Mahakama Kuu yabatilisha Vifungu vya Sheria vinavyowapa mamlaka Wakurugenzi kusimamia Uchaguzi

Je wewe unashauri je ?!. Kwamba huu utaratibu wenye elements za kikoloni ndiyo uendelee au ?!.

WaTz tumerogwa sehemu si bure !!

Hapana.
Nadhani hujamuelewa alichosema, unamlaumu bure na kumbe yeye kasema tu ukweli ulivyo. Mahakama haiwezi kubadilisha sheria kama mleta mada alivyosema. Baada ya uamzi huu wa mahakama inatakiwa bunge lipitishe mabadiliko ili sheria mpya itakayokuwa imepitishwa na bunge iweze kutumika. Na ukiangalia kwa makini, toka sasa hadi 2020 kwenye uchaguzi unaofuata, ukiacha hizi chaguzi za mitaa, mda wa bunge kufanya hivyo haupo, hasa ukichukulia kwamba hili ni jambo wasilolitaka wanaotawala.

Njia inayowezekana ni kwa vyama vya upinzani kukomalia kufanyika uchaguzi wowote bila marekebisho kufanyika na wafanye hivyo kwa kuwaelimisha wananchi, na kuomba msaada toka kwenye Jumuia za Kimataifa.

Hii ni kazi inayotakiwa waifanye kwa nguvu zote tokea sasa hivi na kuendelea mbele.
 
Je wewe unashauri je ?!. Kwamba huu utaratibu wenye elements za kikoloni ndiyo uendelee au ?!.

WaTz tumerogwa sehemu si bure !!
Kaka Vifungu Vitaendelea Kutumika mpaka Pale Serikali Itakapopeleka Muswada Wa Marekebisho Ya Hiyo Sheria, Vifungu Vinakosa Uhalali Kama Serikali Ishapeleka Muswada Bungeni Then Bunge Likarekebisha Vifungu Husika Lakini Serikali Kwa Maana Ya Tume Ikaendelea Kuvitumia
 
Mmeweka "alama kwenye taifa letu," Najua Fatma yupo, huyo Bob bado yupo au alishaondoka?

Hii ni hatua ndogo sana, hata kama ni hatua nzuri kuelekea kwenye chaguzi huru na za haki. Mda unakwenda mbio sana, marekebisho mhimu kwenye taratibu za uchaguzi yanatakiwa yafanyike haraka ili uchaguzi wa 2020 uwe halali.
Sina matumaini sana kuwa hilo litawezekana.
Lakini mahakama ikishabatilisha huwezi kuendelea kutumia vifungu hivyo tena. Labda serikali ikate rufaa na hukumu ibatilishwe, vinginevyo mabadiliko ni lazima
 
Hakuna kitu kama hicho

Tanzania hakuna Judicial Review, yani nguvu ya mahakama kubatilisha sheria, ikafa hapo hapo. Ambacho ndio maana ya neno la Kiswahili "batilisha."

Katiba inasema mahakama nguvu yake inaishia kulinasihi bunge hii sheria imevunja katiba, do something ( rekebisha, futa, fanya ufanyavyo...)

Na haitakiwi kuzidisha: hakuna kutoa time frame (nakupa siku saba to do something) wala kutahadharisha madhara yake (usipo do something itakuwa hivi na vile).

Kwa hiyo, hivi tunavyoongea ukitokea uchaguzi kesho asubuhi ni hii sheria ndio itatumika.

Nchi ambazo zina Judicial Review, mahakama ikisema sheria hii ni batili sheria hiyo inakufa papo hapo!

Ukibisha njoo na vifungu na vipengele vya sura na ibara
 
Mtusaidie kujua kilichobadilishwa huenda moyo wa kwenda kupiga kura ukarudi tena
Hakuna kilichobadilishwa Bali kimebatilishwa.

Naamini serikali chini ya AG watakata rufaa ili kuvuta time. Bongo ya sasa siiamini. Wanaweza wakawa wamekuja na hiyo hukumu kimkakati ili kwenye rufaa ikiamuliwa vingine inakuwa vigumu kuilaumu mahakama.
 
Mtusaidie kujua kilichobadilishwa huenda moyo wa kwenda kupiga kura ukarudi tena
Itakuwa marufuku hao wakurugenzi kusimamia uchaguzi na kutangaza matokeo maana wanatabia ya kutangaza matokeo wanayotaka wao au aliyewateua
 
Huyo ndiye shangazi wa taifa letu aliyekulia na kusomeshwa kwa huduma zoote za ccm lkn anaona ni heri auvae uzalendo ili kuwatetea wanyonge.
Hongera sana shangazi
Habari nzuri sana hii.

Kila siku nawaambia wanasiasa wasiishi kwa mazoea. Wakurugenzi sasa wajipange upya kuchakachua kura.

Asante sana Chacha. Umeleta mabadiliko tunayoyataka. Tunaelekea kwenye tume huru sasa. Asante Mheshimiwa Fatuma Karume. Mumeacha alama kwenye taifa letu.
 
Habari nzuri sana hii.

Kila siku nawaambia wanasiasa wasiishi kwa mazoea. Wakurugenzi sasa wajipange upya kuchakachua kura.

Asante sana Chacha. Umeleta mabadiliko tunayoyataka. Tunaelekea kwenye tume huru sasa. Asante Mheshimiwa Fatuma Karume. Mumeacha alama kwenye taifa letu.
Una uhakika hawawezi kupindua meza?
 
Mkuu tayarisha kichinjio chako mapema maana makada wote wa ccm kwa kofia ya ukurugenzi sasa hawatakaa tena mezani na kuamua nani mshindi
Mtusaidie kujua kilichobadilishwa huenda moyo wa kwenda kupiga kura ukarudi tena
 
Huo ndiyo msimamo thabiti haswa
Safi sana!

Kiburi cha Jiwe sasa kitapungua.

Ni imani yangu mahakama itakuwa imetamka kuwa vifungu hivyo ni kinyume na katiba na kuagiza vifutwe/virekebishwe.

Ushauri:
Serikali/Bunge wasipotekeleza amri hii mpaka tarehe ya uchaguzi mkuu wa mwakani,nashauri wapinzani waiombe Mahakama izuie uchaguzi mkuu unaokuja mpaka pale amri hii halali ya Mahakama Kuu itakapotekelezwa.
 
Huyo ndiye shangazi wa taifa letu aliyekulia na kusomeshwa kwa huduma zoote za ccm lkn anaona ni heri auvae uzalendo ili kuwatetea wanyonge.
Hongera sana shangazi
Mmawia.

Vipi wameshaweka wazi kuwa nani atasimamia sasa hizo chaguzi?

Kwa style hio ccm wanaweza wapate jimbo la chato tu.
 
Back
Top Bottom