Makampuni Makubwa Yatikisika

Makampuni Makubwa Yatikisika

Mabadiriko ya kisiasa na kiuchumi huambatana na athari chanya na hasi.Maboresho ya sera,sheria,usimamiaji sheria,utekelezaji maazimio na usimamiaji.Athari chanya na hasi haziepukiki pindi mapinduzi ya taratibu za kimaisha zinapobinuliwa kwa maslahi tofauti kitaifa na kiuongozi.

Taasisi na makampuni mengi za kibiashara {uwekezaji} zimeyumba hata kupelekea kufunga biashara,kupunguza wafanyakazi,kusimamisha biashara,kuuza hisa na kutafuta wabia mbadala.lakini pia zipo kampuni ambazo zimewekwa chini ya uangalizi wa taasisi za fedha na nyingine kuwa katika mchakato wa kufirisiwa.

Mfano wa taasisi na makampuni tajwa ni Airtel {Redundancy},TBL{Redundancy},Home Shopping {Change Name},GSM Malls {Punguza Wafanyakazi},GSM Media {Imefungwa},Living Room {Kupunguza wafanyakazi},Subway-Diamond Plaza {Fungwa},IPP,SSB,Cocacola,Bravo {redundancy},BMTL {redundancy},Freightworld {redundancy},MTL,DSM Collidor,Quality Group,Abla Properties {...},Spencon {winding up},Acacia {Makinikia},Twiga Bancorp {Supervisory},Gapco {Sold to Total} n.k..

Kama taifa yatupasa kuhakiki faida na hasara za muda mrefu za mabadiriko,marekebisho,maboresho na ufinyangaji wa michakato,sera,usimamizi,utekelezaji wake.Ninayo imani yamkini ipo nia thabiti kabisa ya kila linalofanywa sasa kwa faida za kizazi kilichopo na kijacho hivyo basi tathmini ifanyike ili kulinda biashara halali zilizopo pamoja uwekezaji wa mabilioni na wenye athari mtambuka {ajira,kodi,n.k}.
Wamwekwa watu wa paper work kwahiyo wanafanya utafiti km Taifa ndiyo maana tunashauri ''Teachers would like to treat every body like their student'' Utashauri wee wanapotezea tu
 
Kuna mambo matano ya msingi ambayo Serikali yetu hii naamini inayajua lakini inajifanya haiyajuai.

1. Market base yetu (kama ilivyo kwa nchi nyingi za Afrika ukitoa Kenya, South Africa, Nigeria na North Africa) ni very weak ambayo halitoi incentive kubwa kwa wawekezaji wakubwa kuvumilia " political-based policy shocks" kama hizi. Bado nchi inategemea sana wafanyakazi wa serikali kama "middle class". Ukiangalia kinachofanywa kwa hao watumishi wa umma definitely, lazima athari zake zitaonekana katika soko.

2. Sekta Binafsi yetu ni changa na very weak na kwa kiasi kikubwa imepata msukumo kidogo kutokana na uwekezaji wa makampuni mengi ya nje ikiwa pamoja na Kenya na hao wazungu tunaowaona wezi au wapiga dili.

3. Kwa muda mrefu, nchi za kiafrika zimekuwa zikibuni njia za ziada za kuvutia uwekezaji wa nje ili kuvutia mtaji, kuchochea ushindani na kuvutia teknolojia na utaalam. Haya masuala ya incentives yamebuniwa ili ku-rectify changamoto za uzalishaji na mazingira mabovu ya biashara (Supply side constraints and unfavorable business environment".

4. Biashara, au tuseme uchumi kwa ujumla hautaki "kiongozi imara", vinataka taasisi imara ikiwa pamoja na mazingira yanayoruhusu matumizi ya sheria katika kupata haki. Tukumbuke, tumetumia nguvu kubwa sana kuishawishi jumuiya ya kimataifa kwamba hatutarejea kwenye nationalization au centralized economy.

5. FDI tunayojisifia ambayo tumekuwa tukiongoza katika eneo la Afrika Mashariki limechangiwa na sekta za natural resources ikiwemo madini, gesi, nk.

Kwa kuwa hizi sekta zipo katika hali ya uchanga ukizingatia tuna hiztoria ya nationalization huko nyuma, kufanya maamuzi yasiyozingatia masuala haya bila shaka kuna "gharama" huko mbele ya safari. Serikali ilipaswa itumie diplomasia ya hali ya juu katika kurekebisha pale palipokuwa na makosa badala ya maamuzi yanayotawaliwa na mihemko ya wateule wa Rais.
 
shell= Vituo vya mafuta
Shell ni kampuni kubwa ya mafuta huko America.. ni kama zilivyo PUMA, BP, TOTAL na ORYX

Tumezoe kuita shell na inaeleweka tu.

