Kiongozi, kama bado kuoa wala usikatishwe tamaa na hizo tarakimu. Sio wazazi wote wenye fikra za kuozesha kwa kuuza binti zao. Na bahati nzuri, siku hizi unakuwa katika urafiki kiasi kwamba, binti anaelewa uwezo na kipato chako, kama kweli ana nia ya kuishi na wewe wala hatokubali kuidhinisha mahari ya 6m, hata yeye ana say katika hili..!
Kama wakati umefika, unayo nia ya kuoa, lakini tatizo ni hili [mfano] usijipe hedeki, mchumba wako atatengeneza njia tu...! Coz kadri unavyozidi kusubiri, umri haukusubiri.
Mkurugenzi,sijaoa,lakini nikikatishwa tamaa na hawa binadamu wasiojielewa hapa JF nitakuwa na akili kama zao ....
W atu wapo hapa JF kujiliwaza na ufukara walionao kwa kuishi masiha ambayo wanayaona ndotoni tu,kuna watu humu maisha yameshawapiga sana na wanajidai wanaishi maisha ya juu,wengine wanataka waje wajifidie kwa wanaume ambao watawaoa,wengine imeshashindikana kuolewa basi wanakuja hapa kujilisha upepo na kujidai hawana shida na ndoa,huu ni uji nga mkubwa sana
Mkurugenzi,ninachotaka kusema hapa ni kuwa,kuna watu wana njaa sana hapa JF na wanataka kuponea kwenye mahari au vibuzi vyao,hawa ni wengi sana,tatizo lao hawataki kujikubali tu,kwani wakijikubali watabadilika nini?
Najua kuwa hata kama huyo wa mil 6 atagoma kushusha nitakwenda kuona mwingine ambae atajua kuwa thamani ya mwanae haiwezi kuletwa na mahari,wanawake wapo wengi sana,ni kitu gani kitanifanya nimng'ang'anie mwanamke mmoja?
Hivi huyo ana nini kwanza?
Mkurugenzi,katika vitu ambavyo havipo kabisa kwenye mawazo yangu ni suala la kuhangaikia kumbembeleza mwanamke kumuoa au wazazi kupunguza mahari,akiniambia mil 6 na uwezo sina namuambia hivi; "Mzee,kwa kukusaidia kutopoteza muda na ku nipotezea muda wa mazungumzo meeengi,uwezo wangu ni laki 2 tu,kama unaridhia nipe mwanao tukaanze maisha kama unaona haiwezekani niambie hapa hapa nianze harakati za kutafuta ambae atanifaa na wa kukubali kiwango changu" .....kisha namsikiliza
Yanini kubembelezana bana wakati "soko huria" na wapo weeengi sana?