Makapuku Forum

Muziki na Mapovu Makanikia bila kuwa Makini

Utatoa hutoi, ndivyo kibwagizo cha singeli moja inasikika kwa mbali, najipitia zangu tu kurudi home maana tayari nishaingiza siku kwa deni. Yeah, kukopa ndo ubinadamu huo, tunakopa na kukopesha, tunakopeshana kuanzia mali hadi mwili. Hongera kwa mliokopa leo. Tunakopesheka.

Jumatano inaenda kuisha, na bila kujali muda huu tunarudi kuburudika na muziki huku kama kawaida maneno sikiza mwenyewe , kipengele kinaangalia utamu wa gitaa.

Nilitamani kuweka kibao cha kukataliwa kubaya kukataliwa matesooooo matesoooo lakini nikagundua kuwa nitakuwa ninajiumiza bure bila malipo. Ninasonga na usiku huu tumewaona wote wenye shobo walioamua kubugia foma gold (bila makanikia) na spaleta moto ili kushambulia jukwaa hili, tuwakaribishe. Tuko pamoja

Bendi ya Msondo (kwa ombi maalum la Shunie na anko lee empire ) inaweza kuwa bendi maarufu kabisa kwa hapa Tanzania tangu tumepata Uhuru, imebadili majina mara kadhaa kutokana na umiliki na mambo kadhaa lakini mtindo wake umebaki kuwa alama yake, msondo ngoma.

Inaundwa na wanamuziki maarufu na badhi washatangulia mbele ya haki lakini nani anaweza hata kuwakumbuka wapiga gitaa walionogesha sauti za kina Guruma, Bitchuka, Moshi, Jumbe na wengine, sana sana mtamkumbuka Romario na kidevu chake akipuliza midomo ya bata.

Kwenye clip hii hebu angalia na usikize gitaa la mtaalamu Said Mabera, lakini pia wapigaji wengine maarufu wa Msondo ni pamoja na Uvuruge bila kumsahau Pangamawe Ridhiwani

Burudika mdau na nianwapongeza wote mliomeza foma gold bila makanikia kuisema makapuku forum bila kutafuata ukweli wake. Hongereni

 
Got u
 
Umerogwa😡, niweke silaha chini ili niitwe muoga!! Wewe wa wapi wewe? nimerudisha majeshi nyuma narudi kujipanga. Maana inaonekana BH kuna kina nyie mnamtakia mema hamtaki awe na mimi sasa furahini sababu nimerudi kujipanga. Ni suala la muda tu
[emoji23] [emoji23] [emoji23] binamu hurumia mbavu zangu naonekana chizi
 
Binamu yangu asante jamaan
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…