Hata hivyo, hiyo ni kampuni ya kiholanzi na makao yake makuu yako Netherlands

Shell ni kampuni ya Kingereza / Kiholanzi. Ina makao makuu UK na Incorporated Uholanzi.

Ipo karibia dunia nzima.
 
Ni ishara nzuri kwa wenye makampuni kujua athari za kufanya biashara kwa kutofuata taratibu na sheria zilizowekwa.

Wala hakuna issue ya mfumo wala Sera ni udhaifu wa watendaji wa Serikali iliyopita kuruhusu mambo kufanyika kiholela na makampuni mengi yakajisahau.

Amekuja mwenye nchi Sasa wengi wamechanganyikiwa wakiambiwa wakumbuke sheria zinazoongoza taratibu za hayo makampuni.
 
Mimi nilishawambia kuw utawala wa awamu ya tano umeingia na gia nzuri ya kubana mianya yarushwa.
Wafanya biashara walimudu mfumo uliopo wa kodi kwa sababu waliweza chezea kidogo na mfumo wa digital ulikuwa haujaimarishwa.
Sasa imeingia serikali mpya na kurithi mfumo ambao si rafiki. Kitu cha kufanya ni kupunguza viwango vya kodi ili ilipwe bila shuruti.
Hapo biashara na makampuni yatashamiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha yafunge tu, yametupiga mno.
Kama yangekua yanalipa kihalali yasingeyumba

Sent using Jamii Forums mobile app
Usiwe mjinga Hakuna kampuni ambayo ipo tayari kuzalisha halafu hakuna walaji, ninamaanisha kwamba uchumi umeshuka kwa walaji yaani wananchi hawana pesa. Sasa ukiendelea kuweka wafanyakazi utawalipa nini wakati huo wewe huuzi kile ulichozalisha!!? Hivyo basi hakuna sababu ya kuendelea kuwa na kiwanda wakati huo serikali wanataka kodi yao bila kuangalia athali zinazomkabili huyo tajiri.
 
Hayo makampuni yanayotikisika lazima yatakuwa ya wapiga dili.
Ni kweli, kodi haijaongezeka, sheria Ni zilezile, hizo kampuni zilikuwa za kupiga dili tu, magufuri kaza Uzi tu mpaka kieleweke. Kampuni nyingi Tanzania zilikuwa zinakwepa kodi ndo maana zilishine sana, na nyingi zilifanya kazi na serikali kwa kuiba sana serikalini, kuingiza vitu Vila kulipa kodi, etc. Kwa hiyo hizo siyo kampuni za kufumbia macho, wacha wafilisike, wafunge biashara n.k.
 
Sio ishara nzuri kwa makampuni makubwa kuyumba .....

Lakini tutafakari kwa makini nini kimebadilika Tanzania?.

Kama ni kodi je uko nyuma walikuwa wanalipa kodi?.

Kama ni ndio kwa nini wanayumba?......

Maswali yanabaki kuwa na wao kuna sehemu wamekosea pia......

Maana kila mmoja hapo naona anguko lake ni tofauti na la mwingine......
Afadhali umeonyesha upande mwingine wa shilingi, tatizo watu wanalaumu tu bila kufanya uchambuzi wa kutosha. Katika hayo makampuni kuna mengine yameuzwa na mengine yamebadilisha majina. Pamoja na hali ngumu tunayolalamika ni vizuri kujiuliza hao walionunua makampuni yaliyouzwa na waliobadili majina wanafanya je biashara? Tusiangalie upande mmoja tu, huko ndani ya makampuni usika nako kutakuwa na tatizo ambalo mwandishi wa makala hii alitakiwa afanye kazi ya ziada kuja na mifano ya kina zaidi.
 
Ushabiki at work!!!!!!!! Mengi ya makampuni mlioyataja ni ya wapigaji, na walikuwa hawafanyi biashara ktk ushindani uliosawa. Nyingi ya hizo kampuni ndio nilikuwa mkizinasibisha na Jakaya!!!!!!!!
 
= Mabadiliko
= mabadiliko

Hujuwi namna ya kuwacha nafasi "spacing" unapoandika?

Huwa mna mawazo mazuri lakini mnapoyawasilisha kwa kukosea wapi pakuweka R na wapi pakuweka L ladha yote ya kusoma inaondoka.

Hivi mlienda shule kusomea ujinga?


Hujuwi = Hujui
Kuwacha = Kuacha


faiza, toa boriti jichoni kwako kabla hujatoa kibanzi kwa mwenzio. Inakuaje unatoa kasoro zenye kasoro. pambana na hali yako.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Back
Top Bottom