Makampuni Makubwa Yatikisika

Makampuni Makubwa Yatikisika

Hapo yanabanwa makampuni na wateja wao vile vile. Mfano TBL inaongoza kwa ulipaji kodi, lakini nalo linapunguza wafanyakazi, pengine ni ukweli kuwa ama wateja wao wamepunguziwa uwezo wa kufanya matumizi au kodi zimeongezeka na athari wanazipata wao kama kampuni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nafikiri tunahitaji kuwa na kodi endelevu kutokana na kukua kwa makampuni.
 
Mabadiriko ya kisiasa na kiuchumi huambatana na athari chanya na hasi.Maboresho ya sera,sheria,usimamiaji sheria,utekelezaji maazimio na usimamiaji.Athari chanya na hasi haziepukiki pindi mapinduzi ya taratibu za kimaisha zinapobinuliwa kwa maslahi tofauti kitaifa na kiuongozi.

Taasisi na makampuni mengi za kibiashara {uwekezaji} zimeyumba hata kupelekea kufunga biashara,kupunguza wafanyakazi,kusimamisha biashara,kuuza hisa na kutafuta wabia mbadala.lakini pia zipo kampuni ambazo zimewekwa chini ya uangalizi wa taasisi za fedha na nyingine kuwa katika mchakato wa kufirisiwa.

Mfano wa taasisi na makampuni tajwa ni Airtel {Redundancy},TBL{Redundancy},Home Shopping {Change Name},GSM Malls {Punguza Wafanyakazi},GSM Media {Imefungwa},Living Room {Kupunguza wafanyakazi},Subway-Diamond Plaza {Fungwa},IPP,SSB,Cocacola,Bravo {redundancy},BMTL {redundancy},Freightworld {redundancy},MTL,DSM Collidor,Quality Group,Abla Properties {...},Spencon {winding up},Acacia {Makinikia},Twiga Bancorp {Supervisory},Gapco {Sold to Total} n.k..

Kama taifa yatupasa kuhakiki faida na hasara za muda mrefu za mabadiriko,marekebisho,maboresho na ufinyangaji wa michakato,sera,usimamizi,utekelezaji wake.Ninayo imani yamkini ipo nia thabiti kabisa ya kila linalofanywa sasa kwa faida za kizazi kilichopo na kijacho hivyo basi tathmini ifanyike ili kulinda biashara halali zilizopo pamoja uwekezaji wa mabilioni na wenye athari mtambuka {ajira,kodi,n.k}.

Huwezi kujenga ghorofa kwenye mchanga ukategemea litasimama upepo ukipita.
 
Sio ishara nzuri kwa makampuni makubwa kuyumba .....

Lakini tutafakari kwa makini nini kimebadilika Tanzania?.

Kama ni kodi je uko nyuma walikuwa wanalipa kodi?.

Kama ni ndio kwa nini wanayumba?......

Maswali yanabaki kuwa na wao kuna sehemu wamekosea pia......

Maana kila mmoja hapo naona anguko lake ni tofauti na la mwingine......
Sasa hivi unajadili kwa akili timamu. Hongera sana dogo
 
= Mabadiliko
= mabadiliko

Hujuwi namna ya kuwacha nafasi "spacing" unapoandika?

Huwa mna mawazo mazuri lakini mnapoyawasilisha kwa kukosea wapi pakuweka R na wapi pakuweka L ladha yote ya kusoma inaondoka.

Hivi mlienda shule kusomea ujinga?
Sidhani kama ni ujinga bali ni nguvu ya lafudhi tawala ya lugha ya mtu. Umekwishaongea na Mganda akutamkie "Executive?" Utadhani alisahau Kiingereza ama Mshona wa Zimbabwe akutamkie "Arrow root?" Mganda atatamka "cu" katika executive kama "chu" na Mshona ataweka "rrrrrrrhhh" nzito sana katika 'r' zote kiasi utashindwa kujua kwa hakika anasema neno gani hilo. Utasikia kama vile anasema "arrrrrrrhhhoooh rrrrrrruuuut!" Ama Mwitaliano umemsikia wewe!! Mchina je! Wahindi ndugu zangu wa South India Je.Acha bwanaa! Jaribu kumsikiliza yule mtangazaji wa mpira wa soka kule Brazil wakicheza kile kiingereza chake.Utakipenda. Kireno chao ndiyo basi hadi watu wa Angola na Msumbiji wanasema kile sio Kireno. Mwaka fulani tulitoka Sao Pauo tukatua Johannesburg nikiwa njiani kurudi Dar. Mwanadada mmoja wa South African Air akatoa tangazo kwa Kireno kwa abiria kama kawaida likirudiwa kwa Kiingereza. Alipomaliza abiria mmoja akasema hiki ndicho Kireno sio kile tulichokisikia Sao Paulo na Porto Alegre, Brazil. Tulicheka saanaaa. Kwa hiyo lugha usimcheke mtu. Hasa ikiwa ana lugha nyingine tawala anayozungumza.
 
Ni ishara nzuri kwa wenye makampuni kujua athari za kufanya biashara kwa kutofuata taratibu na sheria zilizowekwa.

Wala hakuna issue ya mfumo wala Sera ni udhaifu wa watendaji wa Serikali iliyopita kuruhusu mambo kufanyika kiholela na makampuni mengi yakajisahau.

Amekuja mwenye nchi Sasa wengi wamechanganyikiwa wakiambiwa wakumbuke sheria zinazoongoza taratibu za hayo makampuni.

