Makapuku Forum

Makapuku Forum

THE DOM

Sehemu Ya 4

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487 WhatsApp

Instagram....

Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←

SON OF PRESIDENT GU

Salehe aliondoka Ikulu na gari yake yenye usajili wa nymber za serikali, na gari hilo anaruhusiwa kuwa nalo ili usumbufu wa barabarani usitokee pale anapotakiwa kuwahi mahari fulani,..
Sahi alifika nyumbani kwake majira ya saa tano za asubuhi, aliweka kila kitu chake,... Kisha akalikagua vizuri lile begi aina ya dranka maalum la kuwekea vifaa vya upelelezi,... Sahi alicheka sana huku akitoa kifaa kimoja kilichokaa mfano wa Hard drive,... Huku akisema
"huu ndio utajiri unaotafutwa na serikali yangu,... The Discate Of Money,... Nazitaka hizo codes zake... AHahahahahahahah.."

Sasa cha ajabu na cha kushangaza, kumbe discate of money anayo sahi, au BB,.. Tena anataka na hizo codes zake,... Wakati huo anacheka kwa mbwembwe nyingi sana huku akiiangalia hio Discate ya noti ya shilingi lakini moja,.....
"How can get the codes?"
Salehe au BB alijiuliza atazipataje cedes hizo?.... Wakati huo sahi anacheka kwa dharau huku akiiangalia ramani ya Jengo la BOT lilivyo..

ENDELEA.............

Ama kweli ukijua kula na kipofu, basi utafaidi vingi sana, mana sahi ndie alie kabidhiwa jukumu la kuitafuta discate hio, alafu kumbe yeye mwenyewe ndio anayo katika mikono yake, tena wakati huo akiwa anapiga mahesabu ya kuingia, BANK OF TANZANIA (BOT) Ili kukamilisha codes za hio discate,.. Sahi au BB kwa jina la kazi aliweza kurudisha discate hio katika kisanduku maalumu cha discate hio kisha akakiweka katika dranka la vifaa vyake,...

Kesho yake asubuhi salehe akiwa na mtu mmoja hivi ambae kwenye uongizi hayupo, yaani ni mwananchi wa kawaida tu, huyo ndie aliekabiziwa jukumu la kumpeleka salehe katika kazi, na kitengo cha kwanza alipelekwa TSS kitendo ambacho kipo mjini kati lakini hakijulikani, hicho ni kitengo cha usalama wa taifa cha siri sana tena kinahusika na mambo mengi hususan upelelezi, na ndio mana salehe kaletwa huku mana kuna wapelelezi wenzake,... Na sio wapelelezi tu bali ni wapiganaji wazuri ila wao wamesomea Tanzania,

Mzee huyo yupo spesho kama baba wa salehe, na salehe yeye hajui popote anapo pelekwa hata huko TSS hapajui hata kidogo... Gari iliingia katika ghorofa moja safi sana, juu ni makazi ya wao wao wenyewe, lakini kwa chini sasa ndio kuna kila kiti, kwanza gari ikiingia geti linafungwa, afu papo hapo baada ya kulipita geti, mbele kuna kibanda, kama cha sevisi za gereji hivi lakini sivyo,.. Gari ikifika pale, hua panabonyea chini, kwahio makazi ya TSS yapo chini ya ghorofa katika underground, yaani chini ya ardhi ndipo makazi ya TSS yalipo,... Na mlango mkuu ni hio sehemu iliokaaa kama sevisi za magari kumbe ndio mlango mkuu wa kuingilia huko ndani,

