Maiti bado zinaokotwa ndani ya viroba, tutubu dhambi ya kumsingizia Hayati JPM la sivyo itaendelea kututafuna

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,608
Watanzania tunapenda sana kutengeneza habari za uongo. Ni kipaji fulani kisichofaa kuwa sifa ya mtu lakini ndio ukweli kwamba tunacho na tunapenda kukiendeleza.

Uvumi unaweza kusambaa haraka sana mpaka mhusika anapokuja kukanusha tayari habari zinakuwa zimeshambaa kila kona na uongo wa kutungwa unakuwa ndio ukweli. Labda ni ukosefu wa kazi unaotusumbua siku zote!.

Labda ni ukosefu wa elimu unaotunyima fursa ya kutafakari jambo kwa kina na kuona kama kinachosemwa ni cha kweli au ni cha uzushi, au labda ni robo mbaya tu inayochanganyika na wivu inayotusumbua.

Hapa Mbezi Beach yapo majengo mawili yenye kufanana, moja limeshamalizika na linatumiwa kama ukumbi wa shughuli za harusi linaitwa SEA BREEZE HILL na lingine bado linajengwa halijamaliziwa. Ukiwa unatoka mjini kuelekea daraja la apson utayaona yapo kushoto kwako na kulia utaona maghorofa ya BOT. Kwa muda mrefu tu inavumishwa kwamba ni mali ya Ridhiwani Kikwete wakati ukweli ni tofauti kabisa na huo uvumi.

Yanamilikiwa na Mzee fulani mwenye hoteli yake mitaa ya Kariakoo karibu na kituo cha mabasi ya mwendo kasi, lakini uvumi uliovumishwa na watu wengi wakidhania ni ukweli ni kuwa yale maghorofa ni mali ya Ridhiwani mtoto wa JK, Hivyo wanaojenga hoja kuwa familia ya JK ina mali nyingi wanakuwa wamehesabu pia na hayo maghorofa!!.

Ni kama ambavyo zile maiti zilizokuwa zikiokotwa pale Coco Beach zilivyohusishwa na awamu ya JPM, watu wengi maskini ya Mungu wakajua ni hivyo!, kwamba JPM anawashughulikia wote wanaokwenda kinyume na matakwa yake.

Lakini awamu ya sita ikiwa inafikia nusu ya safari bado kuna miili ya watu inaokotwa ndani ya viroba sehemu mbalimbali za Tanzania, je hizi ni maiti zenye uhusiano na awamu ya tano?.

Unyama ni sifa ya binadamu, tuna roho mbaya sana siku zote. Hatufahami juu ya unyama wetu kwani vyombo vya habari havifiki kila sehemu na kuripoti matukio. Lakini kila siku kuna watu wanachinjwa, wanadhalilishwa na kuwekwa ndani ya viroba ni sifa mbaya ya binadamu.

Tulitenda dhambi ya kumsingizia JPM kuwa ni mtu mwenye kuondoa uhai wa watu, lakini mpaka kesho bado matukio yale yale ya awamu yake yanaendelea kutokea hapa nchini. Tuitubu hii dhambi vinginevyo itatuumiza sana huko tuendako.
 
Watanzania tunapenda sana kutengeneza habari za uongo. Ni kipaji fulani kisichofaa kuwa sifa ya mtu lakini ndio ukweli kwamba tunacho na tunapenda kukiendeleza.

Uvumi unaweza kusambaa haraka sana mpaka mhusika anapokuja kukanusha tayari habari zinakuwa zimeshambaa kila kona na uongo wa kutungwa unakuwa ndio ukweli. Labda ni ukosefu wa kazi unaotusumbua siku zote!.

Labda ni ukosefu wa elimu unaotunyima fursa ya kutafakari jambo kwa kina na kuona kama kinachosemwa ni cha kweli au ni cha uzushi, au labda ni robo mbaya tu inayochanganyika na wivu inayotusumbua.

Hapa Mbezi Beach yapo majengo mawili yenye kufanana, moja limeshamalizika na linatumiwa kama ukumbi wa shughuli za harusi linaitwa SEA BREEZE HILL na lingine bado linajengwa halijamaliziwa. Ukiwa unatoka mjini kuelekea daraja la apson utayaona yapo kushoto kwako na kulia utaona maghorofa ya BOT. Kwa muda mrefu tu inavumishwa kwamba ni mali ya Ridhiwani Kikwete wakati ukweli ni tofauti kabisa na huo uvumi.

