Makampuni Makubwa Yatikisika

Makampuni Makubwa Yatikisika

NMB pia nao wametangaza kuhamisha share zao, ila wao nadhani sio kuyumba kwa biashara,wajuvi wataifafanua hii.
 
Hilo kundi linamsubiri 2020 limshughulikie vilivyo,na atakiona cha mtema kumi

Yapo makundi mengi ukiachilia mbali hilo
Huko ni mbali sana chamoto atakiona kuanzia 2019 wenzake watakapoona hawana cha kupoteza
 
Unapandisha kodi af unaua nguvu ya manunuzi unateg3mea nini?
kodi sio rafiki na biashara ni ileile.....
mfn unakampuni ya usafrishaj una gari 50 ulkua unalpia @lak3 each sasa piga esabu ni kiasi gani unalipia asaiv baada ya kuamishiwa kwe Mafuta? na biqshara baada ya Kukua znazid kudumaa

Wataka kUkimbia na auna brek....what do u expect?
 
Sio ishara nzuri kwa makampuni makubwa kuyumba .....

Lakini tutafakari kwa makini nini kimebadilika Tanzania?.

Kama ni kodi je uko nyuma walikuwa wanalipa kodi?.

Kama ni ndio kwa nini wanayumba?......

Maswali yanabaki kuwa na wao kuna sehemu wamekosea pia......

Maana kila mmoja hapo naona anguko lake ni tofauti na la mwingine......
Hakuna mwaka ambao mfanya biashara hakulipa kodi. Hivi wwe ni mfanya biashara?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kati ya makampuni uliyoyataja ni yapi yanaongoza kwa kulipa kodi nchini?
Ni kweli!
Kodi ni ile ile. Kilichobadilika ni ukusanyaji wa kodi hakuna kukwepa kama kipindi kilichopita!
 
Mabadiriko ya kisiasa na kiuchumi huambatana na athari chanya na hasi.Maboresho ya sera,sheria,usimamiaji sheria,utekelezaji maazimio na usimamiaji.Athari chanya na hasi haziepukiki pindi mapinduzi ya taratibu za kimaisha zinapobinuliwa kwa maslahi tofauti kitaifa na kiuongozi.

Taasisi na makampuni mengi za kibiashara {uwekezaji} zimeyumba hata kupelekea kufunga biashara,kupunguza wafanyakazi,kusimamisha biashara,kuuza hisa na kutafuta wabia mbadala.lakini pia zipo kampuni ambazo zimewekwa chini ya uangalizi wa taasisi za fedha na nyingine kuwa katika mchakato wa kufirisiwa.

Mfano wa taasisi na makampuni tajwa ni Airtel {Redundancy},TBL{Redundancy},Home Shopping {Change Name},GSM Malls {Punguza Wafanyakazi},GSM Media {Imefungwa},Living Room {Kupunguza wafanyakazi},Subway-Diamond Plaza {Fungwa},IPP,SSB,Cocacola,Bravo {redundancy},BMTL {redundancy},Freightworld {redundancy},MTL,DSM Collidor,Quality Group,Abla Properties {...},Spencon {winding up},Acacia {Makinikia},Twiga Bancorp {Supervisory},Gapco {Sold to Total} n.k..

Kama taifa yatupasa kuhakiki faida na hasara za muda mrefu za mabadiriko,marekebisho,maboresho na ufinyangaji wa michakato,sera,usimamizi,utekelezaji wake.Ninayo imani yamkini ipo nia thabiti kabisa ya kila linalofanywa sasa kwa faida za kizazi kilichopo na kijacho hivyo basi tathmini ifanyike ili kulinda biashara halali zilizopo pamoja uwekezaji wa mabilioni na wenye athari mtambuka {ajira,kodi,n.k}.
Waliokuwa wanaishi kama malaika wataishi kama mashetani.
 
Sio ishara nzuri kwa makampuni makubwa kuyumba .....

Lakini tutafakari kwa makini nini kimebadilika Tanzania?.

Kama ni kodi je uko nyuma walikuwa wanalipa kodi?.

Kama ni ndio kwa nini wanayumba?......

Maswali yanabaki kuwa na wao kuna sehemu wamekosea pia......

Maana kila mmoja hapo naona anguko lake ni tofauti na la mwingine......
Kupunguza wafanyakazi,kufunga makampuni na kuweka baadhi ya makampuni chini ya usimamizi ni dalili tosha ya uchumi uliokwama.

By the way nchi haiwezi kuimarika kiuchumi kwa makusanyo ya kodi,faini na tozo mbalimbali tu. Lazima nchi ijikite kwenye kuongeza uzalishaji na tija katika sekta zote kama kilimo,viwanda,uwekezaji n.k

Tusipoangalia na kuzitathmini sera hizi vizuri tutaendelea kuota kuhusu viwanda huku sera zetu ziko against industrial economy.
Kazi ya serekali ni kutengeneza sera rafiki kwa wawekezaji zenye tija kukuza uchumi sio kukomoana kama hiki kinachofanyika now

Sent using Jamii Forums mobile app
 
= Mabadiliko
= mabadiliko

Hujuwi namna ya kuwacha nafasi "spacing" unapoandika?

Huwa mna mawazo mazuri lakini mnapoyawasilisha kwa kukosea wapi pakuweka R na wapi pakuweka L ladha yote ya kusoma inaondoka.

Hivi mlienda shule kusomea ujinga?
walienda kusomea kubet mkuu
 
This is not a good sign to the economy of the country. It is very true that Companies should adhere on the required Country polices, but at the same time the Government must put in place a conducive ways to the businesses in order to operate successfully and be able to pay taxes to meet the Government budget. No business no Taxes, this is the simple logic.
Hayo unayosema ndio yanafanyika Botswana,Ghana, North of sahara countries

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukweli ni kwamba wameshafunga na wafanyakazi wao sasa wanapumzika nyumbani. DHL alikuwa anapeleka mpaa ndege kwenye migodi ya acacia kuserve courier needs lakini tenda zote hizo kwishney.

Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee!

Nakumbuka ofisi yao pale iwanja wa ndege lile jengo lao lilifunguliwa na aliewahi kua makamo wa rais wa Tanzania, Ghalib Bilal mwaka 2014 hivi au 2013.

Biashara ya ujanja ujanja hapa Bongo ni shida kwa sasa. Mukulu hataki tena huo ujinga.
 
Back
Top Bottom