Walipofika chini huko, yaani ni sehemu kubwa sana utafikiri ni nje, kumbe ni ndani,.. Hua mtu akishafika huko haulizwi sana kwasababu kama huhusiki huko, basi hata kwenye mlango mkuu pale hufiki, lakini kama umepita mlango mkuu basi unahusika,.... Sasa mzee ndio kipau mbele na hana wasiwasi, kwanza ni mtu mwenye pesa afu kaagizwa na kiongozi wa nchi, hivyo hakuwa na hofu kuingia ndani zaidi,.. Ukipita hapo kwenye maofisini kumejaa makompyuta ya kazi, na wakati huo watu wapo bize kana kwamba kila mtu kuna anchokitafuta au kuna kazi anaifanya, unaweza ukashirikiana na mwenzako lakini kila mmoja ana kazi iliomleta kama vile Salehe, kaletwa na kazi ya kutafuta discate na hapa sio kuwa discate ndio ipo ila awe na kazi ya kujizuia ili hata watu wanaomshtukia kuwa huyo ni nani, wakitafuta information zake wakute ni mwanafunzi wa TSS afu pia ni mwanafunzi wa TMA (TANZANIA MILITARY ACADEMY) Mana atakuwa anafanya kazi katika vitengo viwili kwa nyakati tofauti tofauti,... Lakini kazi hizo hazina maana kwake ispokua yupo kwa ajili ya kuitafuta discate,...
Mzee huyo alietambulika kwa jina la mzee Rashidy, na hata hilo jina sio lake ni ili tu kujifanya amemleta mtoto wake asomee upelelezi kwahio kitengo hiki kipo kwa ajili ya kukufunza practically jinsi ya kupeleleza,... Na pia hapo hapo kinafanya kazi, yaani unafunzwa huku unafanya kazi mpaka unakuwa afisa mkubwa hapo hapo na haruhusiwi kuacha kazi kirahisi mana ni kitengo kinachoijua nchi kwa undani zaidi... Mzee alionana na ofisa mkuu wa TSS yaani yule General mwenyewe ambae anaagiza tu,... Mzee aliongea mengi sana na General wa TSS, wakati huo mzee anaongea kule ofisini, huku Salehe yeye anazungukia ofisi za watu, na hapo wafanyakazi bado hawajamjua kama atakuwa mwenzao nini, kila akipita kwenye kompyuta anakuta wafanyakazi wanafuatilia information fulani kwa kutumia satalaiti,.. Yaani walikuwa bize sana hata kumuona mgeni hawamuoni,... Salahe aliipenda sana ile bize iliokuepo pale, na hapo hajui mtu hata mmoja,...

Huku ofisini mzee amemaliza kuongea na General wa TSS, sasa General anauliza huyo kijana yuko wapi, wakati huo sahi ndio kwanza yupo katikati ya maofisi ya watu,..
Mzee alimpigia sahi simu
"uko wapi wewe"
"nakuja mzee"
Sahi alitoka mbio mpaka ofisini, kwanza kaingia bila hata ya kupiga saluti, sio kwamba hajui ila kaambiwa aende kama mwanafunzi, hivyo ajifanye hajui ili ajue njia nyingi za kufanya kazi...
"ataweza kazi kweli huyu? Mbona kama kalegea legea hivi"
Aliongea general wa TSS, huku Salehe akijifanya kukakamaa kama mwanajeshi, lakini General akajua huyu kijana ni bure, hajui lolote...
Mzee rashidi alimaliza kila kitu na Salahe akawa kapata kazi au shule ya kujifunzi, mana unajifunza kuitumia kompyuta kwa ajili ya upelelezi zaidi, kisha unapelekwa practically kufanya upelelezi wa vitendo,...

Baada ya kumaliza hapo ikiwa ni mida ya saa sita za mchana,.. Sahi na mzee huyo aliekuwa kama baba yake wakiwa wanakwenda Airport kwa ajili ya kwenda Arusha kwenye chuo cha kijeshi, yaani anapelekwa zile sehemu nyeti za usalama wa taifa,... Walichukuwa ndege ya private kisha haooo, wakaondoka kuelekea TMA na huko ndipo atakapoanza kazi yake,.. Ilipofika saa nane ndege inatua arusha, kijijini munduli, ambako ndiko makao makuu ya jeshi,.. Hivyo katika mikoa yote mkiona kambi ya jeshi hayo ni matawi tu lakini makao makuu yapo arusha,.. Walipofika katika kambi hio au chuo hicho cha kijeshi, walishuka kama watu wakubwa fulani hibi, mana walikuja na private jet,

"salama afande"
mzee rashidi alisalimia kwa wakuu wa jeshi aliowakuta katika kambi hio, shamra shamra za mazoezi zilikuwa zikirindima, yaani kila kikosi na mazoezi yao, sahi sio mgeni na hivyo vitu tena kwa yeye anaona ni vitu vyepesi sana, mana ujeshi wake yeye kausomea korea, hivyo ana uwezo mkubwa kuliko mtu yeyote hapo kambini, na yupo kwa kazi maalumu..