Serikali iliyopita ilikua ya chama gani?na uyo mwenye nchi anatokea chama gani pia? Kwanza hapo
 
Sababu kubwa si dili au kutokulipa kodi, hata makampuni yaliyokuwa hayapigi dili na walipaji kodi nao wanayumba. Jambo muhimu ni purchasing power. Kama bidhaa hazinunuliki kwa wateja kukosa pesa hakuna biashara itakayosonga.
Nani kaichukua purchasing power?
Mishahara imepunguzwa?
 
= Mabadiliko
= mabadiliko

Hujuwi namna ya kuwacha nafasi "spacing" unapoandika?

Huwa mna mawazo mazuri lakini mnapoyawasilisha kwa kukosea wapi pakuweka R na wapi pakuweka L ladha yote ya kusoma inaondoka.

Hivi mlienda shule kusomea ujinga?
Kama kawaida yako hizo typing error lakini si umeelewa ujumbe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali iliyopita ilikua ya chama gani?na uyo mwenye nchi anatokea chama gani pia? Kwanza hapo
Kwa hiyo kinachokuuma ni CCM kubadilika?
Mbona CHADEMA kimebadilika na kuwa chama cha kutetea UFISADI hujauliza?
 
Hilo kundi linamsubiri 2020 limshughulikie vilivyo,na atakiona cha mtema kumi

Yapo makundi mengi ukiachilia mbali hilo
2020 kazi anayo kwani amegusa wengi nao wanamsubiri wamsulubishe
 
Mabadiriko ya kisiasa na kiuchumi huambatana na athari chanya na hasi.Maboresho ya sera,sheria,usimamiaji sheria,utekelezaji maazimio na usimamiaji.Athari chanya na hasi haziepukiki pindi mapinduzi ya taratibu za kimaisha zinapobinuliwa kwa maslahi tofauti kitaifa na kiuongozi.

Taasisi na makampuni mengi za kibiashara {uwekezaji} zimeyumba hata kupelekea kufunga biashara,kupunguza wafanyakazi,kusimamisha biashara,kuuza hisa na kutafuta wabia mbadala.lakini pia zipo kampuni ambazo zimewekwa chini ya uangalizi wa taasisi za fedha na nyingine kuwa katika mchakato wa kufirisiwa.

Mfano wa taasisi na makampuni tajwa ni Airtel {Redundancy},TBL{Redundancy},Home Shopping {Change Name},GSM Malls {Punguza Wafanyakazi},GSM Media {Imefungwa},Living Room {Kupunguza wafanyakazi},Subway-Diamond Plaza {Fungwa},IPP,SSB,Cocacola,Bravo {redundancy},BMTL {redundancy},Freightworld {redundancy},MTL,DSM Collidor,Quality Group,Abla Properties {...},Spencon {winding up},Acacia {Makinikia},Twiga Bancorp {Supervisory},Gapco {Sold to Total} n.k..

Kama taifa yatupasa kuhakiki faida na hasara za muda mrefu za mabadiriko,marekebisho,maboresho na ufinyangaji wa michakato,sera,usimamizi,utekelezaji wake.Ninayo imani yamkini ipo nia thabiti kabisa ya kila linalofanywa sasa kwa faida za kizazi kilichopo na kijacho hivyo basi tathmini ifanyike ili kulinda biashara halali zilizopo pamoja uwekezaji wa mabilioni na wenye athari mtambuka {ajira,kodi,n.k}.

Mabadiriko = mabadiliko
Kufirisiwa = kufilisiwa
 
Sio ishara nzuri kwa makampuni makubwa kuyumba .....

Lakini tutafakari kwa makini nini kimebadilika Tanzania?.

Kama ni kodi je uko nyuma walikuwa wanalipa kodi?.

Kama ni ndio kwa nini wanayumba?......

Maswali yanabaki kuwa na wao kuna sehemu wamekosea pia......

Maana kila mmoja hapo naona anguko lake ni tofauti na la mwingine......
Tuseme haya makampuni yalikuwa hayalipi kodi . Lakini yalitoa ajira , walioajiriwa walilipa kodi , waliweza kumudu gharama za maisha ya kila siku, waliweza kusomesha watoto na ndugu na kuwasaidia wazee wao kwa mishahara waliyopata kutokana na hayo makampuni yasiyolipa kodi, walipokuwa wakienda kazini walikodi tax, au boda boda, au bajaji au walipanda daladala au walitumia magari Yao binafsi. Ina maana hawa waajiriwa walioongeza mzunguko wa pesa na kutoa ajira kutokana na matumizi Yao.

Lakini je Hiyo kodi iliyokuwa inakusanywa miaka ya nyuma au sasa hivi inatumika vile ambavyo sisi walipa kodi tunataka?

Kuyumba kwa kampuni moja kunaathiri kampuni nyengine mmoja kwa Moja kwa kuwa mzunguko wa fedha unakuwa umepungua.
Hela zetu nyingi zinatumika katika matumizi ya anasa ma vx, posho n.k.

Siungi mkono kampuni kutokulipa kodi Lakini ni bora isilipe kodi kuliko kufungwa . Athari ni kubwa .
 
= Mabadiliko
= mabadiliko

Hujuwi namna ya kuwacha nafasi "spacing" unapoandika?

Huwa mna mawazo mazuri lakini mnapoyawasilisha kwa kukosea wapi pakuweka R na wapi pakuweka L ladha yote ya kusoma inaondoka.

Hivi mlienda shule kusomea ujinga?
Hujuwi = hujui
 
Back
Top Bottom