Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

Magufuli, Pesa hizi zinatoka wapi?

Hapa kuna dhana ya kutotambua taratibu za serikali na Bunge. Bunge lina mipaka na ndio linalopitisha matumizi. Hivi karibuni Benki ya Dunia imeonya juu ya matumizi makubwa ya serikali na madeni ya wakandarasi kukaa muda mrefu bila kulipwa.
Leo mwingine anaongeza matumizi ya Serikali. Tukumbuke shule zile zilikuwa zikiendeshwa kwa ada na michango ya wanafunzi ambapo hufika kati ya elfu 80 hadi laki moja kwa mwaka. Pesa hizi anazitoa wapi na kwa Bunge lipi?
 
kwanza ada yenyewe ni shilingi 20000 kwa mwaka kwa sekondar za olevel na 70000 kwa wale wa a level...bado kiuhalisia ni gharama ndogo sana...kwa serikali na mbaya zaidi wanafunz hawa walikua hawailipi hii ada kwa wakat...hili linawezekana...ww unalipa ada ya secondary 5m feza boys ndio maana unaona ni gharama sana

feza ni milioni /7.5
 
Kuna umuhimu gani kuwa na vikao vya bajeti vya kupanga pesa za maendeleo na pesa za matumizi ya serikali?

Pesa za kulipia elimu ya bure amempa nani au ni mamlaka ipi imeidhinisha pesa hizo zitumike ?
 
Kama aatatekeleza hata 1/4 ya ahadi zake zote nchi itakua mbali sana na tutamuona mwanamume wa kweli.
bado watu watasema tu,jk alitimiza ahadi karibu zote na bado wanamsema,yeye afanye kwakadri ya uwezo wake tu,binadamu hawanaga shukrani
 
Yaani leo ndo unakumbuka kuuliza hili swali?
Kwahiyo hakuna kuuliza maswali yoyote sasa hivi? "Hapa kazi tu" lazima iendane na taratibu na sheria za nchi. Uchaguzi wa zanzibar ni kiashiria cha kupungua kwa misaada kutoka kwa nchi wahisani. Pesa anazozungumza Magufuli katikati ya bajeti anazitoa wapi? Hiyo kodi ya wafanyabiashara na safari za nje shs ngapi?
 
Wenyewe mnaona waliokuwa wakimuunga mkono lowasa na ahadi yake yaelimu bure ndo haohao sasa wanageuka na kuuliza magufuli atatoa wapi hela na kwa idhini ipi
 
Serikali ina namna nyingi ya ku reshuffle matumizi. Kumbuka Budget ya Rais ilikuwa inaisha wakati mwingine ndani miezi minne tu lakini haikumzuia Kikwete kusafiri.

Jambo lenye neema namna hiyo nani atapinga? Wanaweza kufanya mini budget kabla ya hapo. Ni kitu cha kawaida. Wapinzani hawatakuwa wendawazimu kukataa kitu kama hicho.
 
Mimi nitakujibu si lazima rais.

Mh.Rais amewaambia TRA kwa mfano kusiwe na kusamehe kodi ovyo, kila anayestahili kulipa kodi ni lazima alipe. Hapa peke yake pana pesa nyingi sana.

Rais pia amefuta safari zote za nje zisizo za lazima za viongozi wote.Hapa pia pana fungu kubwa sana. Ukiona jinsi Emirates ilivyokuwa inajaa viongozi, tena business class, utajua kweli TZ ilikuwa shamba la bibi. Nakumbuka pia kwamba Rais ameongelea swala la manunuzi.

Hapa pana swala la kuacha manunuzi na matumizi yasiyo ya lazima na inflating amounts of money paid in terms of taxes,prices of goods and services rendered.

Hapa kwa makusudi kabisa ningeomba serikali itupie macho TRA yenyewe, TBS na TFDA. Hapa pana hela nyingi inayopotea. Hii ina maana pia kubuni vyanzo vipya vya kodi.

Tusisahau pesa itokanayo na madini ikiwemo gas,utalii,sector ya mifugo,fisheries, kilimo nk.Vyote hivi vikisimamiwa vizuri, there is so much money out there. Kwa hiyo kuwapa watoto wetu elimu ya bure sio shida kabisa.
 
Serikali ina namna nyingi ya ku reshuffle matumizi. Kumbuka Budget ya Rais ilikuwa inaisha wakati mwingine ndani miezi minne tu lakini haikumzuia Kikwete kusafiri.

