Majina ya uswahilini vs Masaki & Oysterbay

umekosa cha kuandika wewe ndugu!
aya bwana tushajua umeishi msasani na mikocheni miaka mingi
alafu hii post ni ya fb sio jf kwa great thinkers!

FB na JF tofauti yake hasa ni ipi? Kwangu mimi zote ni social networks.

Inategemea unaowasiliana nao ni watu wa namna gani.JF pia kuna watu wenye mambo ya kitoto
kama ambavyo FB nako kuna watu wanawasiliana kwa mambo ya maana
ikiwemo mitandao ya kibiashara na kuelimishana.
 
FB na JF tofauti yake hasa ni ipi? Kwangu mimi zote ni social networks.

Inategemea unaowasiliana nao ni watu wa namna gani.JF pia kuna watu wenye mambo ya kitoto
kama ambavyo FB nako kuna watu wanawasiliana kwa mambo ya maana
ikiwemo mitandao ya kibiashara na kuelimishana.
unauhakika? unacho kinena mdada

 
Miongoni mwa ustaarabu wa mtu ni jina analompa mwanawe. Ukisikia jina la mtoto fulani unaweza kujua baba au mama yake au aliyempatia jina yu mwenye fikra gani. Waswahili wana tabia ya kuita majina kulingana na kipindi na mazingira aliyozaliwa mtoto. Kwa mfano, Jumapili, Jumanne. Majina mengine ya uswahilini, Sikitu, siwajui, sikudhani, siwajali, sikutegemea, sikutaraji, chausiku na cha ajabu mengi kati ya majina haya ni ya kike sijui kuna mfungamano gani kwa kweli. Yamkini baadhi ya majina hayo yakawa yanaashiria masaibu aliyopata mama wa mtoto huyo, au kukaaa muda mrefu bila kupata mtoto halafu akaja kushika mimba, hivyo akaamua kumweita mtoto wake sikudhani. Any way, kila amwitae mtoto wake jina fulani huwa na sababu zake nadhani wakiulizwa wazazi wenyewe wenye watoto wenye majina hayo wanaweza kuwa na majibu mazuri. Kuna wale mashabiki kama wa akina gaddafi, saddam, scud, hitler na majina mengine au Nejad (Rais wa Iran), au majina ya wachezaji mashuhuri na kadhalika. Hivyo kila mtu huwa na msukumo na sababu zake katika kumpa jina mwanae. La msingi unapochagua jina la mwanao hakikisha ni jina zuri na ambalo limezoeleka katika jamii anayoishimkwani kinyume na hivyo huenda akagezwa kichwa cha utani na masikhara.
 
Nimeishi Mikocheni na Msasani kwa miaka mingi, lakini sikubahatika kumsikia msichana akiitwa Chausiku au Havijawa. Sana sana niliwajua kina Karen, jacquline, Linah, nk. Kwanini kuwepo tofauti kubwa ya majina kwa wasichana wa uswahili na kwenye mageti makali?:phone:


Mbona mwanaasha yupo magogoni anapigwa upepo mwanana wa baharini?
 
Lakini huwa najiuliza hivi mzazi anafikiria nini kumpa mwanaye majina ya nuksi nuksi tu kama Tabu,matatizo,chuki,jalala,mashaka,mkiwa,huzuni mbona kuna majina ya kiswahili mazuri tu kama majaliwa,hekima,busara,upendo n.k hivi mtoto huyu akija kuwa na maisha ya ajabu akikulaumu atakuwa anakosea kweli?
 
yani navuta picha jf ingejaa thread zinazousu resources!!
Na inawezekana ata wewe unajiita great thinker!!

Sijiiti great thinker, pili sidhani kama umesoma coment yangu mpaka mwisho, na la tatu inawezekana JF pakawa na specific thngs to discus like science and technology, resource in our country and how to utilize them! Tatizo ukikaa sana facebook akili yako inakua so taken on discusing cheap issues like people bt wengine wamezoea kujadili ideas sio izi kitu!
 
