Maisha yamenishinda!!

Maisha yamenishinda!!

Maharage bei ya 1kg leo ni sh 2000!hii awamu ya 4 ni CHUMA ULETE!
 
Kaka ni mshahara mkubwa sana, bana matumizi naona kama shida yako kubwa ni gari sio muhimu sana.
Hutakiwi kujiona kama unamatatizo kuna watu wanafamilia kubwa kuliko yako na kipato chao ni cha chini zaidi.
Unajiona unashida kwa sababu hujui shida za wenzako
 
kaka kusema ukwel maisha ni mgumu mno mana kila kukicha mambo yanazid kuwa mabaya cjui 2fanyeje mana kila pesa unayoshka hv sasa haina chenji cjui 2ish vp na ukichek kusoma 2mesoma lakn joto ya jiwe 2naiona mungu wangu cjui 2nakwenda wap kaka co wewe 2uu hch ni kilio cha weng walio kuwa na magar walikwepa kulipa kod au wameiba mahal au ya mikopo
 
Kwa kipato cha shs 542,000 hutakiwi kulalamika. Kuna watanzania kama 85% ambao wanapata 1/4 ya unachopata (135,000) na wanaishi na familia zao watoto wa3 and above na bado utakuta ana kibanda chake Charambe, Kongowe, Kitunda au Kipate.

Wewe una mke na mtoto mmoja na unatumia daladala unalalamika nini. Nakushauri kuwa na vipaumbele, acha makundi ya starehe kama ulevi. uzinzi then hicho kipato kinaweza kukutoa. Hebu tufanye mchanganuo hapa chini.

Tshs 542,000/=

1. Kodi ya nyumba shs 100,000
2. Chakula nyumbani shs 150,000
3. Chakula kazini shs 60,000
4. Nauli ya dala dala 30,000
5. Mengineyo shs 100,000

Jumla ya matumizi ni shs 440,000 hivyo unabaki na akiba ya 102,000. Ukitunza hii akiba kwa miezi sita unaweza ukampatie mke wake mtaji wa shs 612,000 baada ya miezi sita na mkaanza mkakati wa kununu ka plot Gongolamboto.

Chukua huo ushauri na usirudi kijijini utajuta.
Kweli hapa siongezi neno!
96.9% akaufanyie kazi huo ushauri kwanza.
 
Mwenzangu endelea kufight huko huko town. Usijaribu kuja huku kijjn. Hata sie tuliopo kjjn tunabana matumizi tupate nauli tuje tubanane huko huko (whether mbagala or gongo...) kjjn noma! Njoo baada ya mwezi hata kanda mbili huvai tena.. utanambia!
 
Posted by BLUE BALAA
Kwa kipato cha shs 542,000 hutakiwi kulalamika. Kuna watanzania kama 85% ambao wanapata 1/4 ya unachopata (135,000) na wanaishi na familia zao watoto wa3 and above na bado utakuta ana kibanda chake Charambe, Kongowe, Kitunda au Kipate.

Wewe una mke na mtoto mmoja na unatumia daladala unalalamika nini. Nakushauri kuwa na vipaumbele, acha makundi ya starehe kama ulevi. uzinzi then hicho kipato kinaweza kukutoa. Hebu tufanye mchanganuo hapa chini.

Tshs 542,000/=

1. Kodi ya nyumba shs 100,000
2. Chakula nyumbani shs 150,000
3. Chakula kazini shs 60,000
4. Nauli ya dala dala 30,000
5. Mengineyo shs 100,000

Jumla ya matumizi ni shs 440,000 hivyo unabaki na akiba ya 102,000. Ukitunza hii akiba kwa miezi sita unaweza ukampatie mke wake mtaji wa shs 612,000 baada ya miezi sita na mkaanza mkakati wa kununu ka plot Gongolamboto.

Chukua huo ushauri na usirudi kijijini utajuta.

Kaka pole sana

Naunga bajeti hii 75% mkono.lkn family zetu ni kubwa,let say kuna mdogo/ndugu yako unatakiwa kumsomesha,wazazi wako wanakuangalia na mbaya zaidi ni kwamba wanajua kuwa ww uko mjini unafanya kazi na unapokea mshahara mwisho wa mwezi.Mm naona anahitaki kufanya kitu cha ziada ili kukimu mahitaji.
 
U
Wakuu Maisha ya Mjini yamenishinda, yaani nikiangalia kipato changu na majukumu niliyonayo naona siwezi kabisa.

Maisha kama haya naona afadhali yale maisha niliishi kwa wazazi wangu enzi za mwalimu pamoja na kuwa babangu alikuwa mkulima lakini tulienda shule na tuliishi maisha mazuri.

Mimi sijui wenzangu mnaishije? mnapata haya machungu nayoyaona mimi? nasimama asubuhi kituoni kwenda kazini naona magari yanapita tu huku mmefunga vioo hivi kweli mna matatizo kama yangu kweli? Hivi nyie pesa mnazipata wapi? mbona najiona mpweke katika nchi yangu hii?

Wakuu siyo siri natafakari kama mambo yakizidi kuwa magumu basi nitafute nauli nirudi kwetu angalau huko nitakuwa na uhakika wa kusogeza siku.

Kipato changu wakuu ni Tshs 542,000/- Nina Mke na mtoto mmoja (5), nimepanga nyumba viwili na sebure - Mambo yamegoma kabisa.

Nipeni ushauri nateketea mtanzania mwenzenu.
Ukifika wasalimie babu na bibi,waambie umeona maghorofa yanatembea baharini(meli),wazungu magari na ukuta unatoa pesa(ATM)!!
 
Mshahara wako upo juu zaidi hata ya ule TUCTA inataka serikali ilipe watumishi wake, mapendekezo ya TUCTA ni 350,000/=

Ushauri ni kama ulivyoambiwa hapa bana matumizi,mke apate shughuli ya kufanya,na pia potelea mbali itavyokuwa kataa kabisa kuchangia hizi harusi etc ni mfirisi mkubwa mijini siku hizi
 
Pole sana, jaribuni kubana matumizi sana, mwambie wife asione aibu ajaribu kutengeneza hata karanga, aisikrimu au maandazi aweke hapo dukani kwa mangi ili yeye awe ananunua msosi halafu wewe unadili na matumizi mengine.

Muhimu, baneni matumizi acha kuchangia harusi, birthday nk.

I feel ur pain, wengine hapa tunasomesha wadodo vyuo, bado wazee nyumbani yaani acha tu ndugu yangu tupo wengi wala hauko peke yako.

Kaka hayo maisha tuyabane vipi? mke wangu pia ana kipato chake kama 300,000/- kwa mwezi tukichanganya tunapata 840,000-

Sasa mkuu hebu fuatilia mchanganuo huu.

Matumizi ya Nyumbani kwa siku - 8,000 kila siku.
Nauli zetu na chakula cha mchana tunagawana elfu tano tano - jumla 10,000
Umeme kwa mwezi - 10,000
Bill ya Maji kwa mwezi - 5,000
Pango la Nyumba kwa mwaka Tshs (50,000 kwa mwezi times 12) = 600,000 /-

Sasa nibane matumizi kwa namna gani wakubwa? hapo sijapata mgeni, sijamlipia mwanangu michango ya shuleni, hatujanunua nguo zetu na uniform za mtoto wetu n.k.
 
Njia nyingine ndg yangu ni kuwa kama ungekuwa umeingia SACCOS uka-save kiasi fulani then ifikie wakati uchukue mkopo kwa riba nafuu uanzishe ka-mradi kadogo kenye kuhitaji mtaji kiduchu. Vinginevyo ungeingia kwenye siasa ili wananchi walio wengi ambao ni walalahoi wakupe kura uingie Dodoma maisha yabadilike. Take a chance. G.day
 
Huku kijijini na mimi maisha yananishinda.
Nataka niuze mahindi nije mjini, mjini kuna nyumba nzuri na magari. Nasikia magari madogo ila yanakimbia hayo. Yakikua makubwa ndio yanazidi kukimbia. Nikiyaona nitahamasika kutafuta vyangu.
Huku kijijini tunacheza na ngedere tu.

ha ha ha ha ha ha ha ha aaa mkuu karibu sana mjini! ila akili kumkichwa

Fuso wasikutishe na magari yao mengi ni mikopo, cha muhimu ni kujipanga tu vizuri we na mama watoto wako huo mshahara bado sio mbaya sana
 
