa 1897 na kujiua mwaka 1945 akiwa na umri wa miaka 47 Huyu alikuwa Kansela wa Ujerumani kwa muda wa masaa 5 pekee mwaka 1945 May 1
Wakati Vita Kuu ya Pili ikiendelea na Adolf Hitler kuonekana kuzidiwa akaamua kumteua swahiba wake Goebbels kuwa Kansela akiamini ni Waziri wa Propaganda ndo pekee anayeweza kumuokoa jahazi lake linalozama

Lakini hata kabla hawajaanza propaganda zao za Hamphrey Polepole wakagundua wamezingirwa hivyo kuamua kujiua
Jamaa kaonja ukansela masaa yasiyozidi matano pekee

.........................................
Zitaendelea baadaye
 
 
Usijali Van jik na keita watastabilize defence... Keita probably the best defensive midfielder on the planet. Hao Leipzig na Southampton wanasumbua mahakama tu... Watachota mzigo Wanataka Hawataki.
 
Huyu wa siku 2 nae katisha
 
5/Boris Yeltsin Alizaliwa mnamo mwaka 1931 na kufariki dunia 2007 akiwa na miaka 76 baada ya kupambana na maradhi
Huyu mzee alijiteua mwenyewe kuwa Waziri mkuu wa Urusi mwaka 1998
Hii ilikuwa wakati yeye akiwa Rais na mgogoro wa kisiasa ukiwa umepamba moto hivyo akaamua kumpunguzia majukumu Waziri Mkuu kwa kujiteua yeye mwenyewe
Baada ya kukosolewa vikali na wananchi wake na wapinzani na kuambiwa ni dikteta na mzee wa kukurupuka akaamua fasta kuachia huo Uwaziri na kumteua mtu mwingine

Yaani ndani ya masaa manne tu...kukurupuka ni kubaya!!!

.............
 
4/Skender Gjinushi

Alizaliwa Disemba 24 1949
Huyu alionja Urais wa nchi ya Albania kwa muda kiduchu kama masaa mawili au manne tu
Ilimuwa mwaka 1997 baada ya uongozi wa kibepari wa Sali Berisha kushindwa uchaguzi wa kidemokrasia halafu kukataa kuachia madaraka hivyo Spika Slender akaamua kuchukua madaraka kwa mujibu wa katiba kuwa Rais wa mpito
Kisha Bunge la Albania likaamua kumtangaza mshindi halali wa Uchaguzi Mkuu Rexhep Meidani kuwa Rais mpya wa Albania

Hii ilifanyika ndani ya masaa manne pekee

...........
 
3/Carlos Manuel Piedra
Alizaliwa mnamo mwaka 1895 na kufariki dunia 1988 akiwa na miaka 93
Huyu alikuwa Rais wa mpito kwa muda kati ya masaa 2 hadi 5 baada ya kujiuzulu <b>Fulgencio Battista</b> mwaka 1959
Hii ilikuwa baada ya Makamu wa Rais naye kuingia mitini kufuatia mapinduzi yaliyoongozwa na vijana akina Fidel Castro, Camilo Confuegos n.k
Katiba ilikuwa ikimraka Jaji Mkuu mwenye umri mkubwa zaidi ndo achukue madaraka hivyo Piedra akatangazwa Rais mpya halafu fasta ndani ya nasaa machache akina Castro walikuwa washaiteka Havana hivyo akakimbilia Ubalozi wa Marekani na akina Castro kuchukua madaraka

Yaani alidumu kati ya masaa mawili au manne tu

..............
 
2/Siaka Stevens
Alizaliwa mwaka 1905 na kufariki dunia mwaka 1988 akiwa na umri wa miaka 82.....aliwai kuwa Rais wa Sierra Leone kuanzia mwaka 1971 hadi mwaka 1985
Huyu alikuwa Waziri Mkuu wa Sierra Leone mnamo March 21 1967 aliapishwa kuongoza Taifa hilo
Lakini ndani ya nusu saa tu waasi wakamzingira na kumkamata hivyo kuwa nwiaho wa utawala wake wa kiKassimu Majaliwa
Baadaye akafanikiwa kurudi madarakani kuanzia mwaka 1968

Yaani alitawala nusu saa tu mwaka 1967 kama Waziri Mkuu

............
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…