Mimi aisee katika maisha ya kibachela masuala magumu ni kupika na kuosha vyombo tu. Hata hivyo uvivu wa kuosha vyombo haunisababishii kuwa mchafu kiasi hicho!
Shida ni kwamba nikiosha vyombo nakuwa mgumu kuvitumia kwa uhuru, ...nikitumia kijiko kuchotea sukari nakimbia kukisuuza....,, nikinywa chai lazima kikombe na vyombo vingine nilivyotumia nivioshe....,, zamani nilijikuta na kitabia cha kulia kwenye sufuria ili tu nisichafue vyombo vingi

na sufuria lazima niioshe ndo niendelee na mengine...
Binafsi ni kijana msafi sana, si usafi ule wa magumashi kuvaa nguo za nje safi halafu za ndani chafu! Ama kusafisha geto pale tu anapokuja manzi, no! Nina usafi wa uhakika ambao napenda nione na kuamini mwenyewe kwamba ni usafi, kuliko kupendelea zaidi kuonekana kwa watu. Mabinti wa hostel walikuwa wanaogopa kuingia ovyo geto kwangu kwa hofu ya kuchafua duh!
Shida ya vijana wengi uchafu ni tabia, kiasi kwamba walishazoea eti maisha ya uchafu ni UANAUME! Kumbe uvivu tu. Wengine wanaleta hata humu nyuzi zao wakisema mwanaume lazima uoge kwa ku-beep, unuke kikwapa, na blah blah kibao.
I can say 96% ya vijana nilio/ninaokutana na kuishi nao ni wachafu completely, hata akijitahidi namna gani kuficha uchafu ataonekana tu! 3.8% ndo wale wanaobabaisha usafi wao, angalau wanajitahidi kidogo. Then 0.2% ndo tuna usafi asilia, si wa kubahatisha!
Mleta mada umedadavua maisha ya mchafu, si ya bachelor.