Makala ya kijamii na kisheria: Idris aliharibuje ushahidi?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,845
Unaweza ukawa na akili lakini usiwe na maarifa.. Makinika... Kumbuka maandishi hayafutiki... Hata unapofuta ama kuhariri maudhui yako hapa JF.. Original version hubaki huko kwenye sever

Tendo la kwanza ndio huwa halisi.. Baada ya hapo uhariri wowote mbele ya sheria huitwa bandia... Yaani sio halisi... Hata ukipiga picha umeshika msokoto mmoja wa bangi na kuirusha mtandaoni... Lakini baadae ukahariri na kuweka sigara ili kuficha uhalisia.. Hilo ni kosa la jinai kisheria na unapaswa kushitakiwa kwa kuharibu ushahidi (tumia neno kuhariri)

Idd baada ya kufanya lile kosa alililoshtakiwa nalo.. Nadhani kuna watu walimshika MASIKIO yake makubwa kwamba afute haraka la sivyo anajiweka matatani... Kwa mwendokasi wa super sonic (sio ya COVID-19) aidha alifuta kabisa ama alihariri maudhui husika ili asalimike kuingia matatani.

Haikufua dafu... Awali ni awali tuu... hakuna awali mbovu... Awali ndio halisi.. Kafuta/kahariri lakini macho kuona yalikuwa yameshachota kila kitu... Alikolalia yeye wenzake ndio wameakia.

Hii kesi ya Idd hata kama ina mapungufu kisheria na kijamii lakini ina funzo kubwa la kutufunza sote hasa linapokuja swala la ushahidi na vidhibiti... Unaweza kuandika na kufuta... Lakini kumbuka umefuta ama umehariri kwenye kifaa CHAKO lakini sio kwenye sever... Siku wakikuhitaji watakupata tuu

Jr
 
Kabisa mkuu hili jambo la kufuta vity kwa vifaa vyetu wengi tumekariri na wengi wetu ndo tuna amini hivyo. Uhalisia mawasiliano yetu yote kuna sehemu inatumika kama backup inayitunza taarifa zote.
 
Ok hilo linaweza kuwa swali zuri ila hawajasema kufuta ushahidi kwa suala gani. Wengi mmekuja na fikra kuwa inahusiana na clip ile.

Mimi swali langu ni hili. Hivi Rais hana wanasheria binafsi wa kumfungulia kesi na kumtetea mahakamani kwa mambo yake binafsi? Nakumbuka Rudy Giuliani alikuwa au labda bado ni mwanasheria BINAFSI wa Donald Trump na hadi kuna wakati kuna kesi binafsi za Trump alikuwa anahusika nazo, mfano zile za wale wanawake waliokuwa wanajitokeza wakati ule.

Sasa imekuwaje hii issue ya kucheka, ambayo haina uhusiano wowote na usalama wa Rais bali ni personal feelings za mtu, watumishi wa serikali ndiyo wanahusika kumshitaki Idd? Hauoni kuwa kuna ufujaji wa kodi zetu? Labda hata uhujumu uchumi?

Imagine Trump angetumia federal prosecutors kumtetea kwa kesi zile, Marekani ingewaka moto!
 
Ok hilo linaweza kuwa swali zuri ila hawajasema kufuta ushahidi kwa suala gani. Wengi mmekuja na fikra kuwa inahusiana na clip ile.

Mimi swali langu ni hili. Hivi Rais hana wanasheria binafsi wa kumfungulia kesi na kumtetea mahakamani kwa mambo yake binafsi? Nakumbuka Rudy Giuliani alikuwa au labda bado ni mwanasheria BINAFSI wa Donald Trump na hadi kuna wakati kuna kesi binafsi za Trump alikuwa anahusika nazo, mfano zile za wale wanawake waliokuwa wanajitokeza wakati ule...
Rais ni taasisi kwahiyo kila jambo linashughulikiwa kitaasisi na hata linapotokea jambo binafsi bado litashughulikiwa kitaasisi kwakuwa rais sio mdoli (robot).

Case ya trump ni tofauti kwakuwa nje ya urais pia ni mfanyabiashara

Jr
 
Kosa lingine hili hapa.. Tujifunze nyakati zimebadilika

UPDATES
Mchekeshaji Idris amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu pamoja na mwenzake Innocent Maiga na kusomewa mashtaka yao

Katika shtaka la kwaza, Idris pekee anatuhumiwa kutumia laini yenye namba 0753 617621 ambayo haijasajiliwa kwa jina lake bali kwa jina la Innocent Maiga

Katika shtaka la pili, Innocent pekee anatuhumiwa kushindwa kuripoti ubadili wa umiliki wa laini hiyo baada ya Idris kuanza kuitumia

Jr
 
Rais ni taasisi kwahiyo kila jambo linashughulikiwa kitaasisi na hata linapotokea jambo binafsi bado litashughulikiwa kitaasisi kwakuwa rais sio mdoli (robot)
Case ya trump ni tofauti kwakuwa nje ya urais pia ni mfanyabiashara

Jr

Hapana sidhani kama ni kweli hilo ulilosema. Nitaendelea kufanya utafiti na kuwauliza magwiji wa sheria halafu nitakueletea mrejesho.

