Umesema kweli.Kwa kawaida ya maumbile bin adam hukiri kwamba kuna muumba kabla hata ya kupata mwongozo kuhusu huyo muumba, na hili hutokana na jinsi alivyoumbwa yeye binafsi pamoja na vile vilivyo mzunguka mfano anga lilivyoumbwa au ardhi ilivyotandikwa milima miti pamoja na bahari, hivi ni vitu ambavyo bin adam aliyekamilika akijitazama yeye pamoja na vinavyomzunguka basi hukiri ni lazima kuna muumba, changamoto inakuja kwamba ni nani muabudiwa halisi, hapo ndio utakuta tunagawanyika.