DHK. ...
KWA WALE WAPENZI WA KAHAWA
.......Unywaji wa kahawa hurefusha maisha
Ni habari njema kwa watumiaji wa kahawa, kwani utafiti uliofanywa hivi karibuni , umebainisha kwamba watu hao wana uwezekano wa kuishi maisha marefu zaidi.
Utafiti huo unaeleza kwamba watu wanaokunywa kati ya vikombe viwili na vitatu, hupunguza hatari ya kifo kwa asilimi 18 wakilinganishwa na wale wasiofanya hivyo.
Kiongozi wa utafiti huo, Profesa Veronica Wendy Setiawan wa Chuo Kikuu cha Southern Califonia (USC), alisema licha ya tofauti ya mfumo wa maisha, hali iko hivyo kwa makundi yote.
Matokeo hayo yanaonyesha uwapo wa uhusiano mkubwa kati ya matumizi ya kinywaji hicho na maisha marefu kutokana na kupunguza uwezekano wa maambukizi ya maradhi ya moyo, saratani, mfumo wa kupumua, kisukari, kiharusi na figo.
Utafiti huo uliwashirikisha zaidi ya watu 185,000 wa asili tofauti kwenye majimbo mbalimbali nchini Marekani na matokeo yakawa sawa.(CNN)