Kibunago
JF-Expert Member
- Jan 11, 2008
- 300
- 122
Zito alisema,
JokaKuu kama ni kweli,nakubaliana nawe hasa ulipochagua kwa umakini kutumia neno wamechafuka. Kwa maana halisi ya kuchafuka, hakika tunaweza kusema kuwa Watanzania wote (wakiwemo mimi na wewe) wamechafuka, maana tumechafuliwa na kitendo cha mtu au watu wachache kutumia fedha za Umma kinyume na taratibu na sheria ziongozazo.
Hata hivyo ni bayana kuwa kuchafuliwa huko hakuwezi kuwa sawa na kusema Wabunge wa CCM wote au in this matter Watanzania wote tulipokea pesa hizo za kifisadi.
Unajua mara nyingi tunaposhindwa kusingle out clearly nani kafanya kosa gani kwa ushahidi usio mashaka ndipo tunapoteza hata namna ya kuwaajibisha wahusika wakosefu. Mfano huu uko wazi katika hukumu ya hivi karibuni iliyowaacha Watz wengi hoi pamoja na kwamba kweli raia wasio na hatia waliuawa. Unaona hapo tunaweza kusema kuwa Jeshi la Polisi lilichafuliwa (lilichafuka) kwa kitendo cha Askari / baadhi ya Askari wake lakini hatuwezi kusema kuwa Jeshi la Polisi lote kama Taasisi walihusika kuua.
Yaani tunawashauri na siyo kuwatisha Wabunge wetu kuwa makini wanapotuumu ili kauli zao zisiendelee kubaki kuwa kelele baada ya kutupwa nje kwa TKO ama kwa kukosea kueleza kosa lililotendwa au kuonyesha Mhusika / Wahusika au kwa kukosa kuwasilisha ushahidi mwanana.
JokaKuu unafafanua,Wabunge wote wa CCM walipata fedha za KAGODA kwenye kampeni zao
..kama CCM walichota fedha za Kagoda na kuzitumbukiza kwenye kasma ya fedha za uchaguzi basi wabunge WOTE wa CCM wamechafuka.
JokaKuu kama ni kweli,nakubaliana nawe hasa ulipochagua kwa umakini kutumia neno wamechafuka. Kwa maana halisi ya kuchafuka, hakika tunaweza kusema kuwa Watanzania wote (wakiwemo mimi na wewe) wamechafuka, maana tumechafuliwa na kitendo cha mtu au watu wachache kutumia fedha za Umma kinyume na taratibu na sheria ziongozazo.
Hata hivyo ni bayana kuwa kuchafuliwa huko hakuwezi kuwa sawa na kusema Wabunge wa CCM wote au in this matter Watanzania wote tulipokea pesa hizo za kifisadi.
Unajua mara nyingi tunaposhindwa kusingle out clearly nani kafanya kosa gani kwa ushahidi usio mashaka ndipo tunapoteza hata namna ya kuwaajibisha wahusika wakosefu. Mfano huu uko wazi katika hukumu ya hivi karibuni iliyowaacha Watz wengi hoi pamoja na kwamba kweli raia wasio na hatia waliuawa. Unaona hapo tunaweza kusema kuwa Jeshi la Polisi lilichafuliwa (lilichafuka) kwa kitendo cha Askari / baadhi ya Askari wake lakini hatuwezi kusema kuwa Jeshi la Polisi lote kama Taasisi walihusika kuua.
Yaani tunawashauri na siyo kuwatisha Wabunge wetu kuwa makini wanapotuumu ili kauli zao zisiendelee kubaki kuwa kelele baada ya kutupwa nje kwa TKO ama kwa kukosea kueleza kosa lililotendwa au kuonyesha Mhusika / Wahusika au kwa kukosa kuwasilisha ushahidi mwanana.