Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 91,913
- 112,263
Hilo ni dorm la Mabibo? Aisee...limechoka sana
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
@ Mopao na Jack mmenichekesha na kunikumbusha mengi nyie watu tunafahamiana sio siri, mnakumbuka yule jamaa alieenda sijui block C akakuta kuku aliyemnunulia demu wake apike wale nakumbuka ilikuwa sku ya J2 jamaa kutoka church akakuta mafupa na jamaa kavaa taulo yake kajitandaza kitandani na nilibaunsa kumpiga hawezi kulia hawezi ikabidi achukue Maliboro aweke kichwani kwa vile jiko lilikuwa na moto bado likayeyusha mnailoni ikaanza kumchoma kichwa
Rural Swagga we ni noma mtu wangu. Hii picha inanikumbusha long time sana. Inanikumbusha maisha ya anasa kipindi cha Boom. Cheki watu wanavyojimwaga na misoda penye REDD. Huyo dada ndo kanywa soda na simu kaweka pembeni anajua hakuna wa kuiiba kwan kila mtu keshavuta mkwanja. Usiombe miezi dume iwadie. Ni mtafutano mtu wangu, hiyo simu ingekuwa ishapitiwa siku nyiiiingi! Tupe picha nyingine mkuu.............
Tehtehteh....nimeshindwa kujizuia kucheka aisee. Maana'ke ni kwamba jamaa alimegewa demu'ake...
Pole zake huyo jamaa...
Coloured: Tehe ...tehe.....Ebwanaeeeeee....Hii ni kali mtu wangu. Thanks a lot kwa kuripoti vzr hili tukio. Yaan ntabaki nacheka Xmass yoote..Aiseeeeeeee...Huyo mdada atakuwa ni MAFIA kinoma. Betray ya hivi ni nomaaaaaa....jamaa hatasahau maisha yake yooote nakwambia. Najiuliza jamaa alienda church kufanyaje sipati jibu. Huenda akiwa church aliombea na yule kuku....Daaaa....Napiga picha ya hilo njemba na kitaulo lakini haitoki..inaungua. Ebwana mkuu Ubarikiwe...
Ngoja nikupatie nyingine kijaaanaaaa!!!
Bros and sists,
Hope mko poa kbs,
Naomba leo tujikumbushe siku za mwanzo vyuoni hasa HOSTEL, mimi nilijiunga na chuo cha UDSM nikitokea mmamndenyi na ucha Mungu wangu na kupangwa pale MABIBO Hostel Block D gorofa ya 2. Nilifurahi sana kujiunga na masomo ya Elimu ya juu na kubahatika kukutana na cream ya nchi nzima, nilikuwa na shauku kubwa ya kujua roommates wangu na kutenegeneza marafiki wapya.
Hali haikuwa kama nilivyotarajia hasa kwenye chumba changu, nilipangwa na watoto wa mujini waliokuwa wanazijua starehe na anasa za dunia. Mimi nilikuwa na poketi money yangu elfu kumi navaa soksi naingiza ndani nafunga raba bendi juu ili isiibwe kwani boom lilikuwa halijatoka na hata Bank a/c nilikuwa sina. Wenzetu walikuwa wanafweza hadi kukodi tax kwenda main campus. Nilipangwa kitanda cha juu kwa vile vya chini vilikuwa vimewahiwa tayari. Nili report siku ya ijumaa nikiwa na uchovu wa kutoka milimani kwetu nikawahi kulala. Ilipofika saa 7 nilisikia miguno kwa chini nikahisi mwenzangu mgonjwa, ila iliambatana na vicheko kucheki vizuri mwenzangu alikuwa ana jimama likubwa liko juu yake(........)
Ikawa ndio mchezo kila siku sasa mimi nilikuwa hata gal friend sina. Nikirudi mchana rum kupunzika nakuta mwingine amerudi na mwanamke na wamenifungia nje tena/exile. Nikavumilia kama mwezi nikashindwa nikakusanya kilicho changu nikaenda kulala chini kwa washikaji main campus at least huko nilipumua sito sahau mabibo hostel .......
Ni mimi tu au na nyie mlinyanyaswa au kunyanyasa wenzenu?