"afande, kuna mgeni anahitaji kukuona"
"aingie"
Mkuu wa majeshi Tanzania nzima ndio anamruhu baba yake SALEHE aingie ndani,... Mheshimiwa Nyange akiwa katika kiti chake cha heshima ya ukuu wa jeshi Tanzania nzima,... Sasa sahi kama kawaida yake ya kubaki nyuma, yaani mzee anaingia ofisini yeye kabaki nyuma,.. Saa ngapi asianze kuizunguka hio kambi ya jeshi, palikuwa na vijana wengi sana ni zaidi ya wanafunzi elfu moja ukijumlisha na walimu, wenye vyeo vyao.... Sasa wanajeshi bado hawajamjua sahi kuwa ni nani afu kavalia nguo zkisharobaro hivi, saa ngapi mwanajeshi mmoja hajamtamani sahi,... Yaani ilimradi kumkomoa mana alikuwa akiangalia amgalia mabogi ya magari ambayo ni magari ya kijeshi, sasa sahi alijifanya kuchungulia... Kwanza alishtukia kavutwa kisha kawashwa kofi,
"umemueka baba yako uko chini ya gari"
Aliongea mmoja wa makamanda huku makamanda wengine wakizidi kujaa eneo la tukio,.. Sahi kaambiwa awe mpole, ajifanye hajui, sasa kama unavyojua maonevu ya wanajeshi yalivyo... Kabla sahi hajajibu kasukumwa na mtu mwingine,... Papo hapo akaanza kupewa zoezi la kushusha giabox la gari peke yake, kitu ambacho hakiwezekani kushusha giabox la kalandinga la jeshi peke yako, eti kisa alikuwa anachungulia....
"broo siwezi eti"
Wakati huo sahi akiongea hayo tayari keshalioga vumbi jinga sana, nguo zake za usharobaro tayari zimekuwa kama nguo za kichaaa.... Sasa walipoona anazidi kukataa, likaletwa galeni la oili chafu, yaani hawana utani na hata sahi anajua yaani hata ni kuchomwa mwanajeshi akiamua anakuchoma kweli,... Lile dumu lenye oili lote lilimwagikia yeye, uso mzima kwa mweusi,.... Sasa huku mzee keshamaliza kuongea wanageuka nyuma hawamuoni kijana husika,... Nyange alijua tu tayari kimeshanuka huko nje, mana anawajua makamanda wake walivyo, yaani wakiona raia hapa kambini kama haeleweki wanampa adhabu,... Kweli walipotoka wanaona kuna mahari kuna watu wengi sana, yaani wanajeshi wamekusanyika sehemu moja wakimchezea mtu mmoja yaani wana hamu ya kutesa ile mbaya,...
"waamuru basi vijana wako wamuache"
Aliongea mzee huyo ili sahi aachwe, lakini Nyange hakutaka kufanya hivyo
"kijana wako kaja kujifunza mafunzo ya kijeshi, na kisheria alitakiwa kuanzia JKT, lakini kwa kutumia shotkati zenu, umemleta huku.. Sasa tulia akaribishwe"
"lakini imetosha afande, hebu ona alivyo kama chizi"
Mzee rashidi anajua sahi sio mtu wa mchezo ila inabidi afiche siri,... Sasa mkuu wa majeshi mheshimiwa General Nyange, alipofika alimuuliza sahi,.. Na Wakati huo sahi hata kuona vizuri haoni kutokana na ile oili chafu aliomwagiwa, na hata sura yake haionekani vizuri kwasababu ya hio hio oili
"huo ndio ukamanda kijana.... Karibu kambini kwetu"
Aliongea general huyo, huku akitaka kuruhusu waendelee kumpa mazoezi
"afande naombeni mnisamehe sirudii tena"
Sasa ghafla general akasita kuondoka baada ya maneno hayo kutoka katika kinywa cha sahi,..
"ebu rudia tena hio sauti yako"
General alimuuliza sahi kwa mara nyingine,..
"nisamehe afande"
General alipatwa na kichaa,...
"we mzee, huyu ni mtoto wako"
Nyange alimuuliza mzee Rashidy feki,
"ndio kwani vipi"
"hapana.... Nyie Hebu muosheni huyu kijana nimuone"
Heeeee kumbe general anamjua sahi, lakini sasa kumbe sio General tu, bali kuna vijana wengine wa kijeshi wanaijua sauti hio,....
"muosheni nimuone,... Fanyeni haraka"

Je? Sahi ni nani??? Mbona kila kona anajulikana??? Na je kwanini general anamjua sahi,.. Huyu sahi ni NANI??

ITAENDELEA.....
 
Ni faida gani basi mliyopata siku zile kwa mambo hayo mnayoyataharikia sasa? Kwa maana mwisho wa mambo hayo ni mauti

Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru na kuwa mbali na dhambi na kufanywa watumwa wa Mungu mnayo faida yenu ndiyo kutakaswa na mwisho wake ni uzima wa milele

Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu
WARUMI 6:21:23

Muwe na asubuhi iliyo njema mbarikiwe sana
Kweli nimeanza kuamini Yale Maneno uliyoniambia kule mtaa wa pili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom