Makapuku Forum

THE DOM

Sehemu Ya 3

Mtunzi..... MoonBoy

Simu No. +255714419487 WhatsApp

Instagram....

Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←

SON OF PRESIDENT GU

"I love my mom"
Aliongea huku akilia kiume, ilionekana mama yake amefariki dunia...

Kesho yake akiwa yupo njiani kuelekea Ikulu, kwa ajili ya kupewa kazi yake, wakati huo alikuwa akiendesha gari yenye preti Namba ya usalama wa taifa, yaani ni ya serikali...
Maramoja kijana alifika Ikulu na kuingia mpaka ndani,... Alimkuta waziri mkuu, pamoja na makamu wa rais, huku mlinzi wa rais akiwepo nyuma ya raisi, maana yake walikuwa watu wanne na kijana huyo alikuwa mtu wa tano,...
"shkamoni"
Alisalimia viongozi wote aliowakuta hapo lakini kabla hajakaa, alishangaa vitanzi vyake kumwagwa mezani,.. Lakini kumwagwa kwa vitanzi hivyo sio kitu, kitu ni kwamba vitanzi hivyo vilimshangaza sana kijana huyo, hivyo alishikwa na shauku ya kuuliza
"kwanini imekuwa hivi"
Aliuliza kijana, ambae mpaka sasa hatujalijua jina lake,.... Na hapa ndipo tutakapo lijua jina lake rasmi na kazi yake, bila kujua yeye ni nani na alikuwa nani hapa nchini.....

ENDELEA.........

Alipofika kijana huyo, mara moja rais alimmwagia vitanzi vyake ambavyo alivitoa kwa siku ya jana, na hio ilikuwa ni kwa ukaguzi tu na havikuwa na tatizo lolote, kwani hata kijana huyo alijitetea kwa kusema vitanzi hivyo alitengenezewa na yeye mwenyewe mheshimiwa rais,.. Hivyo havikuwa na tatizo lolote, lakini kijana alipofika ikulu na kuviona vitanzi vyake alishangaa na kuuliza
"kwanini imekuwa hivi"
Mheshimiwa raisi alitoa macho huku akimuuliza,
"jana hujapigiwa simu"
Ilibidi kijana akae kimya kutokana na majibu aliopewa na Mheshimiwa raisi, sasa haijulikani jana alipigiwa simu iliohusu nini mpaka kukubaliana na maneno ya raisi,... Kijana huyo ambae ndio leo tunaanza kumjua kupitia vitanzi hivyo, kwa jina la SALEHE RASHIDY KINGAZI (SAHI)

"utakuwa na kazi mbili... Ila kazi hizo zitakuwa kama vile unajifunza"
Aliongea rais huku Salehe au sahi akiwa tayari kwa kuuliza swali kwa raisi,
"sababu ya kazi mbili ni nini"
Aliuliza sahi huku akisubiri majibu toka kwa mkuu wa nchi
"THE DISCATE OF MONEY IS LOST"
Aliongea raisi kitu kilichomfanya sahi kushtuka sana, mana kifaa hicho ni kifaa maalum kama code ya kuchapishia pesa mpya iliotakiwa kutoka kimepotea,.... Yaani hicho kifaa ndio kina code za pesa mpya ya Tanzania, sasa hio discate inafungwa katika mashine ya kuchapishia pesa, ili itoke pesa ya kitanzania lazima hio discate iwepo,.. Tanzania wanataka kutengeneza noti moja ya shilingi Laki moja, na kila kitu kilishakaa sawa, kilichobaki ni kutangaza tenda katika makampuni ya kuchapisha pesa huko nchi za nje, na wakishakubaliana ndipo wanapewa hio discate ambayo ndio ina muongozo mzima wa pesa hio mpyq... Yaani ukiifunga katika mashine, ndio inatoa mfumo mzima wa laki moja ya Tanzania,.. Kama vile Computer bila Hard Disk ya Windows, basi computer haiwezi kuwaka maisha yako yote, mpaka uweke Hard Disk ya Windows na kama haina Windows utatakiwa kuweka CD ya Windows ili kuweka Windows computer ifanye kazi... Sasa ni sawa na mashine ya kuchapishia pesa.. Na mashine hizi zipo aina mbili, kuna mashine kubwa spesho kwa ajili viwandani kabisa yaani zile zinazopokea tenda za kuchapisha yaani kiwanda kinachojulikana dunia nzima... Afu kuna mashine ndogo, hii ni mashine binafsi, na haziuzwi tu hovyo hovyo na bei yake sio ndogo,.. Hizi mashine ndogo zinakuwa zipo spesho kwa nchi inayotaka kujichapishia wenyewe kutokana na maelewano na kampuni ya IMF, hivyo sio rahisi kuwa nayo mana inauzwa gharama kubwa afu ni mlolongo mpaka kuiweka katika nchi yako..

Lakini sasa pia kuna matajiri ambao wanaweza kumiliki mashine hizo kupitia njia za kona kona, na wakaweza kuzipata, sasa kupata mashine sio kazi, kazi ni kuwa na hio Discate,.. Ukiwa na discate of money, Tayari wewe ni tajiri wa dunia na hakuna atakae kuweza,.. Sasa discate hio yenye ukubwa wa HARD DRIVE au HARD DISK, kwa wale wataalamu wa computer wanavijua hivi vifaa,.. Sasa hiki kifaa ndicho kilicho potea, na kilikuwa kimehifadhiwa BOT (Bank Of Tanzania)

"mkuu, unachokiongea ni sahihi kweli"
"tena hakukuwa na uvamizi wa aina yeyote, inaonekana kuna utaalamu wa uzimaji wa CCTV na aliochukuwa ni mtu anaefahamika na anaejua siri ya shelfu lililowekea Discate hizo"
"kwahio, hizo discate zimebaki ngapi"
"discate zilizobakia ni za Elfu kumi, Elfu Tano, Elfu mbili, Elfu Moja, Na shilingi Mia tano... Hizo ndizo discate zilizobakia, ila hio discate mpya ndio iliopotea, na ni hatari sana mtu binafsi kuingiza pesa hio katika mzunguko, ni hatari sana pale atakapo pata code zake"
Aliongea mheshimiwa rais, kana kwamba pamoja na upotevu wa discate hio bado kuna ugumu wa kuchapisha pesa, mana code number haikuchukuliwa.. Na code number ipo pale pale kwenye shelfu la kuhifadhia hizo discate, na kila discate imekaa pembeni na code number zake,... Sasa mtu aliochukuwa alichukuwa kwa pupa, kana kwamba akasahau kuchukua code zake, na code hizo zipo kwenye kifaa maalum, ambapo pale unapotoa discate, basi na code number zake zipo kwa chini, na sio za kunakili kichwani bali unachukuwa na kifaa chake chote, mana ni number nyingi sana zapata kama number 100 hivi zilizochanganywa na herufi mfano wa code za Facebook kuna wakati ukiingia Facebook kuna Codes wanazitaka na umewekewa juu ya kisanduku uziandike, sasa kwa hii discate zinafika numbers 100, zilizochanganywa na herufi, hivyo huezi kunakili kwa haraka kama unaiba, na hata wakati wa kupeleka hio discate kule Ujerumani ni lazima upeleke na codes number zote yaani unaikabidhisha kwenye kampuni hio ya uchapishaji wa fedha pamoja na codes zake, na wakimaliza kazi, unarudishiwa discate yako na codes zake,.. Usubiri kupeleka kwa wakati mwingine, na kila nchi ina discate zake na codes zake... Sasa huku BOT kilichobakia ni Codes za discate ya shilingi laki moja, yaani noti moja ya laki, sasa discate ndio ilioibiwa... Na urahisi wa kupata codes ni asilimia 90 kwasababu aliochukuwa anaweza kurudi na kuchukuwa zile codes,.. Mana unapofunga hio discate itakuonyesha kwenye screen ya mashine kuwa unahitajika kuweka codes ili discate hio ianze kazi, na wakati huo matirio ya fedha yapo tayari katika mashine...

SAMAHANINI SANA WADAU, NIMETOA MAELEZO MENGI SANA LAKINI NI ILI MUELEWE VIZURI KINACHOFATILIWA NA KIKOJE NA KINA KAZI GANI NA KWANINI KINAFATILIWA,.. SIWEZI KUSEMA TU DISCATE WAKATI HUJUI DISCATE HIO INAKAA WAPI NA KAZI YAKE NINI, NITAKUWA SIJAKUTENDEA HAKI YA KUSOMA SIMULIZI HII.... HIVYO TUTAVUMILIANA TU ILI TUSIDANGANYANE SANA,

"kwahio unataka kuniambia codes bado zipo"
"ndio, mwizi hajaweza kuchukuwa codes, na ni lazima arudi"
Aliongea rais, huku Waziri wa fedha akiwa ndio anaingia katika kiakao,..
"shkamoo "
Sahi Alimsalimia waziri wa fedha huku waziri huyo akivuta kiti na kukaa,... Lakini alipofika pale, ghafla mada ilibadirika, mana katika watu wanaohisiwa vibaya hata yeye yumo anatakiwa kufanyiwa upelelezi hivyo hapaswi kumjua sahi,...
"Marahaba kijana.. Habari yako"
"nzuri"
"habari yako mheshimiwa rais"
Waziri wa fedha alimsalimia raisi
"salama tu hali yako"
"aahh tunamshukuru mungu kwa newma zake, ila huyu ndie yule kijana uliosema anakuja"
"hapana, huyu ni kijana wangu, wa yule mama yenu wa pili"
Aliongea raisi, huku akimnyooshea sahi kidole,...
"aaahhh kumbe una vijana wakubwa sana Mheshimiwa hongera zako"
"aahhh ndio vijana wetu hawa"
Waziri alisema kumbe mheshimiwa ana vijana wakubwa sana, hivyo inaonekana kuna mtoto wa raisi mwingine tofauti na huyu aliemtambulisha, na je huyu ni mtoto wa rais kweli au kazuga zuga tu..
"haya, mimi nilikuwa napitia tu hapa nadhani wacha nielekee ofisini kwangu"
"sawa kazi njema"
Aliaga wazi huyo huku tukibakiwa na Waziri mkuu, na makamu wa rais, na sahi, pamoja na mlinzi wa rais,..