Kwa sasa ninachoweza kusema ni kuwa haileti picha nzuri kabisa kwa Rais (wa nchi yoyote ile) kumshitaki raia wake wa kawaida kwa mambo binafsi kama kukashfiwa na ndiyo maana ni nadra sana kusikia kesi za namna hiyo.

Kwa kiasi kikubwa huwa wanalazimika kumezea labda ziwe ni serious allegations, hapo ndiyo utasikia mwanasheria BINAFSI wa Rais amejitokeza.

Lakini kutumia state prosecutors kwa suala binafsi la mtu (yoyote yule, ikiwemo Rais) ni kinyume cha sheria. Na kwa uelewa wangu, suala binafsi la Rais ni jambo lolote lililo nje ya usalama wake.

Lakini kama nilivyosema, nitafuatilia zaidi.
 
Unaweza ukawa na akili lakini usiwe na maarifa.. Makinika... Kumbuka maandishi hayafutiki... Hata unapofuta ama kuhariri maudhui yako hapa JF.. Original version hubaki huko kwenye sever
Tendo la kwanza ndio huwa halisi...
Waamishie nguvu kwa kigogo kwa sasa uyo idd aadhibiwe tu hamna namna.
 
Hapana sidhani kama ni kweli hilo ulilosema. Nitaendelea kufanya utafiti na kuwauliza magwiji wa sheria halafu nitakueletea mrejesho.

Kwa sasa ninachoweza kusema ni kuwa haileti picha nzuri kabisa kwa Rais (wa nchi yoyote ile) kumshitaki raia wake wa kawaida kwa mambo binafsi kama kukashfiwa na ndiyo maana ni nadra sana kusikia kesi za namna hiyo...
Kwa siasa na madaraka ya kiutawala Afrika.. Rais ni kila kitu... Hakuna tofauti kati ya binafsi na taasisi..

Jr
 
IDD mwenyewe, Ajitambui... mzee mataga naye ajitambui... sasa Mimi ntampiga mzee mataga kibao kama wananitundilissu wanitundulissu tu
 
Kitu digital footprints inabidi watu wafahamu ni ngumu kuifuta hivyo kuwa makini unacho tupia ktk internet pia unacho search vyote hubaki au kuhifadhiwa na uwezo wa kufuta au kuhariri ni kama kujidanyana tu.
 
Ok hilo linaweza kuwa swali zuri ila hawajasema kufuta ushahidi kwa suala gani. Wengi mmekuja na fikra kuwa inahusiana na clip ile.

Mimi swali langu ni hili. Hivi Rais hana wanasheria binafsi wa kumfungulia kesi na kumtetea mahakamani kwa mambo yake binafsi? Nakumbuka Rudy Giuliani alikuwa au labda bado ni mwanasheria BINAFSI wa Donald Trump na hadi kuna wakati kuna kesi binafsi za Trump alikuwa anahusika nazo, mfano zile za wale wanawake waliokuwa wanajitokeza wakati ule...
Ishu ya raisi alaf unaiita binafsi..kwahyo wewe ukifumaniwa ni ishu yako haiihusu familia yako?
 
Hapo nahisi wanataka kunshitaki kwa kosa moja moja Hadi atoe adabu..ikiisha hiyo watamfungulia ingine
 
Kitu digital footprints inabidi watu wafahamu ni ngumu kuifuta hivyo kuwa makini unacho tupia ktk internet pia unacho search vyote hubaki au kuhifadhiwa na uwezo wa kufuta au kuhariri ni kama kujidanyana tu.

Hivi ukitumia incognito tab labda kwenye chrome, hivi huwa inasaidia katika kutokuweka kumbukumbu ya taarifa zako online kweli!
 
Rais ni taasisi kwahiyo kila jambo linashughulikiwa kitaasisi na hata linapotokea jambo binafsi bado litashughulikiwa kitaasisi kwakuwa rais sio mdoli (robot)
Case ya trump ni tofauti kwakuwa nje ya urais pia ni mfanyabiashara

Jr
Ameshtakiwa kwa kutumia line isiyo yake, hili la kufuta ushahidi sijaliona pale.
 
Back
Top Bottom