Kuna mambo ya kimkakati yalikuwa yanakamilishwa. Katikati ya wiki ijayo atakuwa Zanzibar kufunga kazi. Pia akina Ben Mkapa na Kikwete wanaanza ziara za kuzunguka nchi nzima kumnadi Tingatinga
Inaonekana mtoa mada hafuatilii matangazo ya biashara, sasa hivi Magufuri anawazidi hata cocacola, tigo na voda kwa matangazo ya biashara yake na kwenye mabango ndio usiseme mpaka kinyaa.
Kama ingelikua Lowasa yupo kimya ungelisikia kelele za Magamba ooh yupo Germany Mara moja hahaaahaa
Kumbe wanamsikiliza sana Magufuli anavyomwaga sera zake. Wamemmiss sana
nimekuwa nikifuatilia taarifa za habari kupitia vituo mbalimbali tangu jana tarehe 10/10 nimeona zinarushwa za Edward Lowassa, Samia Suluhu, Maalim Seif, Babu Duni na Dr Shein. Wadau kwa anayejua Magufuli yupo wapi atujuze.........
Tumemmisi mkuu, UKAWA tunataka Ushindi usiokuwa na visingizio. Mwangalieni mkapa asije kutukana tena muwe mnamwandalia vya kusema, Kikwete apite mikoa ya CCM na mwambie asikanyage Arusha, Mara, Mbeya, Iringi labda aende mikoa ya pwani na ngoma ya mdundiko atawapata wanawake wengi. Tunamtaka Magufuli maana anafurahisha sana Jukwaani kama Comedy
Kitu usichokijua ni sawa na usiku wa giza, ccm bado itaendelea kushinda katika chaguzi zake zote, kwani upinzani na wana JF mnachofanya ni propoganda tu, hata chaguzi za serikali za vijiji/mitaa kelele hizi zilikuwepo pia, naamini siku ya ushindi wa upinzani hakutakuwa na vitisho wala kelele kama hizi zilizopo, ccm bado ni taasisi kubwa sana tofauti na uelewa wa watu wachache wanavoelewa, kushindwa kwa Lowasa kuibomoa ccm, ndo sasa imekuwa imara sana, na ushindi utakuwa wa kishindo.
Kwasiku 2. sasa sijaona ripoti ya kampeni ya ndugu Magufuli kwenye vyombo vya habari.amepotelea wapi?
Vipi Magufuli alikuwepo mkutano wa CCM mwembe yanga Jana?
Hakuwepo,mgeni rasmi alikuwa Nchimbi
Acha uongo wewe gamba Makomeo alikua Chalinze na Bagamoyo juzi ijumaa Tarehe 9. 10. 2015.......Kama pumzi imekata semeni imekata tu, chezea mziki wa Lowassa ww??? Lazima aombe poo sababu anapata dozi ambayo akutegemea, pamoja na kusomba watu na mafuso, matusi na kejeli nyingi bt wa TZ wamegoma kuelewa, kajitahidi kuongea ka chiriku, kajidhalilisha hadi na push up majukwaani lkn hamna kitu, kiukweli hata ka ni ww lazima ungeomba poo.
Utamsikia leo akiwa zanzibar.
Tushajua Tumeshinda Magufuli Yupo Mezani Na Wataalamu Kujadili Na Kupanga Mipango Madhubuti Ya Kuendesha Serikali....!!