Majina saba ya askari walio uwawa Sudan

Majina saba ya askari walio uwawa Sudan

attachment.php


Vifo hivi viwakumbushe wanajeshi wetu kwamba watanzania wote ni ndugu na kwamba sote ni mavumbi na mavumbini ni lazima tutarudi. Mateso wanayoyafanya wanajeshi kwa raia wa Mtwara ni ya kinyama!!! Si ya kiutu hata kidogo!!! Ni bahati mbaya kwamba jeshi letu linatumiwa vibaya na wanasiasa!!! Mungu aturehemu sote na roho za wanajeshi hawa zipumzike kwa amani!!

......du! RIP our soldiers....inauma....wameondoka wazima...sasa wanarudi kwenye body bugs....Ifike sasa mahali serikali ya TZ wawe wanafikiria nje ya box....isije ikawa waasi wa uganda wame overlap na kuwafata kuwatandika askari wetu wa kibongo kule Darfur...ikiwa kama response ya waasi(wa uganda)dhidi ya statements za JK kuwataka waongee na serikali zao...I can bet we have lot of enemies around us......na sisi wenyewe wala hatupendani ndani ya nchi yetu.....can't imagine kukitokea vita leo TZ.....sidhani kama uzalendo uliopo TZ sasa ni sawa na ule uliokuwepo tulipochapana na waganda.......
 


hapana na hatuna majeshi somalia




hapana unakosea ukisema hivo.. je unajua wakimbizi wakiingia tanzania gharama zitaongezeka, ujambazi utaongezeka sababu silaha ndogondogo zitapenya... TANZANIA ITASAIDIA PALE ITAKAPOONA INAWEZA

Nimeandika haraka natumia simu hope umenielewa


Appologies kwa kuandika Somalia baada ya Sudan.

Kwa hiyo una maana tumepeleka wanajeshi wetu huko Sudan kwa ajili ya "kuzuia wakimbizi wasiingie Tanzania"....
 
kuna universal set na sub set mkuu.

Afrika ni universal set, Tanzania ni subset. ukiifia Afrika au UN kwa vyovyote vile unakuwa umeifia Tanzania. twende sawa mkuu.

Mkuu hebu rudisha akili, kama angekuwa ni ndugu yako amekuachia mzigo wa kulea yatima kwa sababu ya kulinda amani ya UN halafu jiulize UN ni nini kwako personally.
 
Hayo maneno uliyoandika hapo chini ni upumbavu na kukosa akili kuliko pitiliza.
Rest in peace askari wetu. Mmekufa kishujaa

Si vema kumsahihisha mtu kwa kumtukana, hata kama kafanya kosa gani. Hapo -------- na mkosa akili ni wewe usiyependa kusikiliza maoni ya wengine. Ni kweli huko Mtwara wanajeshi walioshika nafasi ya polisi walioshindwa kuwalinda wananchi wanaendelea kufanya vitendo viovu juu wananchi haohao waliokabidhiwa dhamana ya kuwalinda. Si unajua tena hapa TZ tuna Policcm, ana Jeshiccm? Tuvumiliane na tusitukanane ndani ya jamvi hili.

Wapumzike kwa amani vijana wetu.
 
Wacha wafe tu, haya ndio matokeo ya kimbelembele....
 
Wapumzike kwa amani
Ni pigo kubwa sana na tunaungana na familia za marehemu kwa kuwapa pole nyingi kwa msiba huu
 
attachment.php


Vifo hivi viwakumbushe wanajeshi wetu kwamba watanzania wote ni ndugu na kwamba sote ni mavumbi na mavumbini ni lazima tutarudi. Mateso wanayoyafanya wanajeshi kwa raia wa Mtwara ni ya kinyama!!! Si ya kiutu hata kidogo!!! Ni bahati mbaya kwamba jeshi letu linatumiwa vibaya na wanasiasa!!! Mungu aturehemu sote na roho za wanajeshi hawa zipumzike kwa amani!!

hizi ni laana za wana MTWARA..
 
Ni wanajeshi wa umoja wa mataifa waliotokea Tanzania?

Ni askari wa Tanzania waliokuwa kwenye kikosi cha kulinda amani huko Darful Sudan. Wamekufa kwa kushambuliwa na vikosi vya Janjaweed.
 
Mkuu hebu rudisha akili, kama angekuwa ni ndugu yako amekuachia mzigo wa kulea yatima kwa sababu ya kulinda amani ya UN halafu jiulize UN ni nini kwako personally.

Kamanda we dizaini mbishi eeh?
 
Poleni wafiwa na Watanzania wenzangu kwa vifo hivi.


