Makapuku Forum

TOP TEN
Week end inaendaje wanangu?
Kama vipi njooni Mabibo City Nite Club tule gambe wana....maisha yenyewe mafupi kama stuli !!
Kama kawaida Ijumaa tunamaliza week kiburudani au kiudakuudaku zaidi maana ndo mwendo wetu siasa zinachosha

Umaarufu bila pesa ni kazi bure au ukipenda sema ni kuuza sura tu
Kwa Bongo wanawake maceleb wenye mkwanja ambao unaeleweka ni Lady Jaydee(komando Jide} na Jokate Mwegelo {Kidoti) binti kutoka [Loyola High School inayopatikana Mabibo ndo alisoma hapo akiwa kama dada Mkuu(kiranja) pia aliwahi kutikisa Miss Tanzania

Sasa wana nawaletea wanawake kumi mashuhuri wenye mpunga wa maana huko mamtoni sana sana kwa Mzee Donald Trump

************************
Dola 1 ya USA= 2240 Tsh
***************************
Karibuni
........
 
10/Angelina Jolie Ni mcheza filamu maarufu huko Hollywood nchini Marekani
Ni demu wa Brad Pitt na walijaaliwa hadi kupata mtoto/watoto pamoja yaani kitu kimelipa...pia wameasili watoto kutoka sehemu mbalimbali duniani ikiwepo kutoka Afrika
Kupitia filamu anaingiza mkwanja mrefu kama urefu wa treni ya Mwakyembe inayozurura huku Joto City
Ana mpunga unaokadiriwa kufikia USD 120 Milioni
.....
 
9/Judge Judy Sheindlin Alizaliwa Oktoba 21 1942
NiJaji,mwendesha vipindi vya luninga na pia ni mtunzi wa vitabu(maandishi huishi milele)
Ana Shahada kutoka chuo kikuu cha American University na pia kupata mafinzo ya uwakili kutoka New York Law School ila usishangae kwa Nchi zilizoendelea kuwa na madegree siyo kitu cha kutambia mitaani sio kama akina Profesa Lipumba wanavyotusumbua huku
Ana utajiri unaokadiriwa kuzidi USD 230 Milioni
. .......
 
8/Rihanna Amezaliwa Februari 20 1988
Huyu dada amewahi kuvaa gwanda katika Jeshi la Marekani halafu akaamua kuacha
Kawahi kuwa demu wa Chris Brown wakamwagana baada ya kudundwa vya kutosha kiasi cha kuumuka sura
Ndiye nyota wa kibao cha Umbrella ila pia vipi vingine kibao vikali kami vile Diamonds na kingine matata cha Rude Boy
Ana utajiri wa zaidi ya USD 245 Milioni
.......
 
Nampenda huyu mdada
 
 
Itabidi niitafute
 
7Mary Kate & Ashley Olsen
Wamezaliwa Juni 13 1986
Hawa ndo mapacha maarufu zaidi duniani ila siyo tu umaarufu bali pia ndio wenye mpunga mrefu duniani
Wanajihusisha na vipindi vya televisheni ila wana biashara kibao zinazowaingizia mkwanja wa kutosha
Wanamiliki kampuni ya Dualstar
Wana mpunga unaokadiriwa kufikia USD 350 Milioni
......
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…