C'mon bruh! Lets face it, Norway isn't the favorite destination for Americans. South America is.
Duh,
unajua niliposoma hiyo comment yako kwanza nimeghadhabika. Nikajiuliza kuna Mmarekani gani anataka kwenda kuishi Latin america.
Halafu nikapata wazo, nikawauliza wamarekani wachache nilionao karibu hapa.
Research question yang ikawa: If you had the option to live in any South American Country OR any of the Scandinavian countries, which one would you choose?
Kati ya Wamarekani 8 niliowauliza, 6 walisema South America (huku mmoja akiwa specific kabisa akasema Chile), na wawili tu walisema Scandinavian country.
Majibu yao yamenishangaza na kunitatiza mimi kama Mtanzania na Muafrika. Sikuelewa kwa nini Mmarekani angependa kuishi Latin America akaacha Norway kwa mfano. Sababu zao zilikuwa nyingi na tofauti (labda sababu ambayo ilikuwa common kwa wote ni WEATHER - latin America has the perfect weather na haina mantiki kutoka say Minnesota kwenye snow mpaka April ukahamie Finland).
Katika watu hao 8, niliwauliza watatu (03) kama option ingekuwa NCHI YOYOTE AFRIKA au NCHI YOYOTE YA SCANDINAVIA...naamini unajua jibu lao.
Ndipo nikawaza kuwa sisi tunabishana kwa kuwa wote ni Waafrika, na tunaangalia 'preferences' za wamarekani kwa macho yetu, kwa vile vitu ambavyo sisi tunaviona vizuri kwetu.
Conclusion yangu kwa sasa ni hii;
- Kwa Muafrika ambaye mpaka karne hii hajavuka hata hatua ya kwanza ya demokrasia, ambaye huduma kwa jamii ni kwa hisani ya serikali na sio kwamba ni haki yake, ambaye amekua akiona rushwa kila mahali, ananyanyaswa na watumishi wa umma regardless position zao..Mtanzania huyo kwake kuwa mfungwa Norway ni afadhali kuliko kuwa mtu huru Tanzania.
- Nadhani tutakubaliana kuwa Marekani sio the IDEAL country. Kuna mambo mengi wangetamani kuwa kama hizo ulizoziita 'socialist Europe' (hili jina wamepewa na Wamarekani maana wao wenyewe ukiwauliza hawajioni ni socialist hata kidogo but anyway).
- Kuna middle ground ambayo nchi kama yetu tungekuwa serious tungelenga kuifikia. Middle ground between Socialist Europe na Capitalist America. Sisi ni taifa changa (kwa kulinganisha na Marekani). Hatuna system ambayo ipo so cemented kwamba inakuwa ngumu kubadilika. Tunayo nafasi kama viongozi wetu (au niseme wanasiasa ili kujumuisha vyama vyote) wasingekuwa wabinafsi kuunda katiba ambayo itakuwa a mix ya hizo two sides. Katiba ambayo inaweka misingi (systems) ya uongozi wa nchi yenye kutoa fursa sawa kwa capitalism na kutoa fursa kwa serikali kuhakikisha huduma muhimu zinapatikana kwa watu wote regardless hali yake ya kiuchumi (kama hizo socialist countries). Katiba ambayo haitakuwa na extreme freedoms mpaka inakuwa ngumu ku-control ustaarabu wa watu (Gandhi alisema 'freedom without responsibility is chaos').
Yaani we have the perfect country in Tanzania kuijenga nchi yetu kuelekea huko. Nahisi tatizo ni kuna watu wanaotaka kuiga nchi moja tu. Mimi napendekeza kufanya research hasa ya vile vinavyofanya kazi kwenye nchi hizo zilizoendelea na kongwe (Europe, Asia, Marekani) na kutafuta balance. Kufanya utafiti hasa ya sheria ambazo zimekuwa mwiba kwao (hapa naandika nikiwaza gun laws/second amendment) na kusema sisi tuna uhuru wa kuandika msingi mpya, je tunaichukuaje hii concept na kuiboresha?
Mimi sidhani kama suala la katiba ni la mwaka mmoja la sivyo litafanywa kisiasa na tutapata katiba ya chama kimoja. Kwa mawazo yangu, hata kabla hatujafika huko, hawa wanafunzi wetu wanaosoma sheria wawe encouraged kufanya utafiti (hasa wa mrengo wa compare and contrast - tena kwa specific vifungu) maana ni kutoka katika maandiko hayo tutakuja kufanya mchujo wa mwisho.
Pili ni kuwahimiza wananchi, kwanza, kujishughulisha na maendeleo ya maeneo yao na pili, kuzoeshwa kuwa huru kutoa maoni (na hatimaye kuufanya mfumo rasmi wa uendeshwaji wa nchi). Mtu asiogope kutoa maoni, mtu asibezwe kwa maoni yake. Kuipitia hayo maoni kuanzia ngazi za nyumba kumi, kata, kijiji na kuendelea tutajikuta na yale common maoni yaliyosemwa na wengi na yale machache pia wakati wa kuunda sheria kuu kuangalia jinsi gani walioyatoa watalindwa (au watakuwa incorporated). Hili si suala la kamati sijui ya maoni ya katiba. Ni mchakato wa muda mrefu lakini ni lazima uwe na kiongozi ambaye ataruhusu haya yatokee. Baadaye itafika mahali nasi tutakuwa kama hawa Wamarekani na Wanorway tunaotamani kwenda kwenye magereza yao. Wananchi watakuwa huru, watatamani, watashiriki kwenye maendeleo ya nchi. Wananchi watajiona wana amani kutoa maoni yao bila kuogopa ku...
Tutakuwa na uongozi wa wazi, wa haki, wa uwajibikaji, wa kutokuogopana na kutishana, wa kuheshimiana, wa kuhshimu sheria (rule of law) na demokrasia (democracy as we will decide to define it - sio demokrasia kwa kumuiga Mmarekani au demokrasia kwa kumuiga Mchina...we find the balance, we define our own), ambao viongozi wetu na watumishi wote wa umma watatambua kuwa wao ni 'stewards' tu wa muda wa rasilimali za wananchi.
Ninadhani hii ndiyo Marekani/South America/Norway ambayo tunaiwaza tunapobishana hapa. Inawezekana kujengwa kwenye nchi yetu.