Majina ya askari saba wa Tanzania waliokufa kwenye shambulio la ghafla mjini Darfur yamepatikana.


2.png

Askari hao waliokufa ambao walikuwa kwenye vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa huko nchini Sudan ni :-
1. Sajenti Shaibu Othuman,
2. Koplo Oswald Chaula,
3. Koplo Mohamed Juma,
4. Koplo Mohamed Chikilizo,
5. Pte. Rodney Ndunguru,
6. Pte. Peter Werema,
7. Pte. Fortunatus Msofe.



Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kwenye mtandao ni kwamba askari hao walikwenda kujaribu kumwokoa mwenzao (ambaye hakutajwa) ambaye alisemekana kutekwa na vikosi vya waasi nchini humo.

Wakati wakijiandaa, ghafla walizingirwa na askari hao waasi na kisha kushambuliwa kwa risasi hadi kufa.

Haikufahamika hali ya askari huyo ambaye alidaiwa kutekwa kama bado yu hai ama ni miongoni mwa waliokufa.

Mungu azilaze roho za askari wetu mahali pema peponi, Amina.
 
Ata kama kazi tunatoa kwa dili na safari za huko waliko pia ni kwa dili,basi na mafunzo ya msingi pia yawepo kwa wote ata wasioenda na mafunzo ya ziada yapewe hata kwa wasiotaka kuwapa vyeo, sio kila kitu dili dili mpaka roho za watu dili.
Mungu bariki JW,
Mungu bariki TZ,
Wapumzike kwa amani mashujaa hao!
 
Hivi mkuu wameifia Tanzania ama Sudan?Naomba kueleweshwa kwenye hili.Kuuliza si ujinga mkuu wangu.

Marekani walikwenda Iraq, Afghanistan na kwingineko kwa vile walikuwa na maslahi yao katika nchi hizo. Tanzania ina maslahi gani huko Sudan? Inasikitisha kuona wanatengenezwa wajane na watoto yatima katika nchi ya ugeni. Bahati mbaya mno hata familia za hawa ndugu zetu huenda zisisaidiwe kwa lolote lile, future ya maisha ya hawa waliosalia iko mashakani, watoto hawana baba wa kuwasomesha na kuwapatia mahitaji mengine, mama hawana waume wa kuwahudumia. Mimi nasema hawajaifia Tanzania, wamekufa kwa sababu isiyojulikana (niko tayari kukosolewa).
 
Kamanda we dizaini mbishi eeh?

Sio ubishi, ndio ukweli huo. Tatizo hatutaki kuambiwa ukweli na kuufanyia kazi. Fikiria nchi zilizopata uhuru kupitia TZ, halafu tathmini walipofikia. Kuna maslahi gani huko ya Tanzania kama Tanzania ?
 
Kulikuwa na umuhimu gani wa sisi kuwapeleka vijana wetu huko?
 
kwanza kuna msiba hapa tuwape POLE wanafamilia na wanajeshi wenzao.Hili la UISLAMU na Ukristo au Upagani wa wanajeshi ni akili ndogo kuwaza hivyo sasa. SAINT IVUGA Kwa nini uanzishe mjadala huo sasa?WEWE AKILI YAKO NA MIKONO YA KUANDIKA HAVIWASILIANI?

Kumbe ni Saint Ivuga, mpuuze Mkuu.
 
Ni habari iliyonisikitisha sana...........maombi yangu ni kwa wanafamilia na wapendwa wote ambao msiba huu umewagusa kwa karibu sana kwamba Mungu awape faraja yake na awafanyie wepesi katika kipindi hiki kigumu wanachopitia.
 
attachment.php


vifo hivi viwakumbushe wanajeshi wetu kwamba watanzania wote ni ndugu na kwamba sote ni mavumbi na mavumbini ni lazima tutarudi. Mateso wanayoyafanya wanajeshi kwa raia wa mtwara ni ya kinyama!!! Si ya kiutu hata kidogo!!! Ni bahati mbaya kwamba jeshi letu linatumiwa vibaya na wanasiasa!!! Mungu aturehemu sote na roho za wanajeshi hawa zipumzike kwa amani!!

umenena mkuu,big up sana!limesahau kuwa ni jeshi wananchi?
 
sio ubishi, ndio ukweli huo. Tatizo hatutaki kuambiwa ukweli na kuufanyia kazi. Fikiria nchi zilizopata uhuru kupitia tz, halafu tathmini walipofikia. Kuna maslahi gani huko ya tanzania kama tanzania ?

hakuna masilahi makubwa kama kulinda utu wa wanadamu wenzako.
 
Back
Top Bottom