Maisha ya ubachela ni vituko

Maisha ya ubachela ni vituko

Ukiwa serious maisha ya ubachela yana raha yake na ni kama adventure fulani hivi. si ajabu ukaanza kupika maharage saa saba usiku. sometime kachumbali huwa mboga kuu. Bila kusahau wakati wowote ni wakati wa chai. Kifupi wengi hutokea kuwa wapishi wazuri ingawa ishue ya kuosha vyombo hasa sururia ni ngoma.
Maharage yanapikwa usiku wa manane ikifika asubuhi yanaliwa na chai....

 
Hatar sana huwa mizinguo tu ila hata wao ni zero kwenye kupika..

Namm nimemfuata yy yani najua kusonga ugali tu mboga usiniambie..
wazee wetu huwa mbwembwe nyingi ila kwenye kupika ndo zero! Umenikumbusha mzee alipika ugali mtepe enzi hizo, sasa ole uinuke mapema, ni nakoz tu
 
Soksi zenyewe nafua bila shida..
Msisahau kuoga na kufua makufuli ni mitihani mingine ya ubachela aachilia mbali ile harufu pendwa ya soksi
Tatizo surali za jinzi, shati ni changamoto sana..
 
Mayai yaliyo ungwa nyanya na kachumbali ndo mboga kuu..
 
*Fahamu maisha ya ubachela*

Maisha ya ubachelor unaweza kujishaua kufululiza kupika msosi hata mwezi mzima ila vyombo visafi vikiisha ndani unarudi kwenye utaratibu ule ule wa kula chipsi na paja la bukujero.Maisha ya ubachela kila siku tunapoteza vijiko kidogo kidogo kwa kumwaga maji ya ukoko wa ugali.

Maisha ya ubachela unaweza kuloweka sufuria ulopikia ugali likakaa na maji wiki nzima yakianza kunuka unamwaga halafu unaweka tena maji mengine.

Maisha ya ubachela mara nyingine neti hugeuka kuwa hema.Ikichomekwa haichomolewi mpaka siku utakapopata mgeni.

Maisha ya ubachela hufika kipindi mtu unageuka mbwa, unanusa kwanza nguo ili ujue kama unaweza kuipa round ya pili au hapana.
Wewe bila shaka utakuwa ni Junior bachelor, Senior bachelao hawezi kuwa hivi...huu ni uchafu uiopitiliza!
 
Mimi nina miaka zaidi ya mitano sijatumia net na nipo dar makao makuu ya mbu.
Ule usumbufu wa chomoa chomeka halafu ukizingatia muda mwingine nafika niko maji nikajikuta nishaisahau net milele.
Hata nikienda guest, utaratibu haubadiliki.
 
IMG_0432.jpg
 
Huo si ubachela, huo ni uchafu grade A

Dj piga kibao cha 'sifa za kijinga' cha Mr Ebbo kiwafikie waunga mkono wote
 
We acha tu wengine ambao hatuna ma dereva unarudi ukipaki umechoka yani hata hicho chakula kwenda kununua unasahau, nashukuru kuna jirani kwa mbali kidogo anakaanga visamaki huwa nampigia simu apike na ugali aniletee namlipa ila mwiko vyombo vichafu kwangu maana ni kukaribisha mende, ninavyowachukia sasa
 
ni mwezi wa 6 sasa toka ninunue neti mpya na kuichomeka sijawahi kuichomoa yaani mpaka inanuka vumbi aiseeee....mashuka yakichafuka yanapandiana tu kwa bed maana kufua kwa wiki2 mara moja
 
Apa tutawajua wasafi na wachafu
 
Back
Top Bottom