kunguni wa ulaya
JF-Expert Member
- Mar 16, 2014
- 4,132
- 6,100
Washawajua wa TZ ni waoga na maboya.
Serikali yaweza kumfanya chochote na raia wasiriact.
Serikali yaweza kumfanya chochote na raia wasiriact.
Amsamehe kwa lipi?boraJPM akaingilia kati kumsamehe kama alivyoweza kuwasamehe wengne
Anza ku react wewe usiwaite wenzako maboya huku umejificha kwenye sketi ya dada yako!Washawajua wa TZ ni waoga na maboya.
Serikali yaweza kumfanya chochote na raia wasiriact.
😂Hizo zako ni husuda na kijicho.... Waswahel wanasema hasidi hana sababu...
Jr
Hana dhamana aliyoruka.Atakuwa kasoma kitabu cha Yerico Nyerere, UJASUSI WA KIDOLA, Bora arudi maana mahakama inamtaka kwa kuruka dhamana, ajibu shitaka lake.
Hata akili zenyewe wanazo basi au ni vichwa vitupu ?Mkuu sikutishi ila hao watu huwa wanaachaga akili nyumbani
Utaniona mbele kabisa nimevaa buti la njenje!Yaani kama kuwekwa ndani niwekwe tu lakini airport nitakuwepo kwa mapokezi. Halafu yule mkuu wa wapiga debe Makondakta si kawa kibajaji sasa hivi?
Ndukiiiii
hatutaki kutoa kiki kwa jpm wakoAkidhurika tena au akiwekwa tena mahabusu serikali itakuwa imejichafua sana. Hata kama vyombo vya ulinzi na usalama vitamkamata ni bora JPM akaingilia kati kumsamehe kama alivyoweza kuwasamehe wengne.
Nami nmeshafika airport! Potelea mbali kwani nimezaliwa kuishi milele, potelea Chato!Asiye na mwana aeleke jiwe. Tuna kwenda kumpokea shujaa
🤣Mwanakuli find..utapata unchokitafuta...
Jr
💪🏾Nami nmeshafika airport! Potelea mbali kwani nimezaliwa kuishi milele, potelea Chato!
Amsamehe kwa kosa lipi?Akidhurika tena au akiwekwa tena mahabusu serikali itakuwa imejichafua sana. Hata kama vyombo vya ulinzi na usalama vitamkamata ni bora JPM akaingilia kati kumsamehe kama alivyoweza kuwasamehe wengne.
Dunia nzima macho Dar es saalam.Weledi na utendaji kazi wa jeshi la polisi unaangaliwa kwa karibu mno siku hii ya leo ya kurejea kwa TAL.
wadanganye wenzako tu, yule ana kesi au unajifanya hujui?? kuhusu wadhamini wake nalo hulijui hilo?? akili haziishi usione ubahili kuzitumiaYamebakia masaa machache Tundu Antipasi Lissu, mwanachama kiongozi na mtia nia ya kugombea urais kwa tiketi ya CHADEMA atue nchini akitokea nchi ya Ubelgiji alipokuwa kwa ajili ya matibabu ya muda mrefu.
Ujio wake si wa kawaida kwakuwa inasemwa kuwa wale waliomsababishia madhila ya yote yaliyotokea mpaka sasa hawajakamatwa na hawajajulilana ni akina nani zaidi ya kuwepo tuhuma ambazo ziko pending.
Ujio huu una maandalizi mengi ya wazi na ya siri. Kuna intelijensia zinafanya kazi kubwa sana kwenye huu ujio na ziko intelijensia tatu muhimu; kila moja inajitahidi kucheza karata zake kwa umakini mkubwa. Intelijensia itakayokosea kidogo tu imekula kwake mazima.
1. Intelijensia ya chama chake
Je, imejiandaaje na ujio wake? Usalama wake? Baada ya kuwasili nchini? Na baada ya hapo? Habari za kuwa atawekwa ndani na bila dhamana hadi uchaguzi upite kutokana na kesi kadhaa zinazomsubiri za huko nyuma kabla hajaondoka nchini.
2. Intelijensia ya kwake mwenyewe
Je, amejiaandaje kwa lolote litakalomtokea? Ni wazi haji kiboya ndio maana anajiamini sana. Pengine escort anayokuja nayo ina options nyingi tayari na imeshajiandaa kwa lolote, kuanzia kukamatwa hadi kuwekwa kizuizini; kama ni kweli hili lipo, hapo kuna jumuiya ya kimataifa itahusishwa pakubwa.
3. Intelijensia ya mamlaka za nchi
Je, itafanya nini kwenye huu ujio? Ni kweli wamejiandaa kumkamata? Je, wameshapima athari zake juu ya hili? Na je, itakuwaje kama watapuuza na kumpa ulinzi wote toka airport mpaka kwake na baada ya hapo?
Kati ya intelijensia zote tatu hii ya mamlaka za nchi ndio inaangaliwa kwa karibu mno kwakuwa chochote itakachokifanya kitaonwa na kusikika kimataifa. Hapa ndio panahitajika kuwa na washauri wenye weledi mkubwa na hekima ya kuamua mambo ya kitaifa
Nu vema intelijensia hii ikazishauri mamlaka ziruhusu mapokezi bila fujo na bila kutunishiana misuli, watakuwa wamefanya jambo moja kubwa sana.
Kwenye jamii kuna kundi moja kubwa sana linapenda matukio na amsha amsha, hiyo ndio hobby yao
Likisikia Miss Tanzania anarudi, utalikuta airport
Likisikia SIMBA imeshinda michuano ya kimataifa, litaenda airport
Likisikia tukio lolote kubwa lazima liwepo kushuhudia
Ni nani anakumbuka ile misafara ya Mwalimu Myerere aliporudishwa nchini, msafara wa Lipumba ariporudi nchini Toma kwenye timu ya kurekebisha uchumi wa dunia, msafara wa kumpokea Ruge nk.
Hili kundi lime-miss hayo mambo. Si kila atakayeenda pale airport ni mwana CHADEMA ni kuwaacha wajipe raha wapunguze fukuto za changamoto za maisha ndani yao, a polisi wawepo kuhakikisha ulinzi na usalama wa TAL, waliokuja kumpokea, wasiohusika na mapokezi na mali za watu wote.
Weledi na utendaji kazi wa jeshi la polisi unaangaliwa kwa karibu mno siku hii ya leo ya kurejea kwa TAL.
Jr