"sasa basi, najua wewe hujamaliza masomo yako, nadhani bado miezi mitatu uweze kumaliza mafunzo yote, sasa tunataka uifanye kazi hii ndani ya mwezi mmoja, tuione discate ikiwa mikononi mwako"
"sawa, nitaifanya kazi kadri ya uwezo wangu"
"sasa, ili usitiliwe mashaka, tunakupeleka jeshini, na pale jeshini utakuwa kama mwanafunzi, tafadhali sana naomna usilete ujuaji mana watakushtukia,... Na Sababu ya kukupeleka jeshini yaani military ya kijeshi, ni ili wajue shughuli zako za hapa mjini... Na pia hutoishia jeshini tu, bali nitakupeleka katika kitendo cha usalama siri cha TSS (TANZANIA SECRET SERVICE) kitengo hiki, hakijulikani Tanzania ispokuwa viongozi wakubwa.. Na kitambulisho chake hiki hapa... Nadhani cha jeshi unacho kwa hapa Tanzania.. Hivyo utakuwa na kazi mbili kwa nyakati tofauti tofauti,.. Wiki moja jeshini, wiki moja mjini TSS, serikali imekukadiria bajeti ya Tsh milioni 500 mpaka pale kazi itakapoisha... Na ukishindwa ndani ya huo mwezi mmoja serikali itakuchagulia adhabu ya kukupa.... Wish you a good Luck"
"ok.. Nimekuelewa mzee, ila napelekwa na nani katika vitengo hivyo"
"ili usijulikane kuwa umeletwa na raiso, kuna raia wa kawaida tu atakupeleka military ya kijeshi, kama vile mzazi wako.. Na pia kule TSS atakupeleka vilevile kama mzazi wako.. Kikubwa hutakiwi kujulikana umeletwa na kiongozi gani"
Aliingea raisi huku akiamka na kutaka kuondoka
"afu nimesahau,.. Jina la misheni utatumia BB yaani (BLACK BOY) utavaa mavazi meusi mwanzo mwisho unapokuwa katika kitengo cha TSS na ukiwa military utavaa nguo za jeshi za kawaida... Lakini wiki ya mjini utavaa nguo nyeusi kuanzia juu mpaka chini.... Alafu hio kitu haruhusiwi kuvua na hutakiwi kujulikana wewe ni nani.. Umenielewa"
"nimekuelewa mkuu"
"nitakuwa nakupa misheni kwa kutumia Transmission ulio nayo katika skio... Jina langu la misheni nitatumia GU.... Hivyo utakaposikia neno GU, basi ujue ni mimi... Kama una swali uliza"
"hapana, sina swali... Ila nilitaka kujua, kuna baadhi ya misheni utakuwa ukinipa, je nikiwa katika wiki ya jeshini itakuwaje na misheni itakuwa ya mjini"
"tutajua cha kufanya pale litakapotokea swala kama hilo... Ila chunga sana huruhusiwi kuwa na wanawake... Mwanamke ni njia moja wapo ya kuvujisha siri zako... Kuwa makini na hawa watu... Na vitengo vyote, utakwenda kama mwanafunzi... Huku ukijua unachokifanya"
"Yes Sir"
Sahi alinyanyuka na kupiga saluti kwa raisi, wakati huo makamu wa rais na waziri mkuu wakitikisa kichwa kuashiria kijana yupo shupavu na makini zaidi..., alipoondoka raisi, kuna kijana alileta begi lililojaa vifaa maalum vya upelelezi.. Kama Rader, Computer ndogo, wireless network, na kuna kifaa kidogo cha satalaiti, bila kusahau miwani inayoweza kuscani mwili wa mtu na kugundua ameficha nini katika mwili wake,....

Salehe aliondoka Ikulu na gari yake yenye usajili wa nymber za serikali, na gari hilo anaruhusiwa kuwa nalo ili usumbufu wa barabarani usitokee pale anapotakiwa kuwahi mahari fulani,..
Sahi alifika nyumbani kwake majira ya saa tano za asubuhi, aliweka kila kitu chake,... Kisha akalikagua vizuri lile begi aina ya dranka maalum la kuwekea vifaa vya upelelezi,... Sahi alicheka sana huku akitoa kifaa kimoja kilichokaa mfano wa Hard drive,... Huku akisema
"huu ndio utajiri unaotafutwa na serikali yangu,... The Discate Of Money,... Nazitaka hizo codes zake... AHahahahahahahah.."

Sasa cha ajabu na cha kushangaza, kumbe discate of money anayo sahi, au BB,.. Tena anataka na hizo codes zake,... Wakati huo anacheka kwa mbwembwe nyingi sana huku akiiangalia hio Discate ya noti ya shilingi lakini moja,.....
"How can get the codes?"
Salehe au BB alijiuliza atazipataje cedes hizo?.... Wakati huo sahi anacheka kwa dharau huku akiiangalia ramani ya Jengo la BOT lilivyo..

Je? Kwanini sahi, anamiliki Discate hio,.... na je? Kaipataje na wakati hakuepo nchini zaidi ya miaka mitatu sasa??.... Huyu Sahi ni mtoto wa nani, na discate kaipata wapi??.. USIKOSE

ITAENDELEA.....
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…