Jambo lenye neema namna hiyo nani atapinga? Wanaweza kufanya mini budget kabla ya hapo. Ni kitu cha kawaida. Wapinzani hawatakuwa wendawazimu kukataa kitu kama hicho.
Hizi ni changamoto za serikali;
1. Kuongezeka kwa budget deficit
2. Madeni mengi ya wakandarasi
3 Hali ya Kisiasa Zanzibar ambayo huenda ikaleta athari za upatikanaji wa msaada kutoka nchi wahisani.
4. Kuteteleka kwa uchumi wa nchi zinazoendelea kutokana na kuimarika kwa nchi zilizoendelea hivyo kupunguza uwekezaji.
Hakuna shida kwa Magufuli kuitekeleza ahadi yake. Je ilikuwa lazima iwe January 2016? Nini kipaumbele hapa, wale kina mama wanaonunua vifaa vya kujifungulia au kufutwa kwa ada? Hii kutafuta headlines si utendaji. Ana miaka mitano au hata kumi, ana haraka gani?
 
Tuache ukigeugeu kaahidi. katekeleza kashatangaza hutaki mpeleke mwanao private school.
 
Mimi nitakujibu si lazima rais.Mh.Rais amewaambia TRA kwa mfano kusiwe na kusamehe kodi ovyo,kila anayestahili kulipa kodi ni lazima alipe.Hapa peke yake pana pesa nyingi sana.Rais pia amefuta safari zote za nje zisizo za lazima za viongozi wote.Hapa pia pana fungu kubwa sana.Ukiona jinsi Emirates ilivyokuwa inajaa viongozi,tena business class,utajua kweli TZ ilikuwa shamba la bibi.Nakumbuka pia kwamba Rais ameongelea swala la manunuzi.Hapa pana swala la kuacha manunuzi na matumizi yasiyo ya lazima na inflating amounts of money paid in terms of taxes,prices of goods and services rendered.Hapa kwa makusudi kabisa ningeomba serikali itupie machoTRA yenyewe, TBS na TFDA.Hapa pana hela nyingi inayopotea.Hii ina maana pia kubuni vyanzo vipya vya kodi.Tusisahau pesa itokanayo na madini ikiwemo gas,utalii,sector ya mifugo,fisheries, kilimo nk.Vyote hivi vikisimamiwa vizuri,there is so much money out there.Kwa hiyo kuwapa watoto wetu elimu ya bure sio shida kabisa.
Naomba ieleweke sina tatizo kwa watoto kusoma bure. Hii ni November na January elimu ni bure. Hayo makusanyo yote uliyotaja mengine yanahitaji mipango na hata kubadilishwa kwa sheria. Mf suala la misamaha ya kodi. Tatizo amekurupuka kudhani ukiahidi leo lazima kesho uanze kutekeleza bila kujua pesa anatoa wapi. Unazungumzia madini, kuna kampuni zinatangaza kupunguza wafanyakazi kutokana na kupungua kwa bei ya dhahabu, kubuni vyanzo vipya; si suala la miezi miwili. Angekuja na hesabu hapa kwa hiyo mipango yake mipya atakusanya kiasi gani na mahitaji ya shule ni kiasi gani. Tumechoka kusikiliza porojo zisizokuwa na evidence. Hizi shule, mambo yatakuwa magumu zaidi. Hao walimu watapata hizo fedha kufidia umbwe litakalojitokeza?
 
Hapa kuna dhana ya kutotambua taratibu za serikali na Bunge. Bunge lina mipaka na ndio linalopitisha matumizi. Hivi karibuni Benki ya Dunia imeonya juu ya matumizi makubwa ya serikali na madeni ya wakandarasi kukaa muda mrefu bila kulipwa.Leo mwingine anaongeza matumizi ya Serikali. Tukumbuke shule zile zilikuwa zikiendeshwa kwa ada na michango ya wanafunzi ambapo hufika kati ya elfu 80 hadi laki moja kwa mwaka. Pesa hizi anazitoa wapi na kwa Bunge lipi?
Jinga kweli wewe, Mkapa hakukosea kuwaita MALOFA na WAPUMBAVU.
 
Wakwepa kodi kama akina mengi na Lowasa hapa ndiyo watachangia wakibanwa vizuri.
 
Back
Top Bottom