Muziki: Jina Lako Linafanana na Muziki
Ni usiku sasa na muda unakimbia kweli kweli, hizi mbio za leo ni za kuitafuta Furahiday. Pamoja na siku kukimbia sana leo sitoacha kukusalimia
Kapuku mheshimika maana salamu ni nusu ya kuonana, wale wa Radio Tanzania Daslam mnakumbuka hili. Usijidai mdogo wakati umezaliwa miaka ya 80, 90s, miaka hii yote RTD ndo ilikuwa radio namba moja na vipindi maarufu vilikuwa Mama na mwana na kile cha Salamu kwa Wagonjwa.
Hivi unajua kuwa uwepo wako hapa unaniongezea maarifa mengi sana, maana najifunza kwa kila unachoandika. mtu makini huheshimu na kujifunza kile ambacho mwingine anaandika au kusema. na hili ndilo linaifanya KF kuwa ni sehemu ya kipekee kabisa, full maarifa, full kuelimishana, full kuloviana, full kujamiiana (socializing stop tantalizing) na zaidi full kuwa pamoja bila kujali nani ni nani.
Muziki sasa, sijachelewa sana leo kuleta muziki na hata kama nimechelewa ni kwa sababu lingekuwa ni tumbo langu peke basi ningewahi lakini kuna matumbo matatu yani nisiporudi nimebeba japo mkate jua staftahi nitastafuhiwa mimi. Kifupi nilikamatika lakini hakijaharibika kitu.
Hivi unajua jina lako linafanana na muziki, ziba pua halafu litamke taratibu, na ukiweza litamke kwa kupiga mluzi (kama una mapengo jaribu mbinu mbadala ya kubananisha fizi na mdomo wa juu, halafu litamke taratibu. Hapo utasikia jina lako linafanana na muziki. Lisipotamkika kimuziki basi inawezekana wakati unaumbwa wazee wako walikuwa wanasikiliza taarifa ya habari.
Kama huamini basi hebu sikiza huu muziki Whats love got to Do, kama hutasikia Husnaaaaa na hii ni kwa
husna muba
Nakupenda sana Kapuku