Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

Pesa nyingi ipo si unajua hata huko wizarani huwa kuna pesa hubakia ( Kasma) hizi pesa huliwa kijanja janja hasa kipindi bajeti ikikaribia ndipo wajanja wachache huzitengenezea mazingira ya ufisadi, kuna pesa nyingi tu zinavuja kwenye Taasisi nyingi hizo pesa zote zikidhibitiwa hakika pesa ya Elimu bure itapatikana pia hata matibabu bure pia yataweza kupatikana kwa wale wasio na uwezo.
 
Hapa ni Maigizo ya hoja Jf....Mungu angalia waja wako Nyerere tutakukumbuka daima dawamu.
 
Mkuu why balozi wa Beijing hahhh? Anakula raha hatumikii wanaomlipa mshahara au?
Mkuu Raisi JPM akifuta swala la wabunge wa kuteuliwa na manaibu katibu ktk wizara na katibu wa kudumu
Wabunge wa kuteuliwa angelenga Walemavu Walimu Wauuguzi Vijana Watoto kila chama kitoe mwakalishi mmoja au wawili mchezo kwisha tutanufaika na kodi yetu huu utitiri wa wabunge wa kuchaguliwa na kuteuliwa unaifilisi nchi. Ama sivyo awaambie wabunge wa kuteuliwa wajitegemee kwa kila jambo tuone nani atabaki walipwe msharahara kwa mahudhurio bungeni nukta!
Ni kweli wabunge wa Kiteuliwa ni shiiiiiida! Hizo million 12 za mishahara ya kila mbunge wa kuteuliwa zingeelekezwa kwenye mambo ya msingi nina hakika Nchi hii ingekuwa mbali kimaendeleo. Ni wakati sasa tuwaige Serikali ya Rwanda mawaziri wote wamekopeshwa magari hawatumii gari za Serikali na hakuna Taasisi ya Serikali inatumia magari ya bei mbaya kote Rwanda Serikali inatumia gari za kawaida tu zisizo na gharama kubwa. Serikali ya Tanzania ndiyo Serikali inayoongoza Africa yote kwa viongozi kutumia magari ya kifahari.
 
Hujasikia ameamua kuwabana zaidi wafanyabiashara wakubwa plus kufuta safar za vigogo nje ya nchi! Wataka nn tena, kama amekulenga sema

Safari za nje wataenda kwa Pesa zao walizovuna awamu wa Nne pia sasa watabuni mbinu zingine za ufisadi na Safari za nje watajigharamia wenyewe kimya kimya, Magufuli akiweza kuzuia wizi wa pesa za Umma nina hakika pesa nyingi ipo na itajaa mpaka watakosa cha kuzifanyia na kuamua kuwakopesha walala hoi wote.
 
Za escrow zipo zimetegwa, opss washatumia Dubai na ....
 
Hujasikia ameamua kuwabana zaidi wafanyabiashara wakubwa plus kufuta safar za vigogo nje ya nchi! Wataka nn tena, kama amekulenga sema

kwa hiyo vigogo wanasafiri nje kila siku? kuna takwimu maalum zinazoonyesha safari za vigogo kwa siku? vipi waenda kutumbua chunusi, watajengewa hospitali hapa?
 
Kwani Lowasa pia si alisema hayo.. Yeye angezitoa wapi hizo hela??

Elimu ni kitu cha muhimu sana ndio maana leo hii w?tanzania wengi wanashabikia vyama vya siasa kama wanavyo shabikia mpira, Na hatuwezi kupata maendeleo kama hatuna elimu nzuri.
Afya pia ni muhimu sana kwani umaskini unasababishwa na magonja na kukosekana huduma nzuri mahospitalini. Ukiwa mgonjwa leo hii utamaliza akiba yote uliojiwekea na kurudi kwenye umaskini.

Hela zipo nyigi saaaana lakini asilikia kubwa zinaishia kwa mafisadi kwa hiyo kazi ya kwanza inabidi abane na kutokomeza ufisadi. Sasa ndio amenza kazi tuone.

Kule South Africa kila wizara kuna kitengo maalum cha kuratibu matumizi ya wizara na wengi wataalam ni Wazungu pia kule Nigeria baada ya ufisadi kukithiri waliamua kuleta wataalam wa kudhibiti ufisadi toka America wamewaweka kila sekta za Umma kwa kweli wamezeza kudhibiti pesa za umma kiasi kwamba hizo Serikali zina pesa nyingi mpaka hawajui wazifanyie nini, hapa Tanzania Serikali ina pesa nyingi sana Tatizo lipo kwenye mfumo mbovu ambao unatoa mianya ya Ufisadi kila kona, kuna pancha nyingi sana zinazovujisha pesa za Umma pia sheria za wizi wa pesa za umma ni mbovu ndiyo maana watu wengi hawaogopi kuiba pesa za umma.
 
