Mahakama yamwachia huru Halima Mdee

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuacha huru mbunge Viti Maalumu (asiyekuwa na chama), Halima James

Alifukuzwa uanachama wa Chadema, yeye pamoja na wenzake 18, tarehe 27 Novemba mwaka jana.

Alituhumiwa kwa makosa usaliti, ikiwamo kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuhujumu Chadema; kughushi nyaraka za chama hicho, kujipeleka bungeni na kujiapisha kuwa wabunge wa Viti Maalum, kinyume na maekelezo ya chama chenyewe.

Mpaka sasa, bado yuko bungeni kufuatilia, Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuendelea kung’ang’aniza kuwa bado wanachama wa chama hicho.

05b14b78-eaa0-46e4-bd57-4eb8629a8642.jpg


Halima Mdee (kushoto), akiwa na Ester Bulaya kwenye jengo la mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu

Uamuzi wa kumuachia huru Mdee, umetolewa na Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba leo Alhamisi, tarehe 25 Februari 2021. Akisoma uamuzu huo, Hakimu Simba amesema, upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka dhidi ya Mdee.

Alisema, “…baada ya kupitia ushahidi wote, nimejitosheleza kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yake. Hivyo, mshitakiwa nimeamua kumuachia huru.”

Mdee alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza, tarehe 10 Julai mwaka 2017.

Mbunge huyo viti maalumu alidaiwa kutenda kosa hilo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya Chadema, ambapo alidaiwa kusema, “Rais John Magufuli anaongea ovyo ovyo, anapaswa kufungwa breki.”

Katika utetezi wake, Mdee alidai kuwa maneno aliyodaiwa kuyasema hayaoneshi kama yalikuwa yanamlenga nani; na kudai kuwa mtu anayeongea ovyo ovyo maana yake, anaongea vitu ambavyo sio kweli na havina mantiki.

Mdee amefika mahakamani hapo akiwa na swahiba wake mkuu, Ester Bulaya.

Chanzo: Mwanahalisi Online
Kwani alikuwa rumande?
 
Je, asingesalimu Amri na Kukubali kutumika na Tawala ( Mamlaka ) ya sasa ( kutokea Upinzani ) tena CHADEMA hii Hukumu yake ingetoka hivi kwa Kumkuta hana Hatia yoyote? Ni Unafiki mtupu na wenye Akili tulishategemea Hukumu kama hii Kutolewa labda Wapumbavu tu pekee ndiyo walikuwa hawajalijua hili tokea zamani.
 
..alisindikizwa na maafisa wa ubalozi, pamoja na walinzi wa jamhuri waliokuwa wakimlinda wakati wa kampeni.

..na kabla ya hapo jamhuri ilimpatia pasi mpya ya kusafiria kwasababu TL alikuwa anatumia pasi ya zamani.

..ndio maana najiuliza kwanini Polisi hawakumkamata; kwasababu inajulikana ana kesi 6 mahakamani, na zote zilikuwa zinaahirishwa kwasababu ya kampeni za uchaguzi.

..Je, serikali iliwaogopa mabalozi walioamua kuingilia kati suala la TL?
Likely ndiyo maana siku Lissu alipo kamatiwa kwenye korido za ofisi za ubalozi na bahati watu wa ubalozi wakaona scenario mzima wakaamua kumfuata hadi pale central
 
Je, asingesalimu Amri na Kukubali kutumika na Tawala ( Mamlaka ) ya sasa ( kutokea Upinzani ) tena CHADEMA hii Hukumu yake ingetoka hivi kwa Kumkuta hana Hatia yoyote? Ni Unafiki mtupu na wenye Akili tulishategemea Hukumu kama hii Kutolewa labda Wapumbavu tu pekee ndiyo walikuwa hawajalijua hili tokea zamani.
Upo sahihi kabisa kiongozi
 
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuacha huru mbunge Viti Maalumu (asiyekuwa na chama), Halima James

Alifukuzwa uanachama wa Chadema, yeye pamoja na wenzake 18, tarehe 27 Novemba mwaka jana.

Alituhumiwa kwa makosa usaliti, ikiwamo kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuhujumu Chadema; kughushi nyaraka za chama hicho, kujipeleka bungeni na kujiapisha kuwa wabunge wa Viti Maalum, kinyume na maekelezo ya chama chenyewe.

Mpaka sasa, bado yuko bungeni kufuatilia, Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuendelea kung’ang’aniza kuwa bado wanachama wa chama hicho.

05b14b78-eaa0-46e4-bd57-4eb8629a8642.jpg


Halima Mdee (kushoto), akiwa na Ester Bulaya kwenye jengo la mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu

Uamuzi wa kumuachia huru Mdee, umetolewa na Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba leo Alhamisi, tarehe 25 Februari 2021. Akisoma uamuzu huo, Hakimu Simba amesema, upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka dhidi ya Mdee.

Alisema, “…baada ya kupitia ushahidi wote, nimejitosheleza kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yake. Hivyo, mshitakiwa nimeamua kumuachia huru.”

Mdee alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza, tarehe 10 Julai mwaka 2017.

Mbunge huyo viti maalumu alidaiwa kutenda kosa hilo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya Chadema, ambapo alidaiwa kusema, “Rais John Magufuli anaongea ovyo ovyo, anapaswa kufungwa breki.”

Katika utetezi wake, Mdee alidai kuwa maneno aliyodaiwa kuyasema hayaoneshi kama yalikuwa yanamlenga nani; na kudai kuwa mtu anayeongea ovyo ovyo maana yake, anaongea vitu ambavyo sio kweli na havina mantiki.

Mdee amefika mahakamani hapo akiwa na swahiba wake mkuu, Ester Bulaya.

Chanzo: Mwanahalisi Online
Kila sekta,inaendeshwa na jiwe,

Sent from my TECNO CD6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom