Tinna, hakuna niliposema watu waoe/waolewe bure, hayo umeleta wewe. Japo siku hizi familia nyingi tu zinaozesha bila kutoza mahari. Nilichosema ni kuwa, wadada wana ''feel the pinch'' kwa waume zao, kwa hiyo ikitokea mahari imekuwa kubwa kushinda uwezo wa kijana huwa wao ndio huomba kwa wazazi ili iwe reasonable, kutokana na uwezo alionao mchumba wake.
Ninachokiona kwako labda ni kutaka ''kuweka heshima mjini'', na sio wewe tu, mpo wengi wa sampuli yako. Siwezi kutoa hukumu coz hii ni platform kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni, lakini unaonekana kuweka ''heshima ya pesa'' kuliko utu wa huyo anayekuoa..! Na wala sio dua, siwezi kukuombea mabaya bhana, ila kama unampenda huyo mwenzako, utamjali tu na kama upo kwa ajili ya alichonacho, hutajali.