1. Kama utakua haukuwa shuleni, unaweza kulinganisha kampuni ya sigara , kampuni ya bia kabla na bada ya ubinafsishaji , waulize waliokuwa wanakunywa na kuvuta watakuambia.
2. Kuhusu TTCL ametaja hapo thana ya collective responsibility-issue ya tufanye au tusifanya ilishapitishwa na PSRC, Maana ya haigusi yeye mojakwa moja lakini hapaswi kutojibu kwa niaba ya serekali -hapo unapata sifa yake ya team work na sio individual empire and glory-ndio maana kwa ufupi tu zitto kaamua kuwa mpole .jibu lipo makini sana
Msulibasi,
Wewe inaonekana aidha ni fisadi au ni shabiki wa Prof. Mwandosya.
Yaonekana hata unachokiongea hukijui. Nionyeshe shirika linalopata faida baada ya ubinafisishaji chini ya utawala wa Mkapa na huyu Waziri wake kihiyo anayejiita Profesa.
Hivi wewe ni mgeni katika nji hii? Hizi habari za TTCL, ATC,TRL,NBC n.k huzijui? Haya ni mashirika yaliyokuwa yanatengeneza FAIDA na fedha za mashirika haya zilikuwa zikitumika vibaya kwa kuchotwa bila mpango na haohao Vigogo wa Serikali ya Chama Cha Mafisadi kwa ajili ya matanuzi na vikao vya chama huko Chimwaga na Dar. Kama hujui uliza mwanakwetu tukujuze. Kuna watu bado wameweka vimemo vya vigogo wa Serikali na CCM wakiomba fedha kwa ajili ya Kampeni za chaguzi mbalimbali. Vipo na zinaweza kutolewa kama ushahidi!!!
Hata kama unazungumzia swala la Collective responsibility bado huyu jamaa yako Mwandosya alikuwa kwene ngazi ya Waziri ambaye anatakiwa kumshauri Rais inavyopaswa kuhusu Ubinafsishaji kama ulikuwa na tija kwa Taifa au la! Labda nikujuze tu ya kwamba MSI/DETECON hawakuja na mtaji wowote wa kuanzisha Celtel leo hii inaitwa Bharti Airtel. Hivi vitu tunavifahamu na tuna ushahidi ambao unaweza kutolewa wakti wowote na mahali popote kwenye Mahakama yoyote.
Jambo la kwanza unatakiwa ufahamu kwamba Celtel alilipa jumla ya Dola 64.5milioni tu kununua 35% ya hisa ndani ya TTCL na 65% zilizobaki zilikuwa zinamilikiwa na Serikali kinadharia tu kwani Serikali haikuwa na sauti yoyote ndani ya TTCL pamoja na kumiliki hisa kubwa! Kwa kutumia mbinu za kifisadi Serikali ya CCM (Prof.Mwandosya na Rais Mkapa)ilitoa maelekezo HAZINA kwamba HAZINA iwape Celtel zile dola 64.5m ili wawekeze kwenye miundombinu ya TTCL kwa nia ya kuiendeleza! Kwa maana ningine ni kwamba Celtel kama Celtel hawakuja na MTAJI wowote wa kuwekeza ndani ya TTCL baada ya kuuziwa/kupewa kwa bei ya kutupa!!Kwa hiyo MSI/DETECON walikuja na Briefcase tu na pum**u zao.
Katika mkataba wa Ubinafsishaji wa TTCL hawa jamaa walikuwa wamepewa masharti ya kutimiza/kutekeleza ikiwemo kuongeza idadi ya simu za kawaida(mezani/fixed) toka 300,000 kufikia 804,000 ndani ya miaka 4 lakini pia kujenga mtandao wa simu za mkononi kupitia Celtel. Baada ya hawa matapeli kuingia TTCL walichofanya ni kinyume cha mkataba kwa kukomba hela yote kwenye akaunti za TTCL na kuzihamishia ughaibuni na kidogo kuwekeza kwenye Celtel.
Walitumia Raslimali watu ya TTCL pamoja na Mtaji wa TTCL ikiwemo fedha waliyorudishiwa kutoka hazina kwa kiasi. Watanzania wazalendo tunajua walianza na Celtel Tanzania huku wakisema ni Kampuni tanzu ya TTCL lakini baada ya kuona wanatengeneza faida kubwa kwa kutumia Raslimali watu ya TTCL na mtaji wa TTCL na fedha kiasi toka Hazina wakabadilisha jina na kujjita Celtel International na kutangaza rasmi kuwa Celtel International haina tena uhusiano wowote na TTCL!!