Ila sasa hivi hata uwahilini kuna wakina Ciara,Ciello,Preta nk Na hata kutofautisha mtoto wa Masaki na Mbagala ngumu sana sa hivi wachina wametoa ile tofauti ya mwenye nacho na siye nacho.
 
Miongoni mwa ustaarabu wa mtu ni jina analompa mwanawe. Ukisikia jina la mtoto fulani unaweza kujua baba au mama yake au aliyempatia jina yu mwenye fikra gani. Waswahili wana tabia ya kuita majina kulingana na kipindi na mazingira aliyozaliwa mtoto. Kwa mfano, Jumapili, Jumanne. Majina mengine ya uswahilini, Sikitu, siwajui, sikudhani, siwajali, sikutegemea, sikutaraji, chausiku na cha ajabu mengi kati ya majina haya ni ya kike sijui kuna mfungamano gani kwa kweli. Yamkini baadhi ya majina hayo yakawa yanaashiria masaibu aliyopata mama wa mtoto huyo, au kukaaa muda mrefu bila kupata mtoto halafu akaja kushika mimba, hivyo akaamua kumweita mtoto wake sikudhani. Any way, kila amwitae mtoto wake jina fulani huwa na sababu zake nadhani wakiulizwa wazazi wenyewe wenye watoto wenye majina hayo wanaweza kuwa na majibu mazuri. Kuna wale mashabiki kama wa akina gaddafi, saddam, scud, hitler na majina mengine au Nejad (Rais wa Iran), au majina ya wachezaji mashuhuri na kadhalika. Hivyo kila mtu huwa na msukumo na sababu zake katika kumpa jina mwanae. La msingi unapochagua jina la mwanao hakikisha ni jina zuri na ambalo limezoeleka katika jamii anayoishimkwani kinyume na hivyo huenda akagezwa kichwa cha utani na masikhara.
 
jina lina nafasi kubwa sana na maana sana kwa m2 yyt,huo ndo ukweli.
Yanabeba maana mpaka kwny maisha yetu.(mfano,'ulimboka-means Mungu niponye')....ss mpe jina mtt,majuto,na atajuta kweli maisha yake yote
 
Mbona uswahilini pia kuna majina kama flora, agness, jacqline, Karen, Linah, happy?

Kweli huku kwetu uswazi wapo hao ila yanavyotamkwa mhh! Mfano flora-fulola, karen-kaleni, jakilini nk. Ila wakina Havintishi, Semeni wapo nao.
 
Majina kama pamela ruby heaven rarely sana kuyapata uswahilini.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mbona Mwanaasha anakaa Ikulu? It doesn't get better than that now does it?
 
Kweli huku kwetu uswazi wapo hao ila yanavyotamkwa mhh! Mfano flora-fulola, karen-kaleni, jakilini nk. Ila wakina Havintishi, Semeni wapo nao.

Ha ha ha mkuu umetisha, Petrol-Petulo dah
 
Mzungu akiitwa Green, Hammer, Limehouse, Cabin, Crabtree, Second etc. it's not a big deal na is ok.
Mswahili akiitwa Nyundo, Ndimu, Pili, Tatu, inakuwa issue. Tukumbuke hayo majina ya akina Karen sijui Jacqueline tuliletewa na sio yetu. Ni lini tutaachana na mental slavery??????
 
Mbona Mwanaasha anakaa Ikulu? It doesn't get better than that now does it?

Heheheee No Lie Kaka! Hapo Ikulu tu kwa' Kiranja Mkuu' kuna MWANAASHA(jina commonly used huku Kwetu USWAZI), sasa ndio wajiulize kati ya hao wa Masaki na yule wa IKULU nani wa-Kishua!
 
Nimeishi Mikocheni na Msasani kwa miaka mingi, lakini sikubahatika kumsikia msichana akiitwa Chausiku au Havijawa. Sana sana niliwajua kina Karen, jacquline, Linah, nk. Kwanini kuwepo tofauti kubwa ya majina kwa wasichana wa uswahili na kwenye mageti makali?:phone:

mmm viroba jogoo@ its network!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom