Maisha ya Ubachelor sometime yanachosha

Maisha ya Ubachelor sometime yanachosha

Bila kusahau ile mambo ya kuwekeza kwa mama lishe,

Yani akiwa na katoto kazuri basi unageuza test pilot wife, Utakula bure, katakuja kufua bure, na mzigo utakula...

Mostly ukiwa unaanza ubachela mvua ikinyesha unawaza mbono tu..aka ngono[emoji4][emoji4][emoji4][emoji4]
 
Wachezaji wa kulipwa wapo wengi kwanini ujitese
 
Ikifikaa Mida ya Kupika saa 12 jioni hujui wala huoni cha kupika.. sasa ngoja mida iendee saa 2 hiv njaa imekoleaa ndo akili inakuja..
ama kweli, dawa ni kupika mboga mchana unabakiza ya jioni kulia ugali
 
Ukiwa bachela usiombee ununue samaki wa kukaanga, nakuhakikishia rate ya kuwapika ni ndogo sana, utaenda gengen vzr tu kununua mazaga kama nyanya, ngogwe na vitunguu ila ukishaingia geto tu akili inakutuma, hv si hapo nje panauzwa maziwa ya mtindi? Kifuatacho nahc hakuna asiejua, nyanya nilikua nagawa kwa mother house. Uzuri wa maisha ya geto huoni tofaut ya ugali mbich na ulioiva, nilishawah kupika ugali mgumu nahc kupita viwango vyote, jinsi ulivyokua mgumu na mbichi ulikua umeachana achana kana kwamba ukigeuka pemben kunawa mikono ukirud mende kaingia katkat ya ugali unakula nae bila wewe kujua kua mzee mchafu yupo ndani.
 
"A bachelor is a silly stupid person who lives like a king but dies like adog "sasa tafakari....
 
Hahaaaa kuna hiii nimesahau, ni wachache sana geto wanaandaa maji ya kunawa, weng wetu tunanawa kwenye sufuria ya ugali, mimi nilikua naenda mbali zaid njaa ikikaza, maswala ya kuchota maji sijui kwenye bakuli huku nina ubao, utashangaa tu paap mikono imetua kwenye ndoo yoyote ya maji iliyowazi na karbu hata kama imejaa, baadae nikishashba ndo najiuliza hv nimefanya nini? Kaz nilizokua nazichukia zaid,
1. Kuosha vyombo
2. Kuchomoa net, kaz niliyokua naifanya bila hata kupanga nashangaa tu nimeifanya ni kuosha mwiko, hii ni kutokana na malez, kwa bimkubwa ilikua sahau vyote ila si mwiko wa ugali baada tu ya kuepua. Yoote hilo tu ndo naweza kujisifu 100%
 
ukiamka asubuhi unasepa tu... akili inasema nitatandika kitanda nikirudi... 😀😀😀😀
Unalalaje hadi shuka zinachomoka? Unazivuta? Kazi ni kunyoosha shuka kidogo,kukunja uliojifunika na kuweka mito vizuri haichukui dakika tano
 
Back
Top Bottom