Safari za nje na ile budget ya chai inatosha kabisa kulipia ada zote. Akiongeza na kuondoa mashangingi yote, then posho ya vikao maana wahusika wanalipwa % zaidi kwenye mishahara yao plus misamaha ya kodi basi hadi lap top watanunuliwa 😀😀

Tanzania pesa ipo nyingi tu inatumika kinyume na haki na nyingi inapotelea mifukoni mwa wajanja wachache lakini hakika wakiamua kudhibiti pesa za umma kwa uhakika na umakini kila huduma za muhimu zinaweza kupatikana bure pasipo Tatizo lolote.
 
Tumuache afanye kazi, hii ni siku yake nne tu be positive even if it will take 2 years. Lazima ndoto yake ya elimu bure aitimize.
 
Si ameshafuta Safari zote za nje! Makongamano! Think this despot J kikwete used 50 million USD by only himself plying the world; doing his business! The money is enough to educate our boys and girls!!

By the way Mr. JPM remove this ambassador at the Beijing Embassy!

China wamegharamia uchaguzi wote kwa kuwapa CCM mapesa mengi na huyo balozi ndiyo katengeneza michongo yote Sidhani kama anaweza kumng'oa huko, cha msingi labda awaombe china wampe mbinu za kuthibiti pesa za umma zisiwe zinaibiwa kirahisi rahisi hivi.
 
Mkuu acha dharau unauliza fedha zinatoka wapi??????!!!!!!! Serikali ina vyanzo vingi vya pesa tofauti na tunavyoelewa sisi kwa hiyo kitu cha msingi hapo ni kupokea utekelezaji wa ahadi zake na usihoji fedha imetoka wapi unadhani itakuwa imetoka wapi?????? Wakati wa kampeni alijua fedha zitatoka wapi na ndiyo maana alisema, Yule wa mazingaombwe ya kumaliza matembe nchi nzima naye alijua atapata wapi wakandarasi wa kujenga na kulipwa ili kumaliza matembe yote jamhuri nzima ya Tanzania. Ushauri wangu tumhoji anaposhindwa kutekeleza ahadi na tusihoji anapotimiza ahadi.
Pesa zipo nyingi tu yeye anajua zipo wapi pia akidhibiti wizi wa pesa za umma pesa itapatikana nyingi zaidi mpaka hospital huduma zitakuwa bure.
 
Acheni rais afanye kazi, kwani lowasa aliposema elimu bure mpaka chuo kikuu mliwahi kumuhoji?, acheni zenu
 
Mbona tunasahau haraka hivi? Kwani kuna jipya alilofanya Magufuli hapo kwa kutangaza kuanzia mwakani elimu iwe bure? Si anatekeleza sera mpya ya elimu iliyozinduliwa mwaka jana na tukaambiwa elimu itakuwa bure kuanzia mwakani? Kama hilo halikutiliwa maanani wakati wa bunge la bajeti itakuwa ni uzembe wa wizara na bunge zima.
 
Tunacheza na akili zenu tu. Nafuta ada ila michango mtatoa ili kuendesha shule zenu. Kuna unafuu hapo? Ni ile ile!
 
Tra wanakusanya kodi ndogo sana.wamwambiwa wasipoleta 1,6 trilion kwa mwezi walale mbele hapa kazi tu
 
Mh Rais umetutangazia kuwa elimu itakuwa bure kuanzia January 2016. Lakini hujatueleza kuwa pesa hizo za elimu zinatoka sehemu gani katika bajeti yetu na ukizingatia Bunge lilishapitisha bajeti yetu. Je, zinapunguza pesa kutoka afya? Miundombinu au wapi? Ni kweli umetoa ahadi nyingi za katika ilani ya CCM lakini utekelezaji wa "hapa kazi tu" bila mipango unaweza kuyumbisha maeneo mengine muhimu ya serikali.
Tafadhali angalia usikwame mapema kama vikao vya Ngurudoto.
wabongo hao tabu tupu
 
tatizo la watanzania kila jambo tunaleta siasa. Mtu akihoji serikali anaitwa Mpinzani hivyo watu wanapenda viongozi wapigiwe makofi tu kila wanaloongea . Mtoa hoja kaeleza vizuri sana tena kufatatana na matumizi ya serikali lazima yaidhinishwe na Bunge kinyume cha hapo ni kudanganyana tu na wasiwasi wake ni kuwa bila ya bunge kuidhinisha fedha za kulipia ada . Pia tukumbuke gharama ya elimu sio hiyo ada ya 20,000 au 70,000 kwa olevel na alevel bali kuna gharama kubwa zaidi ya hizo. hivyo wanasiasa wetu lazima wabanwe ili waeleze namna watakavyotekeleza sera ya elimu bure kwa vitendo la sifyo litakuwa changa la macho la kufuta ada na kubakiza michango kwa wazazi kama ilivyokuwa awali. hivyo michango kwa uchache huzidi 300,000 kwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza. sasa kama serikali itafuta ada na kubakiza hiyo michango itakuwa imemsaidia mlalahoi? TUACHE USHABIKI AMASIVYO WOTE TUTAISOMA NAMBA KAMA MLIVYOZOEA KUKEJELI
 
Asipokwambia zitatoka wapi utamzuia mwanao kwenda shule?
 
Back
Top Bottom