Njia nyingine ndg yangu ni kuwa kama ungekuwa umeingia SACCOS uka-save kiasi fulani then ifikie wakati uchukue mkopo kwa riba nafuu uanzishe ka-mradi kadogo kenye kuhitaji mtaji kiduchu. Vinginevyo ungeingia kwenye siasa ili wananchi walio wengi ambao ni walalahoi wakupe kura uingie Dodoma maisha yabadilike. Take a chance. G.day

Ngugu yangu Boney hilo la SACCOS nalijua ila cha kujiuliza huko SACCOS nipeleke nini wakati kipato changu jumla yake kwa kwezi nina negative? ningekuwa nabakiza walau 10,000 kwa mwezi basi ningefanya hivyo ili mwaka ukiisha niwe na 120,000/- ila hiyo elfu kumi kaka niipate wapi katika kipato changu?

.Mfano mwezi wa tatu nalipa kodi ya nyumba 600,000/- hapa nahaha kutafuta hiyo hela kufa na kupona na ndiyo maana nikaona yamenifika shingoni ndiyo nikaamua kuwaandikia haya.
 
Nakushauri ufanye bishara yoyote ile hata kama unapata faida sh.5000 kwa sikuX30 utapata 150,000 zitakupush.

Pia tafuta makazi yanayoendana na kipato chako.

Nunua chakula kulingana na kipato chako na fanya mpangilio wa maisha utayamudu tu.

Kukata tamaa ni dhambi jitahidi kubuni mbinu mpya za maisha utafanikiwa.:hand:
 
Tafuta vyanzo vingine vya pesa.

katavi hii point nataka ufafanuzi zaidi, kwa mafano mke wangu achachike kivipi? mimi mwenyewe nichacharike kivipi? yaani mpaka kufikia hatua ya kuomba ushauri wote wawili tumekaa tumechakachua vimeshindikana na ndiyo maana unaona mwanangu ana 5 years tukaona tusiongeze mwingine kwa sasa hali ni mbaya wakuu - siku hazisogei.
 
Mshahara wako upo juu zaidi hata ya ule TUCTA inataka serikali ilipe watumishi wake, mapendekezo ya TUCTA ni 350,000/=

Ushauri ni kama ulivyoambiwa hapa bana matumizi,mke apate shughuli ya kufanya,na pia potelea mbali itavyokuwa kataa kabisa kuchangia hizi harusi etc ni mfirisi mkubwa mijini siku hizi

Ushari wako mzuri lakini kupata jibu lazima niishi chumba kimoja cha elfu 10,000 kisicho na umeme, mchana wote wawili mimi na mke wangu tusile lunch, jioni tule vyakula kama mihongo, uji na chai siku za weekend tufunge tujifungie ndani ili tusipate wageni.

Tujitenge na familia zetu zote mbili - ili tusave zaidi sababu wao wanajua sisi tupo mjini na tunafanya kazi kwa hiyo maombi ya usaidizi ni mengi tu na wengine wanakuja moja kwa moja kwetu huwezi kuwafukuza.

Kwa haya yote wakuu mi naona niende kijijini tu - nitajua la kufanya huko cha msingi lazima nijipange niondoke na 2m baada ya kuuza baadhi ya vitu vyetu.

Mtoto wangu atasoma huko ila mimi na mama tutajitokea kumfundisha tuition sababu tutakuwa wakulima, tutahakikisha anafauru tu.
 
Kwa kipato cha shs 542,000 hutakiwi kulalamika. Kuna watanzania kama 85% ambao wanapata 1/4 ya unachopata (135,000) na wanaishi na familia zao watoto wa3 and above na bado utakuta ana kibanda chake Charambe, Kongowe, Kitunda au Kipate.

Wewe una mke na mtoto mmoja na unatumia daladala unalalamika nini. Nakushauri kuwa na vipaumbele, acha makundi ya starehe kama ulevi. uzinzi then hicho kipato kinaweza kukutoa. Hebu tufanye mchanganuo hapa chini.



Tshs 542,000/=

1. Kodi ya nyumba shs 100,000
2. Chakula nyumbani shs 150,000
3. Chakula kazini shs 60,000
4. Nauli ya dala dala 30,000
5. Mengineyo shs 100,000

Jumla ya matumizi ni shs 440,000 hivyo unabaki na akiba ya 102,000. Ukitunza hii akiba kwa miezi sita unaweza ukampatie mke wake mtaji wa shs 612,000 baada ya miezi sita na mkaanza mkakati wa kununu ka plot Gongolamboto.

Chukua huo ushauri na usirudi kijijini utajuta.

Pole sana.. Ushauri huu ni mzuri sana... Ila hapo kwenye kununua plot Gongolamboto, Sio mzuri.. Maana ukinunua kiwanja kimoja, unapewa na BOMU moja.

Usirudi kijijini! Tubanane humuhumu! Ila Toa zaka na sadaka kwenye huo mshahara na MUNGU atakujaza..
 
wewe una maisha mazuri sana mpendwa ila hujitambui na ndio maana huridhiki. nimeona mahali unasema matumizi nyumbani kwa siku 8,000/-! mbona hapo unaishi kifalme kabisa? uliza wenzio kwa siku wanatenga kiasi gani kuacha nyumbani? utashangaa kuwa karibu nusu ya watanzania wote huacha si zaidi ya 3,000/- ya matumizi kwa siku na hiy ni kwa ajili ya unga, mafuta ya taa, ya kula, maharage, na viungo vyake, na on top of that wana vibanda vyao.

kwenye ofisi ninayofanya mimi (ya serikali) madereva na wahudumu wote wanavibanda vyao na walishajikomboa na nyumba za kupanga na wote hawa ni wa kima cha chini achilia mbali nyongeza za mishahaa za kila mwaka (JK akipenda), yaani hata pendekezo la TUCTA la 350,000/ wanalimezea mate. but wana furaha na courage ya kusonga mbele! sasa wewe una 840,000/ nyumbani kwako kila mwezi kisha unataka kuutupa na kurudi kijijini?

hebu muogope Mungu ndugu yangu, usitamani magari ya watu au kitu chochote usicho na uwezo nacho. mshukuru Mungu kwa kila alichokupa hata kama ni kidogo na usaidie wasio na uwezo kwa kadiri ya uwezo wako, hapo ndipo utakapoona furaha ya maisha na baraka za Mungu zikiongezeka maishani mwako.

kwa kweli mi sioni sababu ya kukata tamaa na maisha kiasi ulichofikia

pia ni vizuri ukajiendeleza kielimu, elimu ni njia ya mkato ya mambo mengi. ukistruggle kuongeza kipato chako mara kumi unaweza kustruggle hadi mwisho wa maisha yako bila kufikia lengo hilo, ila ukiamua kusoma, ni kiasi cha miaka mitatu au minne tu utafikia lengo hilo. tena hata wpte na mkeo mnaweza kwenda shuleni mkaomba mkopo HESLB kulipia masomo yenu na baada ya miaka mitatu/minne hivi, wote mnaona maisha katika mwanga bora! hebu wekeni akili kichwani hapo.

mbarikiwe
 
Unaweza kutuambia mwaka jana ulipigia watu gani kura? Usije ikawa ulichagua Kijani na Njano halafu sasa unakataa matunda yake!
 
Pole jikaze ...lakini endelea kutafuta ufumbuzi...maana hata kurudi kijijini yaweza kuwa suruhu ya matatizo kama ukiwekeza...Kuna wenzetu wanalima na kupata kipato zaidi ya mjini. Kumbuka maisha sio mjini tu......
Ukikwama saaana tafadhali tuwasiliane ili tuone jinsi ya kusaidiana...naamini na wewe waweza kwenda na gari ukiwa umefunga vioo...
 
Unaweza kutuambia mwaka jana ulipigia watu gani kura? Usije ikawa ulichagua Kijani na Njano halafu sasa unakataa matunda yake!

kaka mimi na nyumba yangu na watu wote wa karibu na mimi tulipigia kura pale mugabe - wote ni CHADEMA damu damu - naligundua hilo kwamba hizi shida zangu nyingi zinachangiwa na hawa viongozi uchwara - kweli shida ni kubwa ingawa wanasema mtoto wa kiume hakuna kukata tamaa lakini inafikia point unapiga hesabu hazipigiki.

Majonzi zaidi ni pale nikimcheki dogo nagundua kuwa future yake ni kiza kinene....
 
Back
Top Bottom