Baadaye walibadilisha tena jina na kujiita ZAIN(Zaina) katika mipango mikakati ya kukwepa KODI wakisaidiwa na SERA za kifisadi za CCM za TAX HOLIDAY EVERY AFTER 5 YEARS kwa makampuni ya kigeni yanayowekeza Tanzania si kwenye sekta ya Mawasiliano tu lakini hata kwenye MIGODI YA MADINI yetu policy hii ya kifisadi ya CCM bado inaendelea na ndiyo maana nchi hii inaendelea kuwa maskini ya kutupwa na Watanzania wakiendelea kuogelea kwenye lindi la umaskini! Kwa watu wenye akili timamu wanajua ni kwanini uchumi wa nchi unakuwa kwenye makaratsi tu lakini kiuhalisia na -ve growth. Tunajua mpaka sasa deni la Taifa limefikia Trilioni 38 na thamani ya Shilingi inazidi kuporoka kwa sababu ya SERA ZA KIFISADI ZA CCM.
Labda kwa sasa nimalize kwa kusema kwamba mpaka MSI/DETECON anaondoka baada ya mkataba kwisha hakukuwa na mabadiliko yoyote ndani ya TTCL. Masharti yote 2 waliyopewa ya kuongeza wateja wa simu za kawaida toka 300,000 walishindwa kwani mpaka wanaondoka TTCL ilikuwa na wateja chini ya 200,000!!!Na hili la kujenga mtandao wa simu za mkononi halikuwepo tena kwani tayari Celtel International haikuwa Kampuni tanzu ya TTCL! Kuna jambo moja la kuchekesha kama siyo la kusikitisha ambalo hawa jamaa walilifanya ndani ya TTCL. Walianzisha mtandao wa Simu za mkononi ndani ya TTCL unaoitwa CDMA wakidai ni teknolojia mpya na ya kisasa. Mtandao huo wa kibabaishaji umeendelea kuitesa TTCL mpaka leo kwani Watanzania walishindwa kuupokea maana Makampuni yote wanatumia mtandao wa GSM. Mpaka leo huwa najiuliza ilikuwaje TTCL na Serikali mwenye hisa 65% wakakubali ulaghai huu wa kutumia CDMA wakti wenzao wote wanatumia GSM?
Haya ni ya TTCL tu bado sijagusa ya TRL, ATC, NBC na kadhalika. Labda kabla sijazzungumzia hayo nikukumbushe tu mheshimiwa sana kama utakuwa na kumbukumbu sahihi kuhusu alichosema Baba wa Taifa hili Mwl.J.K.Nyerere kuhusu Ubinafsishaji baada ya kuona Mkapa na Mafisadi wenzake wameigeuza Ikulu kuwa Pango la Wezi na Wanyang'anyi. Alisema hivi. Kama serikali inataka kubinasisha Mashirika basi ifanye hivo kwa yale yaliyokuwa yanajiendesha kwa hasara si kila shirika. Hawa jamaa Mkapa na kina Mwandosya waliweka pamba masikioni waakendelea kubinafsisha mpaka Benki ya NBC iliyokuwa inatengeneza faida kwa bei ya kutupa yaani Tsh. Bilioni 15 tu. Hapa ndipo Mwalimu alivyowatelea uvivu na kumwambia Mkapa na Serikali yake kwamba kwa kasi na mtindo wa ubinafsishaji waliokuwa wanaenda nao BASI WANGEBINAFISISHA MPAKA MAGEREZA!!!!!!!!
Shirika la Ndege Tanzania liko wapi? Ni aibu Tanzania kutokuwa na shrika la ndege huku ikipitwa na vinchi vidogo kama RWANDA,BURUNDI, UGANDA,KENYA, ETHIOPIA n.k. tena vinchi ambavyo havina Raslimali nyingi kama Tanzania. Hivi hii kama siyo laana tuseme ni kitu gani hasa???
Iko wapi TRC(Shirika la Reli Tanzania) lililokuwa maarufu enzi za Mwalimu, iko wapi TAZARA jamani???Mafisadi wa Serikali ya CCM wameamua kuua RELI zote ili waweze kufanya biashara ya kubeba MIZIGO na ABIRIA kwa kutumia maroli yao(Semi-trailer) na Ma-bus ya YOU-TONG made in China!! Upo hapo mwanakwetu????
Nitaendelea tena baada ya kufanya loading.......