Maji marefu wewe ni msomi uliyebobea mpaka kufikia hadhi ya kuwa profesa, wanafunzi wako wa chuo kikuu wakiona hii habari hawataipenda kabisa.
Majimarefu Asema Picha Imetengenezwa
Amemaliza maongezi na wakili maarufu jijini kuiburuza CHADEMA na MWANANCHI Mahakamani Jumatatu kwa kumchafulia jina na heshima yake ndani ya chama na jamii kwa ujumla
"Picha hii nilipigwa nikiwa na huyu mbunge mwenzangu, Vicent Nyerere (kulia), lakini huyu wa kushoto (Joshua Nassari) hakuwepo karibu yangu kabisa! Yeye alikuwa mbali akiamrisha vijana wanichome moto tena akiwa na hasira, tofauti na anavyocheka katika picha hii. Huu ni mchezo mchafu wa kuunganisha picha kwenye kompyuta uliofanywa na CHADEMA na kwa makusudi gazeti hili likaichapisha, baada ya kuona kwamba hatua aliyofanya Nassari ya kutaka niuawe jana ni mbaya sana. Nitalishitaki gazeti hili". Analalamika Mbunge wa Korogwe Vijijini Stephen Ngonyani wakati akionyesha picha inayomuonyesha akiwa katika furaha ya hali ya juu yeye, Nyerere na Nassari. Picha hiyo imechapishwa jana ukurasa wa kwanza gazeti la Mwananchi.Vilevile ukurasa wa kwanza gazeti la Tanzania Daima.
amesoma pale muhas enzi zile ipo chini ya udsm ikiitwa muchs. pale pana kitengo cha traditional medicines. Sasa sikumbuki kama alibaki pale kufunza mpaka akafika level ya uprofesa au alipomaliza alienda chuo kingine
Lazima 2015 tutampleka moshi mjini akamngoe kibabu NdesamburoHuyu mbunge ni janga la kitaifa sijui alipataje ubunge
Sipati picha maji marefu kwenda mahakamani hata hao waliomshauri hata kkama ni mawakili toka mbinguni lazima wangekubaliana nae afungue kesi kwa wanachotaka wao ni hela. Maji marefu ajitambue kuwa yeye ni mteja tu kama wateja wengine mbele za mawakili kwa hiyo hakuna kitu hapo.