Invisible
JF Admin
- Feb 26, 2006
- 16,286
- 8,447
Kasheshe,Zitto,
Mimi nakuaminia sana, lakini katika kukujenga... nakuomba ujirekebishe kwenye haya.
1. Punguza umimi, unao sana mkuu, mfano hii interview haikuwa lazima uilete wewe.
2. Punguza kuona wengine wajinga, hii mara nyingi umetukana wazee wenye heshima zao Bungeni, tumia lugha laini lakini ujumbe ufike... Nyerere alikuwa akimtusi Mwinyi lakini kwa lugha ya kiutu uzima.
3. Munkari, sio kila jambo linahitaji majibu, jifunze kutoka kwa Mzee John Samuel Malecela. Usiwe kama Mh. Sitta.
Mwisho nakukubali sana mzee endeleza libene.
Namnukuu Zitto:
ndugu zangu, ninawaomba radhi niweke mahojiano yangu haya na gazeti la jambo leo katika uwanja wetu. Humo kuna kauli yangu rasmi kuhusu mijadala inayoendelea. Baada ya muda naomba mod akusanye hizi thread nyingi zinazomhusu zitto na kuziweka pamoja. Nadhani kwenye ile thread ya rev. Kishoka.
......
nawaomba radhi tena kwa kuweka hii interview. Nadhani ni muhimu wakati huu. Naelewa kuna zitto sana, mniwie radhi kwa hili langu mwenyewe!
Sasa Zitto kama mwanachama wa JF sidhani kama kakosea, ni kwakuwa alikuwa na access ya information hizi sisi hatuna, kutushirikisha nadhani hajakosea. Tena, katumia lugha ya kiungwana sana...!
Aidha, sipendi kumsemea kuhusiana na ushauri mwingine lakini nadhani atakuwa kakusoma.