Yanamilikiwa na Mzee fulani mwenye hoteli yake mitaa ya Kariakoo karibu na kituo cha mabasi ya mwendo kasi, lakini uvumi uliovumishwa na watu wengi wakidhania ni ukweli ni kuwa yale maghorofa ni mali ya Ridhiwani mtoto wa JK, Hivyo wanaojenga hoja kuwa familia ya JK ina mali nyingi wanakuwa wamehesabu pia na hayo maghorofa!!.

Ni kama ambavyo zile maiti zilizokuwa zikiokotwa pale Coco Beach zilivyohusishwa na awamu ya JPM, watu wengi maskini ya Mungu wakajua ni hivyo!, kwamba JPM anawashughulikia wote wanaokwenda kinyume na matakwa yake.

Lakini awamu ya sita ikiwa inafikia nusu ya safari bado kuna miili ya watu inaokotwa ndani ya viroba sehemu mbalimbali za Tanzania, je hizi ni maiti zenye uhusiano na awamu ya tano?.

Unyama ni sifa ya binadamu, tuna roho mbaya sana siku zote. Hatufahami juu ya unyama wetu kwani vyombo vya habari havifiki kila sehemu na kuripoti matukio. Lakini kila siku kuna watu wanachinjwa, wanadhalilishwa na kuwekwa ndani ya viroba ni sifa mbaya ya binadamu.

Tulitenda dhambi ya kumsingizia JPM kuwa ni mtu mwenye kuondoa uhai wa watu, lakini mpaka kesho bado matukio yale yale ya awamu yake yanaendelea kutokea hapa nchini. Tuitubu hii dhambi vinginevyo itatuumiza sana huko tuendako.
Kabla ya kusema kuwa alisingiziwa.....

Rudi nyuma kwa Baba wa Taifa hili na waliokuja baada yake,ni nani ambae ndani ya tawala yake,hapajatokea mauaji ya namna hii.......?!

Kisha
Itazame Dunia...ni Nchi gani ambayo hakuna mauaji kabisa........
Tufahamu Chief
Amani ni ghali sana kuliko tunavyofahamu,kuna mengi yanatokea nyuma ya pazia,sisi kama Raia,hatujui......
Muhimu
Kutunza amani ya nchi kwa ujumla na kumuomba sana Mola muumba juu ya hili

Shukran
Barikiwa sana
 
Tumia akili alisema hivi!

Pale St Peters kuna baadhi wanaolinda maslahi ya wakubwa na wanataka ku delay upatikanaji wa kitabu kipya!

Anaongeza watakaushwa kimya kimya!!nadhani ni mwenedelezo ule!!

"Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA"!
Hiyo katiba mpya itaondoa hao wanaokaushwa mmoja mmoja?. Nadhani tuachane na huu uvivu wa kufikiri tupanue ubongo wetu.
 
Kikwete, mkapa, mwinyi,wote kwenye tawala zao nao waliua. Tatizo la DIKTETA MAGUFULI alitekeleza mauaji Kwa UKATILI wa kutisha. Alitengeneza Genge lake la hatari kuliko hatari yenyewe.
 
Hauliwi zuzu
#Shika Hilo..... Ajenda na maslahi ya watu Fulani yalindwe even kwa nguvu ya chama
 
Tumuulize Membe kulikoni tena? maana alituhakikishia kwamba hakuna tena kuokota maiti kwenye viroba.
 
Hiyo katiba mpya itaondoa hao wanaokaushwa mmoja mmoja?. Nadhani tuachane na huu uvivu wa kufikiri tupanue ubongo wetu.
NDIO

Kuakushwa kimya kimya ni matokeo mabovu ya katiba iliyopo!!

Jpm aliitumia katiba vibaya kufanya yake ndio ikazaa viroba Ili akosane na wananchi na wakafanikiwa chuki ikazidi yakatokea hayo ambayo Ndio historia !

Na Sasa kuna vita vya kimya kimya Kati ya wanaotaka katiba mpya na wanapsaka vyeo KWA katiba iloyopo!Lazima kukaushana kutakuwepo Kati ya pande mbili Hadi katiba itakapopatikana!!

"Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA"
 
Kikwete, mkapa, mwinyi,wote kwenye tawala zao nao waliua. Tatizo la DIKTETA MAGUFULI alitekeleza mauaji Kwa UKATILI wa kutisha. Alitengeneza Genge lake la hatari kuliko hatari yenyewe.
Kikwete na Mkapa wao walikuwa wanafanya mauwaji ya aina gani ambayo hayakuwa ya kutisha au ndio yale ya mfano wa Ulimboka au yapi?
 
Back
Top Bottom