Ndio baadhi ya watu wanavyoamini, eti kiongozi bora, huwa hana msimamo unaoeleweka. Yaani hatabiriki! Hii falsafa wengi wanaojaribu kuiiga inawashinda, kwani wanachanganya, kutotabirika na kukosa mwelekeo. Viongozi waovu ndo huwa hawana mwelekeo na mara nyingi hawatabiriki. Kama umesoma vizuri historia ya jinsi hitler alivyoingia madarakani, kutotabirika kwake ndo ilikuwa silaha yake kuu. Hata alipoingia madarakani, alijaribu kujionesha kuwa kiongozi bora huku chini chini akiendelea na kampeni zake za kuangamiza watu. Umesema ukweli mtupu.kikwete ni kigeugeu na hiloo linatosha kuiondoa ccm madarakani.
Msimamo wa Kikwete katika masuala mengi ya kitaifa umekuwa ni wa kutatanisha kwani usafi wake unatiliwa shaka. Kwa hiyo hata suala ambalo linaonekana wazi ni chafu; huwezi kujua Kikwete yuko upande gani! Ndo maana watendaji wake mara nyingi wamekuwa wakijikuta katika mapambano ya wao kwa wao bila kujua ni yupi hasa yuko upande wa Bwana mkubwa. Kifupi ana sifa zote za viongozi waliokuja kuwa viongozi wa hatari kabisa duniani.
Kutoeleweka kwake badala ya kusaidia, kumekuwa ndo mwiba mkubwa kwa serikali yake. Kwa mfano wakati wa sakata la Richmond ilikuwa vigumu kujua alikuwa kwa kina mwakyembe au kwa kina Lowassa. Lakini njia ya muongo ni fupi. Kutotabirika kwa kuigiza huwa muda si mrefu kunagundulika - kwani baada ya Lowassa kulazimika kujiuzulu Kikwete alionekana ku-shake sana (hata kama alifurahi kiasi fulani Lowassa kuondoka, hakupenda alivyoondoka ukizingatia bado ni mshirika wake wa karibu mno na alikuwa akipenda misimamo yake). Ukweli ni kuwa kutoeleweka kwake kulitishia kuisambaratisha serikali yake kipindi kile. Na hadi leo, kutoeleweka kwake kunaiweka sana CCM matatani.
Kuondoka kwa Makamba CCM kunaweza kurudisha imani kwa chama kwa baadhi ya wanachama, lakini tatizo la CCM si Makamba. Tatizo la CCM ni Mwenyekiti wake. Hivyo kuondoka kwa Makamba kunaweza kuonekana suluhisho kwa muda mfupi, lakini songombingo na minyukano ya ndani haitaisha, kwani mwenyekiti Kinyonga (jicho moja linatazama mbele lingine nyuma) bado yupo pale pale na maguvu yote ya Dola yeye ndo bado anayadhibiti.
CCM isipoondoka madarakani na utawala wa Kikwete itakuwa imepona!