Speaker
JF-Expert Member
- Aug 12, 2010
- 6,324
- 2,238
Kachimbe kisima wewe mwenyewe ndugu yangu na unywe maji yako peke yako.
Usishiriki na mwingine,Ni hatari kubwa sana.
Hakika,maji ya kisima cha watu wengi yameingiliwa na mdudu,
ukiwa na kiu usiyaonje,Utaambukizwa.
Siku hizi kiu ya maji imeongezeka sana,watu wanayanjwa maji kila wakati,...
mengine yanauzwa kila kona ya barabara,..mengine hutolewa bure.
Nani atapona?
Kwa sababu maji yameingiliwa na mdudu,yanapatikana kiurahisi sana.
Ukipita kote utayaona,usiyanywe.
Yapo yaliyowekwa kwenye chupa kubwa na ndogo,wengi wanakimbilia yaliyo
kwenye chupa ndogo wakidhani ndio salama,wana jidanganya....
Hayo ndio machafu kupindukia.
Tafadhalini sana wapendwa,chimba kisima chako mwenyewe.
Chota maji vile utakavyo,chemsha mara kwa mara na usiyanywe na mtu mwingine
nawe utakuwa salama.
Kuweni na weekend njema.
Usishiriki na mwingine,Ni hatari kubwa sana.
Hakika,maji ya kisima cha watu wengi yameingiliwa na mdudu,
ukiwa na kiu usiyaonje,Utaambukizwa.
Siku hizi kiu ya maji imeongezeka sana,watu wanayanjwa maji kila wakati,...
mengine yanauzwa kila kona ya barabara,..mengine hutolewa bure.
Nani atapona?
Kwa sababu maji yameingiliwa na mdudu,yanapatikana kiurahisi sana.
Ukipita kote utayaona,usiyanywe.
Yapo yaliyowekwa kwenye chupa kubwa na ndogo,wengi wanakimbilia yaliyo
kwenye chupa ndogo wakidhani ndio salama,wana jidanganya....
Hayo ndio machafu kupindukia.
Tafadhalini sana wapendwa,chimba kisima chako mwenyewe.
Chota maji vile utakavyo,chemsha mara kwa mara na usiyanywe na mtu mwingine
nawe utakuwa salama.
Kuweni na weekend njema.